Kosa kubwa alilofanya IGP Sirro katika tuhuma za ugaidi dhidi ya Mbowe, ambalo linaweza kuleta fedheha mbaya kwake binafsi, kwa Polisi na Tanzania

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Huwa najaribu kumuelewa IGP Sirro katika suala la kesi ya ugaidi dhidi ya Mbowe, hadi najiuliza hivi kweli uwezo wa IGP Sirro katika kufikiria ndio umeishia hapo?

Suala liko hivi. Huyo askari Luteni wa JWTZ anaita askari anasema ameambiwa na Mbowe kwamba anataka kufanya ugaidi, na anataka amtafutie makomandoo wa kumsaidia kufanya ugaidi.

Askari wanaingia laini ya huyu Luteni (bila kujiuliza kama inawezekana Luteni ana ugomvi wake binafsi na Mbowe na anataka tu kuwatumia Polisi kulipiza kisasi)

Kisha Polisi, badala ya kumalizana na huyo mtu ili wachunguze wenyewe (take ownership of the investigation) kama kweli kuna ugaidi - yaani watafute supporting evidence, wanamuambia endelea kutafuta watu wa kumfanyia ugaidi Mbowe halafu uwe unatupa taarifa.

Sasa ukosefu wa umakini wa Polisi wa pili hapa ni kwamba walipaswa wao ndio watoe hao makomandoo (undercover police), sio kumwachia huyu Luteni fake, lakini IGP hadi hapo hajaona ukihiyo unaofanyika. Hao makomandoo walipaswa kuwa watu wa TISS au polisi ili iwe rahisi wao kuwa insiders, lakini kwa uwezo wa IGP hakuwaza mbali kiasi hicho.

Mfano, ukiwaambia Polisi kuna mtu kanipa kazi ya kutafuta mtu wa kuua mke wake (contract killer), Polisi wanapaswa kukupa askari ambaye atajifanya yeye ndie muuaji aliepatikana , sio wakuambie wewe mtafutie huyo muuaji halafu uwe unatupa taarifa! Hiyo sio tu ni unprofessional, bali ni the most stupid mistake a police force can make!

Baada ya muda Luteni anawaambia polisi haya nimeshampa Mbowe makomandoo magaidi wawili.

Sasa tena, badala ya Polisi kuanza kufuatilia hao watu wanakutanana na nani, wananunua vitu gani (kama milipuko kwa ajili ya kulipulia hivyo vituo) wao wanaamua kwenda moja kwa moja kuwakamata hao "makomandoo". Na sio labda wanawakamata wakiwa na Mbowe wanapanga kitu ili wakamate na evidence, hapana.

