KRA vs TRA: Kwanini Kenya inakusanya kodi mara 3 ya Tanzania

Upo sahihi lakini hata hicho kiwango TRA inakusanya .. unakusanya kutoka base ndogo sana kwa sababu unatoza kodi kubwa.

Mfano

KRA: Capital Gain Tax ni 5%
TRA : Capital Gain Tax ni 10%

Ndio maana tunasema makusanyo ya TRA yamebeba risk kwa sababu yapo kisiasa.

Kama TRA watatoza kodi sahihi kwa wafanya biashara maana yake hatuwezi kufikia hata kiwango cha sasa hadi watakapo kuza base ya walipa kodi na kufikia walau 80% ya wanao stahili kulipa kodi.

Kuna maeneo mengi sana ambayo hayaja guswa na kama yakiguswa TRA inaweza kuwa na nafasi kubwa sana katika maendeleo ya nchi hii.
Mimi wasiwasi wangu ni neno "kisiasa", sijui hili neno linaingiaje. Tatizo kama ulilosema la kuwa na base ndogo la walipa kodi, hilo ndio tatizo kubwa la TRA ambalo Magufuli amekuwa akiwapigia sana kelele TRA, amekwenda mbali hadi kuanzisha vitambulisho vya wamachinga na kuanzisha Masoko ya madini ili kupanua"tax base".

Kushindwa kwa TRA kupanuo tax base ndiko kunakowafanya kutoza kodi kubwa Kama hiyo uliyosema, sasa unaposema wanafanya kazi kisiasa unamaanisha nini?. Lakini tusisahau kwamba wananchi wakenya ndio raia wanaolipishwa kodi nyingi kuliko raia wa nchi yoyote hapa mashariki na kusini mwa Afrika.
 
Mkuu naamini unajua kusoma.. nenda kwenye portal ya KRA ukiona hayo unayo yasema ndio uje ulete huo ushahidi.

Nadhani tujikike kwenye sababu kwanini makusanyo TRA ni madogo.
Zimejumuisha maduuli yote ya serikali kutoka maeneo kama national parks, wizara ya kilimo, wizara ya nishati na agencies nyingine za serikali ambayo mifumo yake kikodi haiintercept na TRA?

Ya Kenya ulioweka hapo ukasema imetuzidi mara 3 imejumuisha hayo yote, sasa na kuuliza na ya Tanzania imejumuisha?
 
Nimekuwa nikijizuia kuchangia katika Jukwaa hili kwani limejaa mihemuko na 'ushabiki maandazi', watu hawaoni taabu kukutukana eti tu kwa kuwa una mtazamo tofauti na wao. Kwa kweli huu ni mjadala mzuri sana na kwa kiasi kikubwa wachangiaji wengi wamekuwa fair isipokuwa wachache (wale wanazi wa Tz vs Ke). Hata hivyo, tukubali au tukatae, TRA ingeweza kufanya vizuri zaidi kama ingeepukana na hili tatizo la kimfumo na rushwa iliyotamalaki miongoni mwa wafanyakazi wake...

Nakumbuka Rais Magufuli alipokutana na wafanyabiashara Desemba 10, 2018 aliiagiza TRA kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo kutengeneza mazingira ya ulipaji kodi, kupitia upya viwango vya kodi na taasisi za biashara na uwekezaji ikiwemo TPA na TIC kuondoa urasimu katika shughuli zao. Alisema kuwa licha ya takwimu kuonyesha kuwa uchumi unakua kwa kasi na mfumuko wa bei kushuka mpaka asilimia tatu, bado ukusanyaji wa mapato hauridhishi na jitihada zaidi zinahitajika kuweka mazingira wezeshi kwa wananchi kulipa kodi ili kukamilisha miradi ya maendeleo kwa wakati.

Baadhi ya sababu zilizobainishwa kusababisha kutokuwa na mapato makubwa ya kodi (japo hadi leo hazijafanyiwa kazi) ni:

1. Kuw
a na mapungufu yanayojitokeza katika mifumo na taratibu za ukusanyaji kodi ikiwemo wigo mdogo wa kulipa kodi usioendana na idadi ya Watanzania.

