MZIMU
JF-Expert Member
- Apr 29, 2011
- 4,057
- 1,371
Katika hali ya mshangao mkubwa ukipita mitaani siku hizi utakuta idadi kubwa ya watu wanauza korosho za kuchoma na sio za kubanguliwa kama kawaida yake. Hali hiyo ilinistusha kwa sababu nakumbuka nilipokua mdogo njia pekee ya wakulima kuuza zao la korosho ili kuzichoma kwa kiwango kikubwa na kuziuza kama karanga. Kulikoni? inamaana serekali imeshindwa kuwatafutia wakulima wetu wa korosho masoko ya zao hilo au wananchi wamekasirika juu ya bei wanayo pewa.
Nilibahatika kuumuliza mzee mmoja pale maeneo ya ferry, Kulikoni mbona korosho mnazichoma? Kwa masikitiko akanijibu hakuna soko.
jeeee! Hali hii inatokeaje. Naona kama kunawatu wanatakiwa kujiuzulu hapa. Maana hata mananasi yamesha anza, na Bakhresa sidhani anaweza kuyanunua yote.
Nilibahatika kuumuliza mzee mmoja pale maeneo ya ferry, Kulikoni mbona korosho mnazichoma? Kwa masikitiko akanijibu hakuna soko.
jeeee! Hali hii inatokeaje. Naona kama kunawatu wanatakiwa kujiuzulu hapa. Maana hata mananasi yamesha anza, na Bakhresa sidhani anaweza kuyanunua yote.