Ku nani tanzania!!

KAMSOPI

New Member
Jan 19, 2011
1
0
Matukio ya hivi karibuni nchini hayapaswi kufumbiwa macho ili kulinda mustakabali wa nchi yetu..

.Tumeshuhudia rushwa ikitawala mchakato mzima wa uchaguzi mkuu
.Tumeshuhudia malalamiko ya wizi wa kura
.Tumeshuhudia baadhi ya wagombea ubunge na urais wakilalamikia uchakachuliwaji wa kura
.Tunashuhudia wafuasi wa Chadema wakipambana na polisi Arusha, na watatu kuuawa kwa kila kinachodaiwa 'kuzima njama za kuteka kituo kikuu cha polisi'
. Na juu ya yote tunaona majibishano ya viongozi wa dini kuhusu kuhusu mauaji ya arusha.

Wakati hayo yote yakifanyika najiuliza matendo hayo ni kudhihirisha kukomaa kwa demokrasia nchini, ama ni dalili za mgogoro mkubwa wa kijamii inayoinyemelea nchi! maana hali kama hii ikiachwa kushamiri inaweza kumomonyoa mshikamano wa nchi!

Ama matukio hayo ni kiashiria kukithiri kwa dhulma, ulafi, na ufisadi ambao unazidi kupanua mipaka ya wenye nacho na wasio nacho?

Tutafakari kwa pamoja.
 
Matukio ya hivi karibuni nchini hayapaswi kufumbiwa macho ili kulinda mustakabali wa nchi yetu..

.Tumeshuhudia rushwa ikitawala mchakato mzima wa uchaguzi mkuu
.Tumeshuhudia malalamiko ya wizi wa kura
.Tumeshuhudia baadhi ya wagombea ubunge na urais wakilalamikia uchakachuliwaji wa kura
.Tunashuhudia wafuasi wa Chadema wakipambana na polisi Arusha, na watatu kuuawa kwa kila kinachodaiwa 'kuzima njama za kuteka kituo kikuu cha polisi'
. Na juu ya yote tunaona majibishano ya viongozi wa dini kuhusu kuhusu mauaji ya arusha.

Wakati hayo yote yakifanyika najiuliza matendo hayo ni kudhihirisha kukomaa kwa demokrasia nchini, ama ni dalili za mgogoro mkubwa wa kijamii inayoinyemelea nchi! maana hali kama hii ikiachwa kushamiri inaweza kumomonyoa mshikamano wa nchi!

Ama matukio hayo ni kiashiria kukithiri kwa dhulma, ulafi, na ufisadi ambao unazidi kupanua mipaka ya wenye nacho na wasio nacho?

Tutafakari kwa pamoja.

Hapa penye nyekundu ndo shida kubwa
 
Back
Top Bottom