Sasa masuala ya kujiuliza;
  1. Polisi walimchunguza huyu Luteni ni mtu wa namna gani, kwa mfano kama ana akili sawasawa au anaweza akawa ana matatizo ya kufikria vitu kichwani kutonakana na post war traumas labda katika mission za JWTZ alizohusika? (Yaani ana paranoia ya ugaidi)
  2. Zaidi ya maneno ya huyu Luteni fake wa JWTZ, Polisi hadi wanaamua kufanya arrests, walikuwa na ushahidi wotewote wa ku-support tuhuma za ugaidi - wanasema Mbowe alitoa fedha, kwani katika kutoa fedha kuna mahali Mbowe aliandika "haya ni malipo halali kwa ajili ya vitendo vya ugaidi nilivyopanga"?
  3. Mmoja wa hao makomandoo aliajiriwa na Mbowe kama mlinzi. Je IGP Sirro hakujiuliza kwamba huyu Luteni wa JWTZ anaweza kuwa yeye ndio alikuwa anawapa maagizo hawa Makomandoo kwamba nawapeleka kwa Mbowe ili mkamsaidie kufanya ugaidi bila Mbowe kuwa na habari kwamba watu aliomuomba Luteni amtafutie kama walinzi wanaambiwa kwamba wanaenda Chadema wakafanye ugaidi
  4. Kimsingi, Mbowe ana fursa nzuri ya kumgeuzia kibao IGP Sirro na huyu Luteni wa JWTZ kwamba wao ndio walipanga kutafuta makomandoo wa kufanya ugaidi kwa kumtumia yeye na Chadema, ili hao makomandoo wakifanya ugaidi, huyu Luteni aseme nilishawaambia Polisi ni Mbowe sio mimi - au kwamba Luteni alitaka kufanya Ugaidi, na ili kujilinda, akawahusisha Polisi ili ionekane ni Mbowe, lakini kimsingi yeye ndio aliwatuma makomandoo wakafanye ugaidi kupitia kivuli cha Mbowe na Chadema (ndio maana ilikuwa muhimu sana Polisi kutoa makomandoo wao fake kumpa Mbowe)
  5. Kimsingi, IGP Sirro alitakiwa pia aelewe philosophy ya kupambana na serikali kwa ugaidi. Matukio ya ugaidi mara nyingi yanaendana na mtu au kikundi kujitambulisha kwamba sisi ndio tunahusika na kulipua kitu fulani ili haki zetu zitambuliwe. Hivi IGP Sirro alijiuliza kama Mbowe angefanyaje ugaidi bila kusema sisi Chadema ndio tumehusika? Wanadai Mbowe angelipua vituo vya mafuta - kwani vituo vya mafuta vinamilikiwa na Polisi au CCM hadi Mbowe awe na ugomvi navyo? Hakuna wanachama wa Chadema wanaomiliki vituo vya mafuta - sasa iweje Mbowe afanye ugaidi dhidi ya wanachama wake wa Chadema?
Nina wasiwasi sana kwamba IGP Sirro, kwa kushupalia jambo hili kwa sababu ya issue zake binafsi na Chadema, na labda kijpendekeza kwa watawala, au kutafuta easy popularity, au labda bila kujua anaingizwa cha kike na Luteni ambae hayuko sawa kichwani au ana akili sana, anaweza akawa ametumika na mtu kirahisi sana, na kufanya jambo ambalo ni la kujifedhehesha mwenyewe, kufedhehesha jeshi la Polisi, na kuifedhehesha Tanzania

Na by the way, mie sio Polisi, bali hapa ni common sense tu. Unfortunately, najua kwamba common sense is not common to everyone, even the supposedly professionals!
 
nashauli tusiwe wepesi kutoa hukumu na kuanza kubagaza watu kabla kesi haijafika popote,

wapo mashahidi wa kutosha

tusubiri watoe ushahidi wao then tuupime.
 
nashauli tusiwe wepesi kutoa hukumu na kuanza kubagaza watu kabla kesi haijafika popote,

wapo mashahidi wa kutosha

tusubiri watoe ushahidi wao then tuupime.
Mashahidi sio ndio hao uliowasikia tayari?

Hawa ndio Polisi wetu tunaowategemea kuwa makini, hata kuandika kiswahili shida, hakuna vituo, vurugu wanaita vulugu, basi tu bora liende

Angalia hapa, "WALIPOFIKA MAENEO YA MTIMA NA KUONA PIKIPIKI INAYOSADIKIWA KUWA IMEBEBA MAGENDO KUTOKA NCHI JIRANI YA MALAWI"

Walisadikishwa na nani ikiwa wameiona tu hata bila kuangalia jamaa kabeba nini?

TAARIFA YA TUKIO LA ASKARI POLISI WETU 7 KUINGIA NCHINI MALAWI.

