Kova: Ongezeko la Maandamano nchini ni matokeo ya viongozi kutowajibika

muhosni

JF-Expert Member
Feb 12, 2011
1,108
152
Katika mahojiano na TBC radio saa 1.30 asubuhi leo akifafanua sababu za kuzuia maandamano ya waislamu kupinga uvamizi wa Libya. Mtangazaji akataka maoni yake kuhusu ongezeko la maandamano tz.

Amesema ongezeko la maandamano nchini linasababishwa na viongozi wengi wa serikali kutokuwajibika na kuwashirikisha wananchi kikamilifu katika masuala ya jamii. Ametoa mfano kwamba kama Umeme umekatika watumiaji wana haki ya kupewa taarifa nini kimesababisha, nini kinafanyika na tatizo litaisha lini.

Kwamba wanayosema viongozi yawe ya kweli na yatokee kweli. Kama kuna mabadiliko wananchi wajulishwe na washirikishwe kutafuta ufumbuzi. Kwamba wananchi hawataandamana huku wakilijua tatizo kwa kina na wakiwa bize wakilitatua. Kwamba wananchi wakishirikishwa wana uwezo mkubwa wa kutatua matatizo kuliko hata viongozi
 
Katika mahojiano na TBC radio saa 1.30 asubuhi leo akifafanua sababu za kuzuia maandamano ya waislamu kupinga uvamizi wa Libya. Mtangazaji akataka maoni yake kuhusu ongezeko la maandamano tz.

Amesema ongezeko la maandamano nchini linasababishwa na viongozi wengi wa serikali kutokuwajibika na kuwashirikisha wananchi kikamilifu katika masuala ya jamii. Ametoa mfano kwamba kama Umeme umekatika watumiaji wana haki ya kupewa taarifa nini kimesababisha, nini kinafanyika na tatizo litaisha lini.

Kwamba wanayosema viongozi yawe ya kweli na yatokee kweli. Kama kuna mabadiliko wananchi wajulishwe na washirikishwe kutafuta ufumbuzi. Kwamba wananchi hawataandamana huku wakilijua tatizo kwa kina na wakiwa bize wakilitatua. Kwamba wananchi wakishirikishwa wana uwezo mkubwa wa kutatua matatizo kuliko hata viongozi
 
MAFISADI HUKATISHA TAMAA WAFANYAKAZI WENYE VYEO VYA CHINI SERIKALINI,
KUSABABISHA UTENDAJI DUNI NA HATIMAYE KUGEUKA PETROLI YA WANANCHI
KUANDAMANIA KODI ZISIZOLETA TIJA HUDUMA ZA JAMII


Haswaaa kazi siku hizi maofisini hamna kitu na watu kujikatia tu tamaa bora siku imepita!!!

Hakika wafanyakazi wengi hivi sasa ni wataalam wa kuning'iniza koti kwenye kiti na kwenda kupiga gumzo na walinzi nje juu ya siasa za mara fisadi fulani kaopoa donge nono kweli hazina au benki kuu au wakati mwingine ni siasa za CHADEMA kupanda chati nchini huku kazi ikilala.

Lakini, pamoja na yote, wengi huku mitaani tunajua fika kwamba wafanyazi hasa wa serikalini wamekatishwa sana tamaa maana UFISADI mnono mnono wanazipitisha wenyewe kwa mabilioni lakini wao huachwa nche kila mara kwenye mgao kana kwamba wao hawa familia wala midomo kuhitaji kula

Ukiona mambo yako hivi basi ndipo mtu kama Kikwete anastahili kuonyesha uzalendo wake kwa nchi kwa kurudisha uongozi uliochakachuliwa kwa wananchi ili nchi ipate kuendelea tena kwa misingi mipya. Jamani tukataeni UFISADI ni mdudu mbaya sana inayoelekeza mawazo ya watu kula vizuri bila kufanya kazi.

Maandamano mbeele kwambeeele!!
 
Kama amesema hivyo kweli, atakuwa ameamka vizuri leo! Au machale yamemcheza??? Maana polisi wengi hupenda kujikomba kwa viongozi.
 
Katika siku mzee wa inteligensia (kamanda Kova) ameongea la maana ni leo!!!!

Rais anakimbia hawezi face wananchi panapokuwa na tatizo
Mawaziri wanakimbia hawezi face wananchi panapokuja na tatizo
e.t.c wanakimbia hawawezi face wananchi panapokuwa na tatizo

Matokeo ni kudai haki kwa maandamano
 
kama kayasema hayo,basi nadhani anajuwa nini kitafuata baada ya kauli yake,ni kustaaaaaafishwa kwa manufaa ya uma,heheheheh
 
Maandamano yenyewe yawe ya maana basi. Kuandamana kwa kuwa Ghadafi anapigwa ili asiendelee kuua watu wake kwa kuwazuia kuandamana haiingii akilini. Hosni Mubarak alikubali yaishe, Yule wa Tunisia vivyo hivyo, kwa nini sio Ghadafi?
 