2. Vyanzo vya ukusanyaji kodi havitumiwi vizuri jambo linalotoa mwanya kwa wafanyabiashara kukwepa kodi wakishirikiana na baadhi ya wafanyakazi wa TRA.

3. Japo Tanzania ina idadi kubwa ya watu kuliko nchi nyingine za Afrika Mashariki, lakini ina dadi ya walipa kodi wapatao milioni 2.27 tu ambapo uwiano wa kodi ukilinganisha na Pato la Taifa (GDP) ni asilimia 12.8.

4. Taxi base yetu ya makusanyo ni ndogo mno, tuko watu milioni 55, walipa kodi ni milioni 2.2 wakati nchi kama Msumbiji wako milioni 27, walipa kodi ni milioni 5.3!

Nadhani wakati mwingine tunatakiwa tuache mahaba na ushabiki wa Tz vs Ke kama kweli tunahitaji kuisaidia nchi yetu kupiga hatua zaidi...
 
Kaka katika kitu kinachomuumiza kichwa Magufuli ni TRA na Wizara ya mambo ya ndani na BoT, wewe mwenyewe umemsikia mara kadhaa Magufuli akichanganyikiwa kutokana na kutoridhishwa na utendaji wa TRA, katika kipindi cha uongozi wake wa miaka 5. amebadilisha makamishina wakuu 5, wastani wa kamishna mkuu mmoja kila mwaka , hii ni dalili kwamba hakuna utendaji mzuri TRA.

Kaka tatizo la TRA lipo kwa wetendaji kuwa na uwezo mdogo, kukosa ubunifu na kutokuwepo na uongozi imara, bado wafanyakazi wengi wa TRA ni mangi meza, sidhani Kama kuna siasa.
Hapana JPM hana basic knowledge ya uchumi, yeye ndo ana demoralize watumishi wa TRA, mtaalamu wa uchumi huongozwa na economic statistics na data sio na political statements kama za JPM haiwezakani kubadili makamissioner watano kwa mda mfupi hivo bila hata annual data report ya kukuongoza
 
Mkuu naamini unajua kusoma.. nenda kwenye portal ya KRA ukiona hayo unayo yasema ndio uje ulete huo ushahidi.

Nadhani tujikike kwenye sababu kwanini makusanyo TRA ni madogo.
Ndio nakuambia ya Kenya uliyoweka ipo sum up the whole Central Bank receipts from other nonKRA peripherals + KRA receipts vipi ya Tanzania uliyoweka imejumuisha hivyo vitu?

Iliyojumuisha hii nimekuwekea bado unaonekana mbishi

2487631_tapatalk_1584017659452.jpeg
 
Well said
Nimekuwa nikijizuia kuchangia katika Jukwaa hili kwani limejaa mihemuko na 'ushabiki maandazi', watu hawaoni taabu kukutukana eti tu kwa kuwa una mtazamo tofauti na wao. Kwa kweli huu ni mjadala mzuri sana na kwa kiasi kikubwa wachangiaji wengi wamekuwa fair isipokuwa wachache (wale wanazi wa Tz vs Ke). Hata hivyo, tukubali au tukatae, TRA ingeweza kufanya vizuri zaidi kama ingeepukana na hili tatizo la kimfumo na rushwa iliyotamalaki miongoni mwa wafanyakazi wake...

Nakumbuka Rais Magufuli alipokutana na wafanyabiashara Desemba 10, 2018 aliiagiza TRA kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo kutengeneza mazingira ya ulipaji kodi, kupitia upya viwango vya kodi na taasisi za biashara na uwekezaji ikiwemo TPA na TIC kuondoa urasimu katika shughuli zao. Alisema kuwa licha ya takwimu kuonyesha kuwa uchumi unakua kwa kasi na mfumuko wa bei kushuka mpaka asilimia tatu, bado ukusanyaji wa mapato hauridhishi na jitihada zaidi zinahitajika kuweka mazingira wezeshi kwa wananchi kulipa kodi ili kukamilisha miradi ya maendeleo kwa wakati.