MNAMO TAREHE 15/09/2021 MAJIRA KATI YA SAA 16:30 - 17:30HRS HUKO MANEO YA KITONGOJI CHA MTIMA, KIJIJI CHA IKUMBILO, KATA YA CHITETE, TARAFA YA BULAMBYA, WILAYA YA ILEJE NA MKOA WA SONGWE ASKARI G.3695 D/SGT RAMADHANI,H.694 PC EDWARD, H.8096 PC SAFARI, WP.12285 PC ANASTAZIA, H.9727 PC JOSEPH, H.9781 PC HUSSEIN NA H.8764 PC JUMANNE WAKIWA NA GARI PT.3676 TOYOTA L/CRUISER MALI YA JESHI LA POLISI TANZANIA WAKITOKEA VWAWA KUPELEKA WATUHUMIWA WA KESI YA MAUAJI PI.3/2020, WALIPOFIKA MAENEO YA MTIMA NA KUONA PIKIPIKI INAYOSADIKIWA KUWA IMEBEBA MAGENDO KUTOKA NCHI JIRANI YA MALAWI, WALIISIMAMISHA LAKINI PIKIPIKI HIYO ILIAMUA KUKIMBIA KUELEKEA NCHI JIRANI YA MALAWI, ASKARI. WALIAMUA KUIFUKUZIA NA KUVUKA MPAKA WA TANZANIA NA KUINGIA NCHINI MALAWI NA NDIPO WANANCHI WA MALAWI WALIIZINGIRA GARI HILO IKIWA NA ASKARI NCO G3695 DSGT RAMADHAN, H.8096 PC SAFARI, H9727 PC JOSEPH, H.694 D/C EDWARD, H.9781 PC HUSSEIN, WP.12285 PC ANASTAZIA NA H.8764 PC JUMANNE WAKIWA NA SILAHA MBILI AINA YA AK 47 NA KUANZA KUWASHAMBULIA.KWA.MAWE NA BAADAYE KUPATA MSAADA WA KUOKOLEWA NA ASKARI POLISI WA MALAWI(+) KATIKA VULUGU HIZO ASKARI MMOJA H8764 PC PC JUMANNE AMBAYE NI DEREVA ALIJERUHIWA KWA KUKATWA NA PANGA KICHWANI HALI YAKE SIO MBAYA ANAENDELEA VIZURI PIA GARI INASEMEKANA LIMEHARIBIWA KWA KUPIGWA KWA MAWE NA SILAHA AK 47 ZOTE MBILI ZIPO SALAMA NA ZIMEHIFADHIWA KITUO CHA POLISI CHITIPA MALAWI. ASKARI NO. G.3695 D/SGT RAMADHANI AMBAYE ALIKUWA KIONGOZI WAO, H.8096 PC SAFARI NA H.9727 PC JOSEPH WALIFANIKIWA KUTOROKA KATIKA VULUGU HIZO NA KURUDI KITUONI SALAMA NA WAPO MAHABUSU KWA HATUA ZA KINIDHAMU. MAWASILIANO KATI YA UONGOZI WA WILAYA NA MKOA TANZANIA NA MALAWI YANAENDELEA KWA AJILI YA KUWAREJESHA NCHI ASKARI HAO PAMOJA NA GARI NA SILAHA.
 
Mashahidi sio ndio hao uliowasikia tayari?

Hawa ndio Polisi wetu tunaowategemea kuwa makini, hata kuandika kiswahili shida, hakuna vituo, vurugu wanaita vulugu, basi tu bora liende

TAARIFA YA TUKIO LA ASKARI POLISI WETU 7 KUINGIA NCHINI MALAWI.

MNAMO TAREHE 15/09/2021 MAJIRA KATI YA SAA 16:30 - 17:30HRS HUKO MANEO YA KITONGOJI CHA MTIMA, KIJIJI CHA IKUMBILO, KATA YA CHITETE, TARAFA YA BULAMBYA, WILAYA YA ILEJE NA MKOA WA SONGWE ASKARI G.3695 D/SGT RAMADHANI,H.694 PC EDWARD, H.8096 PC SAFARI, WP.12285 PC ANASTAZIA, H.9727 PC JOSEPH, H.9781 PC HUSSEIN NA H.8764 PC JUMANNE WAKIWA NA GARI PT.3676 TOYOTA L/CRUISER MALI YA JESHI LA POLISI TANZANIA WAKITOKEA VWAWA KUPELEKA WATUHUMIWA WA KESI YA MAUAJI PI.3/2020, WALIPOFIKA MAENEO YA MTIMA NA KUONA PIKIPIKI INAYOSADIKIWA KUWA IMEBEBA MAGENDO KUTOKA NCHI JIRANI YA MALAWI, WALIISIMAMISHA LAKINI PIKIPIKI HIYO ILIAMUA KUKIMBIA KUELEKEA NCHI JIRANI YA MALAWI, ASKARI. WALIAMUA KUIFUKUZIA NA KUVUKA MPAKA WA TANZANIA NA KUINGIA NCHINI MALAWI NA NDIPO WANANCHI WA MALAWI WALIIZINGIRA GARI HILO IKIWA NA ASKARI NCO G3695 DSGT RAMADHAN, H.8096 PC SAFARI, H9727 PC JOSEPH, H.694 D/C EDWARD, H.9781 PC HUSSEIN, WP.12285 PC ANASTAZIA NA H.8764 PC JUMANNE WAKIWA NA SILAHA MBILI AINA YA AK 47 NA KUANZA KUWASHAMBULIA.KWA.MAWE NA BAADAYE KUPATA MSAADA WA KUOKOLEWA NA ASKARI POLISI WA MALAWI(+) KATIKA VULUGU HIZO ASKARI MMOJA H8764 PC PC JUMANNE AMBAYE NI DEREVA ALIJERUHIWA KWA KUKATWA NA PANGA KICHWANI HALI YAKE SIO MBAYA ANAENDELEA VIZURI PIA GARI INASEMEKANA LIMEHARIBIWA KWA KUPIGWA KWA MAWE NA SILAHA AK 47 ZOTE MBILI ZIPO SALAMA NA ZIMEHIFADHIWA KITUO CHA POLISI CHITIPA MALAWI. ASKARI NO. G.3695 D/SGT RAMADHANI AMBAYE ALIKUWA KIONGOZI WAO, H.8096 PC SAFARI NA H.9727 PC JOSEPH WALIFANIKIWA KUTOROKA KATIKA VULUGU HIZO NA KURUDI KITUONI SALAMA NA WAPO MAHABUSU KWA HATUA ZA KINIDHAMU. MAWASILIANO KATI YA UONGOZI WA WILAYA NA MKOA TANZANIA NA MALAWI YANAENDELEA KWA AJILI YA KUWAREJESHA NCHI ASKARI HAO PAMOJA NA GARI NA SILAHA.
hadi sasa anayetoa ushahidi ni mmoja na bado hajamaliza, ila umeshahitimisha na kuanza kubagaza watu

