Pongezi nyingi kwenu viongozi wetu Mama Samia na Mheshimiwa Mbowe. Kwa hakika kama taifa mmetutoa kimasomaso.
Mama Samia kauvaa ushujaa kwa kutuondolea aibu taifa hili na kuamua kutuunganisha bila kujali maumivu kokote.
Mheshimiwa Mbowe japo muathirika mkuu wa kadhia hii, kwa maslahi ya taifa kaamua kusamehe mara 7 x 70.
"Nani kama Mh. Mbowe na nani kama Mama Samia, madam president?"
Hata hivyo wapo wale ndugu ambao ije mvua au lije jua, zao ni kukaanga mbuyu tu, na kuwaachia wenye meno watafune.
Watu hawa hawaishi chokochoko uzandiki, fitina, uchonganishi na vyote vya namna hiyo. Hawana furaha na amani, wala maendeleo ya nchi hii.
Tuwatambue wanaohaha kutusambaratisha kama Taifa
Kutwa kucha na vihoja uchwara vyao wakishadadia mifarakano:
CHADEMA ni tawi tiifu la CCM
Freeman Mbowe, kada mtiifu wa CCM aliyepewa uenyekiti CHADEMA
Tuwakane hadharani watu hawa bila kujali itikadi zao.
Tuwakemee hadharani watu hawa kwa maana kwa hakika katu, hawa si wenzetu.
Mama Samia kauvaa ushujaa kwa kutuondolea aibu taifa hili na kuamua kutuunganisha bila kujali maumivu kokote.
Mheshimiwa Mbowe japo muathirika mkuu wa kadhia hii, kwa maslahi ya taifa kaamua kusamehe mara 7 x 70.
"Nani kama Mh. Mbowe na nani kama Mama Samia, madam president?"
Hata hivyo wapo wale ndugu ambao ije mvua au lije jua, zao ni kukaanga mbuyu tu, na kuwaachia wenye meno watafune.
Watu hawa hawaishi chokochoko uzandiki, fitina, uchonganishi na vyote vya namna hiyo. Hawana furaha na amani, wala maendeleo ya nchi hii.
Tuwatambue wanaohaha kutusambaratisha kama Taifa
Kutwa kucha na vihoja uchwara vyao wakishadadia mifarakano:
CHADEMA ni tawi tiifu la CCM
Freeman Mbowe, kada mtiifu wa CCM aliyepewa uenyekiti CHADEMA
Tuwakane hadharani watu hawa bila kujali itikadi zao.
Tuwakemee hadharani watu hawa kwa maana kwa hakika katu, hawa si wenzetu.