Kosa afanye jambazi kupigwa apigwe raia, sio sawa

Jindal Singh

JF-Expert Member
Sep 9, 2015
1,853
1,521
Hiki ndicho kilichonifanya nianze uzi bila salaam kutokana na vitendo visivyo vya kizalendo vya askari polisi kupiga na kuumiza raia ambao sisi tunasema kuwa hawana hatia.

Baada ya kutokea shambulizi la kijambazi lililoua askari kadha mkoani pwani sasa imekuwa ni chuki na kulipiza kisasi kwa jeshi la polisi dhidi ya raia yeyote yule atakaeonekana anakatiza katiza barabarani kwa hari yeyote ile, ikiwemo kupigwa virungu na mashuti na ngumi mfano wa mtu anayecheza boxer, hawaishii hapo tu! bali hadi kupora mali za watu katika vioksi.

Kibaya zaidi ni pale mtaji uliozuka kwa wana usalama barabarani kuzidisha kasi ya kukamata magari na kupora pikipiki za watu na kuzifungia.

Sasa hii si njia nzuri ya kuzuia matukio kama haya kuendelea sababu yanaongeza chuki baina ya serikali na raia kwa kupitia polisi.

Angalizo

Njia ya pwani kwa sasa si salama tena kuanzia Mkuranga hadi kibiti hivyo mnaetembea ambao ni wafanyakazi wa ummah basi mnatakiwa muwe na set of ID.
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Nilitegemea wawafanye raia wawe Marafiki zao ili wawezw kupata info za watu wabaya wanaoua Wenzao,then the vice versa. Duh!!!!mbona kazi ipo Hapa jamani....!!
 
Akikusikia mkulu atasema ww mchochezi kwa kauli yake hii "yaani watu wanaimba kwaya kituo cha polisi! i could be IGP" kutakuwa na urafiki kweli hapa?
 
Ndio uweledi wa Polisi ulipoishia hapo badala ya kupenyeza watu wao ili wavune taarifa za kiitelejensia wao wanaongeza gap la chuki
 
Nilitegemea wawafanye raia wawe Marafiki zao ili wawezw kupata info za watu wabaya wanaoua Wenzao,then the vice versa. Duh!!!!mbona kazi ipo Hapa jamani....!!
Wao wameuawa na sokwe? Hiyo ni njia mojawapo ya interrogation.tuache mihemuko raia wema wanajua ubaya wa uhalifu.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom