Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Ni kuendelea na mambo yale yale ya serikali ya Mkapa. Kutokuanza upya kuelekea ujenzi mpya wa taifa la kisasa. Ni kutokukata ile kamba inayomuunganisha yeye na Mkapa na hivyo kuendelea na mtindo ule ule wa uongozi.
Leo hii, kwa kiasi cha kutisha hadi tripu zake za nje (kama nilivyodokeza mwaka jana alipokuja NY) zinaendelea kutumika kama mitaji ya watu wachache.
Kosa hili ni vigumu kulisahihisha kwa kadiri ya kwamba watu aliohusiana nao 2005 na wale waliomwingiza madarakani wakati ule bado wana nguvu kuliko wale tunaowadhaniwa kuwa ni watetezi wa taifa na wanaoongoza vita dhidi ya ufisadi. Kikwete bado hajavunja mahusiano nao, kwani hawezi kuvunja mahusiano hayo. Na endapo akiamua kuvunja mahusiano hayo sasa basi ni kweli hatosimama kama mgombea 2005.
Hata hivyo, kama ilivyokuwa kwa Mkapa, kuna mambo ambayo Jk na washirika wake wanayafanya sasa na siku moja itabidi wayatolee maelezo. Tanzania inahitaji kuanza upya si kuendeleza ya zamani kwa kasi mpya, ari mpya na nguvu mpya.
Kikwete hawezi kuanza upya kwani yeye mwenyewe amefungwa na kamba za fikra za zamani!
That is whats up!
Leo hii, kwa kiasi cha kutisha hadi tripu zake za nje (kama nilivyodokeza mwaka jana alipokuja NY) zinaendelea kutumika kama mitaji ya watu wachache.
Kosa hili ni vigumu kulisahihisha kwa kadiri ya kwamba watu aliohusiana nao 2005 na wale waliomwingiza madarakani wakati ule bado wana nguvu kuliko wale tunaowadhaniwa kuwa ni watetezi wa taifa na wanaoongoza vita dhidi ya ufisadi. Kikwete bado hajavunja mahusiano nao, kwani hawezi kuvunja mahusiano hayo. Na endapo akiamua kuvunja mahusiano hayo sasa basi ni kweli hatosimama kama mgombea 2005.
Hata hivyo, kama ilivyokuwa kwa Mkapa, kuna mambo ambayo Jk na washirika wake wanayafanya sasa na siku moja itabidi wayatolee maelezo. Tanzania inahitaji kuanza upya si kuendeleza ya zamani kwa kasi mpya, ari mpya na nguvu mpya.
Kikwete hawezi kuanza upya kwani yeye mwenyewe amefungwa na kamba za fikra za zamani!
That is whats up!