OLS
JF-Expert Member
- Oct 12, 2019
- 419
- 666
Mapokezi ya chanjo ya COVID19 nchin sio mazuri, mikoa mingi wana chanjo nyingi zimebaki na watu hawajitokezi kuchanja. Hali hii inataka nchi kujitafakari namna bora ya kuwashawishi wananchi ili wakubaliane na chanjo au waweke ulazima wa kupata chanjo hiyo kwa kuweka vikwazo mbalimbali kama kutopata huduma nk.
Katika hali isiyo ya kawaida nchi inaahidi kuleta tena dozi milioni 2 wakati milioni 1 ya mwanzo bado tunahangaika nayo, inawezekana tunakopeshwa au tunapewa bure au ni sharti la kupata mikopo mingine lakini kama tunatumia fedha za wananchi ni matumizi mabaya kuchukua chanjo hizi kabla ya kuelimisha watu ili zigombaniwe na kuonekana ziko chache watu wazichangamkie.
Ushauri wangu kama tunahisi chanjo ni muhimu kwa nchi, tuanze kwa kuwaelimisha wananchi ili ziwe muhimu kwao, otherwise ni kupoteza rasilimali na nguvu ambazo tungeziweka kwenye mambo yenye muitikio hali ingebadilika.
Katika hali isiyo ya kawaida nchi inaahidi kuleta tena dozi milioni 2 wakati milioni 1 ya mwanzo bado tunahangaika nayo, inawezekana tunakopeshwa au tunapewa bure au ni sharti la kupata mikopo mingine lakini kama tunatumia fedha za wananchi ni matumizi mabaya kuchukua chanjo hizi kabla ya kuelimisha watu ili zigombaniwe na kuonekana ziko chache watu wazichangamkie.
Ushauri wangu kama tunahisi chanjo ni muhimu kwa nchi, tuanze kwa kuwaelimisha wananchi ili ziwe muhimu kwao, otherwise ni kupoteza rasilimali na nguvu ambazo tungeziweka kwenye mambo yenye muitikio hali ingebadilika.