Baadhi ya sababu zilizobainishwa kusababisha kutokuwa na mapato makubwa ya kodi (japo hadi leo hazijafanyiwa kazi) ni:

1. Kuw
a na mapungufu yanayojitokeza katika mifumo na taratibu za ukusanyaji kodi ikiwemo wigo mdogo wa kulipa kodi usioendana na idadi ya Watanzania.

2. Vyanzo vya ukusanyaji kodi havitumiwi vizuri jambo linalotoa mwanya kwa wafanyabiashara kukwepa kodi wakishirikiana na baadhi ya wafanyakazi wa TRA.

3. Japo Tanzania ina idadi kubwa ya watu kuliko nchi nyingine za Afrika Mashariki, lakini ina dadi ya walipa kodi wapatao milioni 2.27 tu ambapo uwiano wa kodi ukilinganisha na Pato la Taifa (GDP) ni asilimia 12.8.

4. Taxi base yetu ya makusanyo ni ndogo mno, tuko watu milioni 55, walipa kodi ni milioni 2.2 wakati nchi kama Msumbiji wako milioni 27, walipa kodi ni milioni 5.3!

Nadhani wakati mwingine tunatakiwa tuache mahaba na ushabiki wa Tz vs Ke kama kweli tunahitaji kuisaidia nchi yetu kupiga hatua zaidi...
 
Nadhani yule CG mwa mwisho wa awamu ya JK angeweza kufanya vizuri zaidi kutokana na uzoefu katika biashara na elimu nzuri.

Hawa wa sasa wamechukuliwa vyuoni theory nyingi na waoga kwa wana siasa..

Hapana JPM hana basic knowledge ya uchumi, yeye ndo ana demoralize watumishi wa TRA, mtaalamu wa uchumi huongozwa na economic statistics na data sio na political statements kama za JPM haiwezakani kubadili makamissioner watano kwa mda mfupi hivo bila hata annual data report ya kukuongoza
 
Hivi mirahaba na kodi za madini hukusanywa na TRA au huenda directly Hazina? maana hili gap la kuzidishwa mara tatu ni kubwa!
Kodi ni TRA ila mirahaba ni hazina, Hilo gap sio kubwa sana kama utalinganisha na % ya GDP, Kenya wanakusanya 2% juu ya Tanzania, sasa kwasababu ya ukubwa wa GDP yao ndio pesa inaonekana ni nyingi.

Sisi Tanzania tunakusanya 15% ya GDP yetu ya $64B, Kenya wanakusanya 17% ya GDP yao, ukipiga hesabu ndio utaona hiyo tofauti.

Hata Tanza tukikusanya 17% ya GDP yetu na Kenya wakikusanya 17% ya GDP yao, bado gap itaendelea kuonekana. Ili kupunguza hilo gap, lazima Tanzania tupunguza gap la GDP na gap la ukusanyaji kodi, au tukusanye 23% ya GDP yetu na Kenya waendelee kukusanya 17% au chini ya hapo.
 
Tabutupu,

Bora nisilipe unalipa pesa inaenda kufaidisha maCCM si Bora tuwe tunatafutana tu kwa lazima, mikodi yenyewe mikubwa na ya kubambikiwa.

At the same time Tzn Kuna watu wengi kuliko Kenya, eti uchumi wa kati.
 
Kumbe JPM kwa miaka 5 ameongeza 4% kutoka pale tulipo achwa na JK, pamoja namajigambo bado makusanyo ya TRA yako chini yakiwango, kazi nimoja kwa CCM tenganisha siasa na uchumi wa nchi ndomtaweza kuona performance ya sector ya fedha
Una matatizo yako binafsi na CCM hatuna la kukusaidia.
 
Tabutupu,


Unashindwa kuelewa:

Kenya uzalishaji wao ni zaidi ya mara 3 ya Tanzania.

Obviously kodi lazima iwe mara tatu ya Tanzania.

