Kosa la kutobadilisha jina la African Barrick Gold na Acacia kama lipo faini yake ni elfu moja tu!

Hapana, wameruhusiwa kucheguwa dhahabu tu, na sio madini mengine. Hata wao wanajuwa hilo na ndio Maana hawajatoa kauli kukataa kama wanapata zaidi ya dhahabu. Mkataba ni mibovu nakubali, lakini kama na wao ni waaminifu kwanini mpaka wakakataa mkuu wa mkoa au mtu yoyote wa serikali hata kuona kilicho ndani ya ndege wanazosafirisha dhahabu nje ya nchi. Mkataba mibovu kisiwe kigezo cha kufuta dhambi zao za nyuma. Wamekwepa kodi, watoa taarifa za uwongo, wamedanganya hata kiwango cha mchanga wanchosafirisha kwenda nje.
Sasa mkuu wakishachenjua dhahabu huo mchanga waurudishe tena nchini? Tambua kwamba yale ni mabaki baada ya dhahabu( pure gold) kutolewa. Kiasi kinachabaki kwenye huo mchanga hakuna kinu( smelter) hapa nchini ya kuichenjua na ndio maana wakaruhusiwa kupeleka hayo tunayoita makinikia ambayo yana madini mengine huko wanakojua wao wakachenjue.

Elewa jambo moja mkuu, kama wasingeruhusiwa kupeleka hayo makinikia huko wanakojua wao, yangebaki hapa nchini na wala leo hii habari tunayoijadili isingekuwepo. Labda tungekuwa tunajadili namna serikali itavyojenga hicho kinu( smelter) ili hayo makanikia tuyachenjue wenyewe.
 
Madini waliyochimba ni yao wewe dai kodi kama zipo. Kuizuia mizigo kuna faini hata kile kidogo hutapata na kuishia kuendesha migodi ya watu bila kuvuna hata sumni

Dai BUKU wakachape kazi kwa jina jipya l Acacia
Jamani uzalendo uko wapi? Mbona mnatukaanga ndugu zenu
 
Sasa mkuu wakishachenjua dhahabu huo mchanga waurudishe tena nchini? Tambua kwamba yale ni mabaki baada ya dhahabu( pure gold) kutolewa. Kiasi kinachabaki kwenye huo mchanga hakuna kinu( smelter) hapa nchini ya kuichenjua na ndio maana wakaruhusiwa kupeleka hayo tunayoita makinikia ambayo yana madini mengine huko wanakojua wao wakachenjue.

Elewa jambo moja mkuu, kama wasingeruhusiwa kupeleka hayo makinikia huko wanakojua wao, yangebaki hapa nchini na wala leo hii habari tunayoijadili isingekuwepo. Labda tungekuwa tunajadili namna serikali itavyojenga hicho kinu( smelter) ili hayo makanikia tuyachenjue wenyewe.
Ni sawa uliyosema kama hakuna kinu, vingozi wetu walichukiwa chao, na hawawezi kurudisha mchanga Tz. Lakini lazima tujuwe tunafanya na biashara na nani kuelewa zaidi swala zima la wachimbaji wa madini. Tunalaumu viongozi wetu wakati kampuni hizi ndio zinazomwaga asali kwa viongozi wetu na kushinikiza mikataba mibovu, halafu sisi ndio tunalaumiana wenyewe hapa.

Sisi kuwa na kinu sio hoja kabisa kwasababu ni kitu ambacho kinawezekana, tuna makaa ya mawe hapa yanaweza kutoa moto wakutosha kuyeyusha kitu chochote. Sio sisi tu wenye matatizo kama haya, nchi ya Mali wanasumbuka kama sisi huku. Wakati wa kuibia Africa umekwisha. Enough is enough
 
Tumesikia Acacia haijasajiliwa lakini kampuni mama African Barrick Gold imesajiliwa.

Kusajiliwa kwa African Barrick Gold kunaiondolea Acacia umuhimu wa kusajiliwa mara ya pili bali kubadilisha jina kutoka African Barrick Gold na kuwa Acacia.

Kama hilo halijafanyika ni kosa la kwanza na adhabu yake ni kulipa faini ya Tshs 1,000/= wakirudia watatakiwa kila siku kosa linaendelea walipe faini ya Tshs 5,000/= ambayo nina uhakika Barrick hawana bifu na hilo. Kifungu cha 324 & 327 vya CAP 212 vya sheria ya makampuni ndivyo vinavyotamka

Kichekesho ni kutoitofautisha African Barrick Gold na Acacia hivyo kuja na khoja za kijiweni eti ni kampuni mbili tofauti.

Mwanzisha khoja ni kampuni mbili tofauti ndiye mwenye jukumu la kutoa nyaraka za lini, wapi na kwa kiasi gani Acacia iliinunua African Barrick Gold.

Someni sheria ya kuanzisha makampuni nchini Cap 212 walifuta na kufuta BUKU kwa sheria ya no. 12.

Ushauri

Tudai BUKU kwa sheria iliyofutwa kwani hii mpya hakuna adhabu kwa kuchelewesha kubadilisha jina!
Kala HONGO la Wazungu huyo.
 
Madini waliyochimba ni yao wewe dai kodi kama zipo. Kuizuia mizigo kuna faini hata kile kidogo hutapata na kuishia kuendesha migodi ya watu bila kuvuna hata sumni

Dai BUKU wakachape kazi kwa jina jipya l Acacia

Madini wanayochimba ni yao, lakini lazima watupe hesabu za ukweli, wakidanganya huo ni wizi. Hawa wanevunja sheria, wizi haundani na mkataba pamoja na ubovu wa mikataba, hii inakuwa breach of contract, inatupa nafasi hata ya kuvunja mikataba ikiwa lazima ana sivyo lazima turudi kwenye negotiated table. With our own terms.
 
Back
Top Bottom