hio habari hapo chini haihusiani na tunachozungumzia.
 
Mashahidi sio ndio hao uliowasikia tayari?

Hawa ndio Polisi wetu tunaowategemea kuwa makini, hata kuandika kiswahili shida, hakuna vituo, vurugu wanaita vulugu, basi tu bora liende

TAARIFA YA TUKIO LA ASKARI POLISI WETU 7 KUINGIA NCHINI MALAWI.

MNAMO TAREHE 15/09/2021 MAJIRA KATI YA SAA 16:30 - 17:30HRS HUKO MANEO YA KITONGOJI CHA MTIMA, KIJIJI CHA IKUMBILO, KATA YA CHITETE, TARAFA YA BULAMBYA, WILAYA YA ILEJE NA MKOA WA SONGWE ASKARI G.3695 D/SGT RAMADHANI,H.694 PC EDWARD, H.8096 PC SAFARI, WP.12285 PC ANASTAZIA, H.9727 PC JOSEPH, H.9781 PC HUSSEIN NA H.8764 PC JUMANNE WAKIWA NA GARI PT.3676 TOYOTA L/CRUISER MALI YA JESHI LA POLISI TANZANIA WAKITOKEA VWAWA KUPELEKA WATUHUMIWA WA KESI YA MAUAJI PI.3/2020, WALIPOFIKA MAENEO YA MTIMA NA KUONA PIKIPIKI INAYOSADIKIWA KUWA IMEBEBA MAGENDO KUTOKA NCHI JIRANI YA MALAWI, WALIISIMAMISHA LAKINI PIKIPIKI HIYO ILIAMUA KUKIMBIA KUELEKEA NCHI JIRANI YA MALAWI, ASKARI. WALIAMUA KUIFUKUZIA NA KUVUKA MPAKA WA TANZANIA NA KUINGIA NCHINI MALAWI NA NDIPO WANANCHI WA MALAWI WALIIZINGIRA GARI HILO IKIWA NA ASKARI NCO G3695 DSGT RAMADHAN, H.8096 PC SAFARI, H9727 PC JOSEPH, H.694 D/C EDWARD, H.9781 PC HUSSEIN, WP.12285 PC ANASTAZIA NA H.8764 PC JUMANNE WAKIWA NA SILAHA MBILI AINA YA AK 47 NA KUANZA KUWASHAMBULIA.KWA.MAWE NA BAADAYE KUPATA MSAADA WA KUOKOLEWA NA ASKARI POLISI WA MALAWI(+) KATIKA VULUGU HIZO ASKARI MMOJA H8764 PC PC JUMANNE AMBAYE NI DEREVA ALIJERUHIWA KWA KUKATWA NA PANGA KICHWANI HALI YAKE SIO MBAYA ANAENDELEA VIZURI PIA GARI INASEMEKANA LIMEHARIBIWA KWA KUPIGWA KWA MAWE NA SILAHA AK 47 ZOTE MBILI ZIPO SALAMA NA ZIMEHIFADHIWA KITUO CHA POLISI CHITIPA MALAWI. ASKARI NO. G.3695 D/SGT RAMADHANI AMBAYE ALIKUWA KIONGOZI WAO, H.8096 PC SAFARI NA H.9727 PC JOSEPH WALIFANIKIWA KUTOROKA KATIKA VULUGU HIZO NA KURUDI KITUONI SALAMA NA WAPO MAHABUSU KWA HATUA ZA KINIDHAMU. MAWASILIANO KATI YA UONGOZI WA WILAYA NA MKOA TANZANIA NA MALAWI YANAENDELEA KWA AJILI YA KUWAREJESHA NCHI ASKARI HAO PAMOJA NA GARI NA SILAHA.
kwa mahaba ya kisiasa tusiweke rehani akili na utashi wetu .

