Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 15,546
- 19,409
Jina langu ni Kichuguu mwana wa Porini, huwa natambuliwa rasmi kama Kichuguu Cha-Porini. Rafiki zangu wananiita majina tofauti, wale niliokuwa nao shule ya msingi sekondari na JKT huniiita Kichuguu, na wale niliokutana nao Chuo Kikuu cha Dar es Salaam huniita Cha-Porini. Miaka 18 iliyopita nilihamia Marekani ambako nimekuwa nafanya biashara na kufundisha chuo kikuu fulani. Marafiki zangu wote huko huniita Kichuguu, ila wateja wangu wa kibiashara huniita Mr Cha-Porini, na hivyo wasaidizi wangu kwenye biashara wamezowea namna mbili za kuniita: tukiwa na wateja huniita Mr. Cha-Porini na tunapokuwa peke yetu basi huniita Kichuguu.
Kule kwenye chuo ninakofundisha, wafanyakazi wa ngazi zote wananitambua kwa jina la Kichuguu, ila nikiletewa barua ya kiofisi basi huandikwa kwa Dr. Kichuguu Cha-Porini. Nikiitwa kwenye pati za kikazi basi barua zile huja nyumbani moja kwa moja na huandikwa kwa Kichuguu & Mkewangu ChaPorini, huwa hawaonyeshi titles za Prof, Dr. Mr and Mrs kabisa. Wanafunzi wangu wamekuwa hawatabiriki kabisa; huniita majina yoyote kati ya Dr. Cha-Porini, Professor Cha-Porini, Mr. Cha-Porini, Dr. Kichuguu, Professor Kichuguu na Mr. Kichuguu.
Hivi majuzi nilitembelewa na rafiki zangu wawili tuliokuwa nao pale Chuo Ubungo, mmoja ni Associate Professor (nitampachika jina la Julius Nyerere kuficha identity yake) , mwingine ni Senior Lecturer ( yeye nitampachika jina la Jomo Kenyatta); waliongozana na Assistant Lecturer mmoja ambaye yuko kwenye mchakato wa kuhenyea Ph.D. yake kihalali (huyu nitamwita Milton Obote). Niliandaa hafla ndogo nyumbani kwangu ili kuwakaribisha mjini wageni wangu hawa hivyo nikaalika marafiki zangu kutoka chuoni ambao ni maprofesa kwenye nyanja sawa na za wageni wangu Julius na Jomo, kwani nilidhani kuwa hiyo itawafanya wachanginyakane kwa urahisi- hawatakosa la kuongelea.
Kama mwenyeji nilifungua halfa ile kwa kujitambulisha mwenyewe na familia yangu; nikawaambia wenzangu kuwa mnanifahamu mimi naitwa Kichuguu, mke wangu anaitwa Mkewangu; nikafanya hivyo pia kwa watoto wangu watatu pamoja na mtoto wa dada niliyem-adopt ili kumpa nafasi ya kujipatia elimu. Baada ya hapo nikawatambulisha wageni wetu, nikaanza na yule Associate Professor kwa kusema huyu ni rafiki yangu wa siku nyingi sana tangu utotoni ingawa tulikuwa shule za msingi tofauti lakini tulikuwa tunakaa mtaa mmoja pale Tabora; anaitwa Julius, na huyu mwingine tulikutana tukiwa Chuo kikuu, yeye anaitwa Jomo; huyu wa mwisho nimemfahamu hapa kwa mara ya kwanza, wakati naondoka bongo alikuwa hajajiunga na kile Chuo; yeye anaitwa Milton. Baada ya hapo nikawaomba rafiki zangu waalikwa nao wajitambulishe, wakafanya hivyo kwa kutaja majina yao ya kwanza na tukaendelea na party.
Mwishoni mwa party nikawaruhusu wageni wetu kutoka Dar nao kuzungumza waliyo nayo na kuwashukuru waliohudhuria pati ile. Hapo ndipo nilipojisikia Pwaa!!!!. Rafiki yangu Julius akatumia muda huo kufanya masahihisho kidogo kwenye utambulisho niliokuwa nimetoa mwanzo kwa kusema kuwa yeye jina lake halisi ni Professor Nyerere na huyo mwingine ni Dr Kenyatta, na huyu kijana yeye ni Mr. Obote. Basi tulipofunga pati, marafiki zangu waaalikwa waliwaaga marafiki zangu wageni kwa kutumia majina hayo hayo "kwaheri Professor Nyerere." "kwaheri Dr. Kenyatta" na "kwa heri Mr. Obote." Ilikuwa awkward moment kwangu kwa vile marafiki niliowaalika wote wana Ph.D. na ni maprofessor wa siku nyingi sana wakiwa wameshaandika papers zaidi ya 300 katika nyanja zao ambazo zinashabihiana kabisa na zile za Julius na Jomo, lakini niliwatambulisha wote kwa majina yao ya kwanza.
