Korea Kaskazini yaitia hofu Marekani

guysniper

Member
Apr 2, 2013
59
15
41d8a3de8c9589b8ef547f436b870d79.jpg

Maafisa wa Marekani wanaamini kwamba Korea kaskazini ilitekeleza jaribio jingine la mashine ya kurushia makombora yake .

Jaribio hilo linadaiwa kutekelezwa siku ya Jumatano litakuwa jaribio la kwanza la mashine kama hiyo kutekelezwa na Korea Kaskazini tangu mwezi Machi.

Mashine hizo zinaweza kutumika katika kurusha satelaiti angani, lakini maafisa wa Marekani wana wasiwasi teknolojia hiyo inajaribiwa kutengeza kombora linaloweza kurushwa kutoka bara moja hadi jingine.
 
Mkuu ungebadilisha hata picha bhasi madude hayo hayo habari tofauti kwa nini lakini....


Siku Korea kaskazini akijichanganya tu anapotea kwenye USO wa dunia tuombee ili lisitokeee
 
***** zipigwe tu sasa tumechoka aisee ila wasubiri kidogo tukishagaiwa noah noah zetu ndo watwangane sasa.
 
Yani huyu SAM atulie ivyo ivyo na akotaka ligi team kiduku tutamvuruga mchana kweupeee yani asubuhi tu
 
USA kazoea kuvibutua vinchi visivyo na mbele wala nyuma, now kakutana na know dume haishi kubwekabweka km kahaba alotoa mkopo.
 
Zile meli za kimarekani laini laiiiniii bado zipo rasi ya korea? Mana kim kasema kuzipiga makombora ni uharibifu wa silaha dawa ni kuzigonga tu kama ile ya juzi
 
kuna koment ya mdau mmoja alinichekesha sana kuhusu hz mambo zakujaribu jaribu wanaweza jaribu makombora yakafika hadi kwenye sayari nyingine kumbe huko kuna watu nako tutakuja kupokea kichapo dunia nzima kwan jamaa hawatahitaji kujua limetokea china au usa ni wazo fikirishi sana
 
kuna koment ya mdau mmoja alinichekesha sana kuhusu hz mambo zakujaribu jaribu wanaweza jaribu makombora yakafika hadi kwenye sayari nyingine kumbe huko kuna watu nako tutakuja kupokea kichapo dunia nzima kwan jamaa hawatahitaji kujua limetokea china au usa ni wazo fikirishi sana
Umenichekesha sana. tutapewa kichapo mtindo mmoja, bila kujali nani kawachokoza.
 
Zile meli za kimarekani laini laiiiniii bado zipo rasi ya korea? Mana kim kasema kuzipiga makombora ni uharibifu wa silaha dawa ni kuzigonga tu kama ile ya juzi
Na sisi tutagonga za Putin tena uzuri wa Putin ukiibinya kidogo tu haielei tena inazama bora ya Marekani itaelea mpaka port kupata matengenezo
 
Na sisi tutagonga za Putin tena uzuri wa Putin ukiibinya kidogo tu haielei tena inazama bora ya Marekani itaelea mpaka port kupata matengenezo
Hahahaa sasa kaangalie hiyo ya putin ilikua sio meli vita ilikua ya kijasusi tu kama za kiraia tu lakini marekani wao wana za kivita ila laaaaiiiiiniiii nina uhakika za abiria zitakua bora zaidi kuliko
 
Back
Top Bottom