Kuabudu katika Altare ya Wazungu

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,777
41,071
Kwanini tunapenda kuabudu na kusujudu kwenye altare ya watu weupe? Kila kitu kilicho kizuri na cha kuvutia twakiita hicho ni cha "kizungu"! Imefikia wakati kuwa tunashindwa kusikilizana sisi wenyewe hadi mzungu aje atuambie ndio tunasikiliza. Mswahili mwenzako akisema "shuleni zenu zina hali mbaya" tunadhania hana mpango, ila akija mzungu na kusema kitu hicho hicho.. tunapiga magoti na kusema "ni kweli Mr. Johnson!"

Hatuwezi kuendelea mpaka sisi wenyewe tuanze kujiamini na kuona kuwa na sisi tunastahili vitu vizuri. Barabara nzuri si za Kizungu.. shule nzuri si za kizungu.. nyumba yenye maji na umeme, televisheni na bustani nzuri si ya kizungu!! Hivyo vyote vyaweza kuwa vya kiafrika!! Hata makazini, semina ikiandeshwa na mswahili basi wala hatuitilii maanani ila akija Miss Smith na kasemina kake uchwara, au warsha basi wote tunafungua masikio na kusikiliza... kisa na mkasa ati kwa vile yeye ni mzungu!!

Sipendi tena sitaki kusikia kuwa Waswahili hawana mawazo mazuri au hawastahili vitu vizuri!
 
Mwafrika bila mzungu hana cha kujivunia na wala si lolote kila kitu anamtegemea mzungu.

Hata walioiba pesa ya Tegeta-escrow, bila Mzungu kutia mkono, wangeendelea kupeta bila ya hata kusutwa kwa kidole cha shahada.
Chenji ya Rada, bila Mzungu, wajanja wangeifaidi peke yao bila hata kurudishiwa ile kidogo ya "Madaftari".
 
Back
Top Bottom