Mr Kova knows that cheating is sin but sometimes cunning is absolute bravery. Bravo Kova
 
Hata mm sioni sbb ya maandamano yao,wakutane tu hapo biafra then waanze "kulalamika" jamaa huwa wanajazba hawa,kova is one of the good kamanda
 
kama amsema hivyo basi huyu kamanda anaona mbali sana,ni kwamba anakwenda na wakati,hongera sana mzee
 
inabidi ajenge uhusiano mzuri na chama kipya cha serikali mpya ijayo ya CHADEMA.anasoma nyakati.hapo sawa.
 
Maelezo ya Kova yana maana kubwa sana hasa ukizingatia matamshi ya awali ya baadhi ya viongozi..

Kama serikali inawajibika na utekelezaji wake unaonekana wazi sidhani kama wananchi wanaweza kuandamana bila sababu ya msingi..

Nakumbuka mwezi October wananchi walitangaziwa kuharibika kwa mitambo yya IPTL na matengenezo yake yangechua miezi miwili..
Taarifa hii haikuwa sahihi na hata baada ya kushindwa kutengeteza ndani aya muda huo, serikali haikuwajulisha wananchi badala yake wakarudi na swala la Dowans..Ikiwa Dowans ndio sababu ya mgao na solution ya matatizo, sii upungufu unaotokana na mitambo ya IPTL..

Maisha magumu na mfumko wa bei haukupewa maelezo ya kina na hotuba zote za rais au viongozi chini yake...
Nakumbuika mara ya mwisho rais alizunguimzia hili mwaka juzi kutokana na hali ya kiuchumi duniani wakati haikuwa na athari yeyote kwa nchi kama zetu ambao hatukopeshi wala hatuna mfumo kama wa nchi zilizoathirika..

Ilitakiwa maelezo ya kina kila mwezi na rais na kila week na msemaji wa Ikulu kuwaambia wananchi hali halisi na pia kupokea maswali na mapendekezo yao..

Kama JK atachukua utaratibu huu wa kuzunguumzia maswala ya anayolihusu Taifa zima kwa wakati huo na sii changamoto za kiti chake na serikali kutoka upinzani...maandamano ya nini?

Wananchi wanataka answers kuhusiana na ahadi zake, wapi wamefikia na wapi wanakwenda na kwa kasi gani kutokana na changamoto za kiuchumi..

Hakika maandamano yamesaidia sana kuwaumbua viongozi wengi sana na nadhani serikali ya JK ingetumia nafasi ya maandamano haya kujua upana wa kero za wananchi ili wapate kujua makosa yametokea wapi na who are responsible..badala ya kuyaona maandamano yana nia ya kuiangusha serikali yake..

Sukari na mali kibao zinafichwa ili kupandisha bei makusudi kabisa na kibaya zaidi serikali inatakiwa kutaza kwa umakini uzalishaji nchini na gharama zake kwa sababu haiwezekani kabisa kahawa,sukari,unga,n.k vinavyozalishwa nchini na kufikia finished product iwe ghali madukani kuliko zinazoagizwa toka nje..
Na karibu kila kitu kinachotengenezwa nchini ni ghali kuliko kuagiza nje iwe UK, US,India au China..

Yawekana pia kuwa hizi ndio athari za matumizi ya nyenzo za kisasa za ukulima ikiwemo mbolea na mbegu kwa sababu gharama zake huongezwa ktk bei ya mazao hayo kwa mlaji ambaye kazoea kununua toka kwa mkulima wa asili asiyekuwa na gharama zaidi ya nguvu kazi..Mlijue hili kama halipo basi linakuja..na nina mashaka makubwa kama wananchi wataweza kumudu gharama za kilimo kwanza kutoka mifukoni mwao..
Hilo nalo neno!
 
Atakuwa amefanya jambo la Busara watanzania na kimsingi huo ndo wajibu wake na si kuingiza jeshi la polisi kuwa kitengo cha ccm kama walivyofanya akina mahita na wengineo.
 
Kumbe sa nyingine akili wanazo halafu wanajifanya majuha.kudadadadeki mzee wa intelijensia kova kashasanuka hali ni mbaya.
 
kweli mkuu kaona bora kasema wazi baadaye asije akachekwa kashindwa kazi ndo maana anagoma kwa sababu anakosa ushirikiano , lakini we have to change now maana 2015 sio mbali na watu wanaumiza vichwa maisha yao na huu ukwasi sasa hivi ni mbaya kuliko maisha yote yaliyowahi tokea , tunaomba wahusika na kama wanasoma jf wajaribu kufanya kazi kama mchwa wasichoke maana wakati wanaomba kazi walikuwa mikono nyuma leo wanajibu wanavyotaka na kazi awafanyi wanafanya mipango ya kuninenepesha basi sasa ni mbaya maana njaa ya matumbo ikizidi watu watajaa barabara zote tanzania na ni noma sasa
 
Back
Top Bottom