Tanzania ni li-welfare state,kila kitu serikali eti inatoa bure wakati serikali haina hela hivyo Wananchi hawafanyi kazi seriously maana kila kitu eti serikali inatoa free.

Serikali ndio tatizo, huwezi ongeza uzalishaji kwenye nchi kwa kutoa vitu vya bure,vitu vya bure vina incentivize watu kutofanya kazi maana vitu ni vya bure!Idadi ya watu wahitaji vya bure itaongeza siku hadi siku hua haipungui maana hamna mtu anakataa vya bure iwe elimu,matibabu,etc!

Kitakacho okoa Tanzania ni Capitalism ya kweli.

Kama cure for poverty ni wealth,then lets talk about uzalishaji na sio hii legalized theft inayofanya serikali ya Tanzania kutoka kwa wazalishaji wachache 15% na kugawa kwa poor 75% ya wananchi for free.

Asante
 
Je population ya Tz ni ngapi?

Walipa kodi ni ngapi?

Kwanini tuna pupulation kubwa lakini GDP ndogo?

Huoni kama mfumo mbovu wa kodi unachangia kwa kiasi fulani ukuaji wa GDP?

Correct me if am wrong..
Kodi ni TRA ila mirahaba ni hazina, Hilo gap sio kubwa sana kama utalinganisha na % ya GDP, Kenya wanakusanya 2% juu ya Tanzania, sasa kwasababu ya ukubwa wa GDP yao ndio pesa inaonekana ni nyingi.

Sisi Tanzania tunakusanya 15% ya GDP yetu ya $64B, Kenya wanakusanya 17% ya GDP yao, ukipiga hesabu ndio utaona hiyo tofauti.

Hata Tanza tukikusanya 17% ya GDP yetu na Kenya wakikusanya 17% ya GDP yao, bado gap itaendelea kuonekana. Ili kupunguza hilo gap, lazima Tanzania tupunguza gap la GDP na gap la ukusanyaji kodi, au tukusanye 23% ya GDP yetu na Kenya waendelee kukusanya 17% au chini ya hapo.
 
Pamoja na mengi ninayokubaliana nawe pia suala la Tax base hasa ndio chimbuko la utofauti huu unaouona.

Tanzania taxbase ni ndogo sana na hii inatokana na uchache wa uwekezaji katika sekta nyingi za kibiashara kama viwanda vya kati na vikubwa.

Tukiweza kuifikia Kenya kiuwekezaji hasa kwenye sekta za viwanda na biashara zenye mchango mkubwa na multiplier effect kubwa kwenye uchumi bila shaka utaona utofauti huo unapungua ama kuwapita Kenya kimakusanyo ya Kodi.

Hapa nimezungumzia uzoefu wangu mdogo katika sekta ya kodi na Fiscal policies za nchi hii.
Tzn ya viwanda vya cherehani kwani havilipi kodi? Trade liberalization na kodi ndogo ili kupata walipa kodi wengi ndio jibu,alianza Kikwete huyu mjamaa karudisha nchi nyuma miaka ya Nyerere,ndio kusema gold price zikicolapse na sekta ya utalii kubuma nchi inacolapse na lawama zote kwa beberu wakati ni ushamba wa kijamaa unaua sekta binafsi inategemea nini
 
Mr zero brain hiyo mi bajeti siyo kodi hizo..
Au kwenye akili kisoda yako unafikiri mapato yote ya serikali ni TRA inakusanya? Yapo mapato mengi tu ya serikali ambayo hayapiti TRA

🚮🚮🚮🚮 Zero brain
 
Nimekuwa nikijizuia kuchangia katika Jukwaa hili kwani limejaa mihemuko na 'ushabiki maandazi', watu hawaoni taabu kukutukana eti tu kwa kuwa una mtazamo tofauti na wao. Kwa kweli huu ni mjadala mzuri sana na kwa kiasi kikubwa wachangiaji wengi wamekuwa fair isipokuwa wachache (wale wanazi wa Tz vs Ke). Hata hivyo, tukubali au tukatae, TRA ingeweza kufanya vizuri zaidi kama ingeepukana na hili tatizo la kimfumo na rushwa iliyotamalaki miongoni mwa wafanyakazi wake.