polisi ni watumishi wenye mambo ya hovyo sana wakati mwingi,ila usiwe mpumbavu wa kudhani wanakuwa hivi wote na wakati wote.
 
hadi sasa anayetoa ushahidi ni mmoja na bado hajamaliza, ila umeshahitimisha na kuanza kubagaza watu

hio habari hapo chini haihusiani na tunachozungumzia.
Naona hujui kwamba shahidi wa kwanza ndio anapangwa ambaye atatoa the highest impact (damage) kwenye kesi. Sasa kama the highest impact ya IGP Sirro ni ushahidi wa Ramadhani Kingai, basi IGP na jeshi lake wote ni watu wa kuhurumiwa sana - ndio hao wanafukuza bodaboda hadi Malawi!
 
Naona hujui kwamba shahidi wa kwanza ndio anapangwa ambaye atatoa the highest impact (damage) kwenye kesi. Sasa kama the highest impact ya IGP Sirro ni ushahidi wa Ramadhani Kingai, basi IGP na jeshi lake wote ni watu wa kuhurumiwa sana - ndio hao wanakukuza bodaboda hadi Malawi!
alieanza kutoa ushahidi ni shahidi namba 2 mkuu

shahidi namba moja hatujamsikia, siwezi kusema yupi ana ushahidi wenye impact kuliko mwingine ila najua shahidi namba moja ana ushahidi mzito

mbona kama huna uhakika sana ila unawahi kufanya hitimisho!
 
Hivi uliona wapi mtu ambaye alipata Zero akaona haya policiciemu hawana haya kwakua wengi ni failures , only in Tanzania failures ndio wanapelekwa polisi. wakati kwingine huko kama hauko na IQ kubwa huwezi kuwa kwenye vyombo vya ulinzi na usalama maana huka akili
 
kumbe tunajadili issue nzito na mtu anayeamini mr bean ni mpumbafu na si mwigizaji!!

hehehe!!!
Inaonekana wewe unamapungufu.
Anachozungumza mwenzio, ni Mr Bean kwa maana ya upuuzi wake. Katika upuuzi wake anasaidia watu kwa kipuuzipuuzi hivyo hivyo.
Akiwa Atikson( kama nimepatia jinalake halisi) hafanyi au kifikiri kama Mr Bean, huko kwongine.
 
alieanza kutoa ushahidi ni shahidi namba 2 mkuu

shahidi namba moja hatujamsikia, siwezi kusema yupi ana ushahidi wenye impact kuliko mwingine ila najua shahidi namba moja ana ushahidi mzito

mbona kama huna uhakika sana ila unawahi kufanya hitimisho!
Mkuu, tatizo ni kwamba, usipoanza na shahidi mwenye impact kubwa na ukamweka shahidi mwenye impact kubwa kuja baadae umeshaharibu kila kitu, kwa kuwa shahidi mwenye impact kubwa itabidi atoe ushahidi unaolingana na shahidi wa kwamza hata kama ameboronga. La sivyo utakuwa na mashahidi ambao wanatofautiana na unapoteza kesi.

Kwa hiyo tukisha msikia shahidi wa kwanza na kuona ameboronga, basi tunajua huna kesi tena ya kushinda!
 
Back
Top Bottom