Kuacha Utumishi wa Umma ukiwa unadaiwa na Benki

Dodoma moja

JF-Expert Member
Jan 3, 2014
307
177
Wasaalam wakuu wa GT naamini mko salama na mnaendelea kupambana na majukumu ya kujiingizia kipato.

Kama kichwa cha habari kinavyoeleza, mimi ni Mtumishi wa Umma ambaye natarajia ndani ya muda mfupi ni step down kwenye Utumishi wa Umma kutokana na kukosa muda wa kufanya mambo yangu binafsi ya kimaisha ambayo naamini kama nitayasimamia vizuri na kuonyesha juhudi kwenye kazi yataniongezea kipato kulinganisha na hiki ninachokipata sasa kwenye utumishi wa umma.

Mambo ni mengi lakini kubwa ni kwamba utumishi wa umma umenifanya nikose uhuru lakini pia ni kazi zenye fitina, manyanyaso mengi na kunyenyekea watu na kwa nature huwa sina tabia ya kumnyenyekea mtu au kujipendekeza kwa mtu hilo kwangu ni mwiko.

Hivyo ili kuyaepuka hayo nimeamua kuachana na kazi ingawa najua nje ya ajira kuna changamoto nyingi lakini nitapambana nazo ikiwa ni njia ya kutafuta uhuru wa kujiamulia mambo yangu mwenyewe na si kupangiwa na mtu hivyo nipo tayari nasema nipo tayari narudia tena nipo tayari ila changamoto iliyonifanya nililete suala hili JF ni kupata uzoefu kwa watu walioachana na utumishi wa umma wakiwa wanadaiwa na Benki kutokana na mikopo ya watumishi.

Je, nini kitatokea endapo nitaamua kuondoka angali bado nadaiwa maana kwa sasa nina mkopo na Benki ambao utamalizika baada ya miaka 3.

Asanteni. Naombeni mawazo yenu wakuu lakini nitoe tahadhari naomba yawe mawazo ya kujenga kama huna la kushauri unaweza kupita kimya kimya si lazima ukoment chochote.
 
We acha tu kazi mikopo ya watumishi ina bima, au watasubiri pensheni yako wachukue chao 2040 huko!
 
Mkuu,Mkopo itabidi uulipe tu si huko mtaani utakuwa unatengeneza pesa?au wewe ni mrushi tapeli?Usipolipa utakosa baraka.Kuhusu kutopenda majungua kuamrishwa na kunyenyekea hio iko kila mahali ili utoboe lazima ukubali kuonekana fala sometimes.

So kama unayakimbia hayo huko ili uje huku basi huku yako mengi tena unayapata na pesa hupati tofauti na huko mshahara unaingia kila mwezi.

Ila kama unataka kujua nini cha kufanya basi tuwasiliana PM kwa ushauri zaidi maana unataka kufanya kosa wanalotaka kufanya watu wengi halafu wanakuja kusema wamelogwa kumbe ni upuuzi tu.
 
Nakushauri ukwapue mkopo mwingine ndo uache kazi, mdhamini wako ni serikali hivyo wataendelea kukata mshahara... hongera kwa kuamka utumwani.
 
Usitake kuniambia Motivational speaker's walivyokushauri uache kazi ili upate muda wa kufanya mambo yako walisahau kukwambia kuwa deni ni lazima ulilipe ukiacha kazi? Hilo ni deni mkuu itabidi ulilipe tu rejea mkataba
 
Usitake kuniambia Motivational speaker's walivyokushauri uache kazi ili upate muda wa kufanya mambo yako walisahau kukwambia kuwa deni ni lazima ulilipe ukiacha kazi? Hilo ni deni mkuu itabidi ulilipe tu rejea mkataba
Kila kitu hadi ushauriwe na watu ndio mawazo yako hayo? Wengine hatuna hizo mambo tunaamua mambo yetu wenyewe na hata hili ni maamuzi yangu binafsi baada ya kukaaa na kufikiria kwa makini hivyo sijashauriwa na mtu
 
Back
Top Bottom