Nakumbuka Rais Magufuli alipokutana na wafanyabiashara Desemba 10, 2018 aliiagiza TRA kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo kutengeneza mazingira ya ulipaji kodi, kupitia upya viwango vya kodi na taasisi za biashara na uwekezaji ikiwemo TPA na TIC kuondoa urasimu katika shughuli zao. Alisema kuwa licha ya takwimu kuonyesha kuwa uchumi unakua kwa kasi na mfumuko wa bei kushuka mpaka asilimia tatu, bado ukusanyaji wa mapato hauridhishi na jitihada zaidi zinahitajika kuweka mazingira wezeshi kwa wananchi kulipa kodi ili kukamilisha miradi ya maendeleo kwa wakati.

Baadhi ya sababu zilizobainishwa kusababisha kutokuwa na mapato makubwa ya kodi (japo hadi leo hazijafanyiwa kazi) ni:

1. Kuw
a na mapungufu yanayojitokeza katika mifumo na taratibu za ukusanyaji kodi ikiwemo wigo mdogo wa kulipa kodi usioendana na idadi ya Watanzania.

2. Vyanzo vya ukusanyaji kodi havitumiwi vizuri jambo linalotoa mwanya kwa wafanyabiashara kukwepa kodi wakishirikiana na baadhi ya wafanyakazi wa TRA.

3. Japo Tanzania ina idadi kubwa ya watu kuliko nchi nyingine za Afrika Mashariki, lakini ina dadi ya walipa kodi wapatao milioni 2.27 tu ambapo uwiano wa kodi ukilinganisha na Pato la Taifa (GDP) ni asilimia 12.8.

4. Taxi base yetu ya makusanyo ni ndogo mno, tuko watu milioni 55, walipa kodi ni milioni 2.2 wakati nchi kama Msumbiji wako milioni 27, walipa kodi ni milioni 5.3!

Nadhani wakati mwingine tunatakiwa tuache mahaba na ushabiki wa Tz vs Ke kama kweli tunahitaji kuisaidia nchi yetu kupiga hatua zaidi...
Kaka umemaliza kila kitu, huo ndio ukweli.
 
Kuna vitu vinatia aibu.. mtu unatoka huko unatafuta ulipe kodi haraka unadhani kuna namna rahisi unakutana na menu ambazo hazina hata mashika.

Kuna tatizo kwa wanao ongoza kitengo cha ICT TRA.. inawezekana yupo busy sana kiasi kwamba vitu vidogo kama hivi hajawahi kuwaza kwamba vina impact kubwa sana kwenye kazi za TRA.

TRA inahitaji mabadiriko makubwa kwenye matumizi ya tehama na siku wakilijua hilo watashangaa kazi zao zilivyo rahisi na makusanyo yatakavyo kua kwa haraka japo tunatambua tehama itaua mapato yao binafsi yale ya pembeni.

TRA ICT ndio tupa kule, jaribu ujikute na tatizo linalohusu kukaa nao kikao utachoka, kuna kipindi Magufuli alifuata ICT wa Rwanda wawasaidie pale, sijui iliishaje. Wana taaluma TEHAMA Tanzania walipiga makelele sana kwa kupuuzwa.
 
Budget hutokana na nini? Wacha kuita watu zero brain wakati wewe kichwani hewa! FYI nchi kama Kunyaland haina tax structure kama yetu maana si mining country!
Mkuu watu hata Hawajui wanajadili nini hapa? Mada ipo awkward kichizi na watu wanatiririka kwenye utopolo. 😂
 
Geza ulole na wewe pia.. basi bongo ni shida, anyway tufanye TRA kinara wa kukusanya kodi africa.
Budget hutokana na nini? Wacha kuita watu zero brain wakati wewe kichwani hewa! FYI nchi kama Kunyaland haina tax structure kama yetu maana si mining country!
 
Back
Top Bottom