Nilifanya kosa gani? Je kweli ni lazima nimwite rafiki yangu Professor Nyerere wakati nimekuwa namfahamau kama Julius kwa zaidi ya miaka 40?
Kule kwenye chuo ninakofundisha, wafanyakazi wa ngazi zote wananitambua kwa jina la Kichuguu, ila nikiletewa barua ya kiofisi basi huandikwa kwa Dr. Kichuguu Cha-Porini. Nikiitwa kwenye pati za kikazi basi barua zile huja nyumbani moja kwa moja na huandikwa kwa Kichuguu & Mkewangu ChaPorini, huwa hawaonyeshi titles za Prof, Dr. Mr and Mrs kabisa. Wanafunzi wangu wamekuwa hawatabiriki kabisa; huniita majina yoyote kati ya Dr. Cha-Porini, Professor Cha-Porini, Mr. Cha-Porini, Dr. Kichuguu, Professor Kichuguu na Mr. Kichuguu.
Hivi majuzi nilitembelewa na rafiki zangu wawili tuliokuwa nao pale Chuo Ubungo, mmoja ni Associate Professor (nitampachika jina la Julius Nyerere kuficha identity yake) , mwingine ni Senior Lecturer ( yeye nitampachika jina la Jomo Kenyatta); waliongozana na Assistant Lecturer mmoja ambaye yuko kwenye mchakato wa kuhenyea Ph.D. yake kihalali (huyu nitamwita Milton Obote). Niliandaa hafla ndogo nyumbani kwangu ili kuwakaribisha mjini wageni wangu hawa hivyo nikaalika marafiki zangu kutoka chuoni ambao ni maprofesa kwenye nyanja sawa na za wageni wangu Julius na Jomo, kwani nilidhani kuwa hiyo itawafanya wachanginyakane kwa urahisi- hawatakosa la kuongelea.
Kama mwenyeji nilifungua halfa ile kwa kujitambulisha mwenyewe na familia yangu; nikawaambia wenzangu kuwa mnanifahamu mimi naitwa Kichuguu, mke wangu anaitwa Mkewangu; nikafanya hivyo pia kwa watoto wangu watatu pamoja na mtoto wa dada niliyem-adopt ili kumpa nafasi ya kujipatia elimu. Baada ya hapo nikawatambulisha wageni wetu, nikaanza na yule Associate Professor kwa kusema huyu ni rafiki yangu wa siku nyingi sana tangu utotoni ingawa tulikuwa shule za msingi tofauti lakini tulikuwa tunakaa mtaa mmoja pale Tabora; anaitwa Julius, na huyu mwingine tulikutana tukiwa Chuo kikuu, yeye anaitwa Jomo; huyu wa mwisho nimemfahamu hapa kwa mara ya kwanza, wakati naondoka bongo alikuwa hajajiunga na kile Chuo; yeye anaitwa Milton. Baada ya hapo nikawaomba rafiki zangu waalikwa nao wajitambulishe, wakafanya hivyo kwa kutaja majina yao ya kwanza na tukaendelea na party.
Mwishoni mwa party nikawaruhusu wageni wetu kutoka Dar nao kuzungumza waliyo nayo na kuwashukuru waliohudhuria pati ile. Hapo ndipo nilipojisikia Pwaa!!!!. Rafiki yangu Julius akatumia muda huo kufanya masahihisho kidogo kwenye utambulisho niliokuwa nimetoa mwanzo kwa kusema kuwa yeye jina lake halisi ni Professor Nyerere na huyo mwingine ni Dr Kenyatta, na huyu kijana yeye ni Mr. Obote. Basi tulipofunga pati, marafiki zangu waaalikwa waliwaaga marafiki zangu wageni kwa kutumia majina hayo hayo "kwaheri Professor Nyerere." "kwaheri Dr. Kenyatta" na "kwa heri Mr. Obote." Ilikuwa awkward moment kwangu kwa vile marafiki niliowaalika wote wana Ph.D. na ni maprofessor wa siku nyingi sana wakiwa wameshaandika papers zaidi ya 300 katika nyanja zao ambazo zinashabihiana kabisa na zile za Julius na Jomo, lakini niliwatambulisha wote kwa majina yao ya kwanza.
Nilifanya kosa gani? Je kweli ni lazima nimwite rafiki yangu Professor Nyerere wakati nimekuwa namfahamau kama Julius kwa zaidi ya miaka 40?