Korea Kaskazini watishia kuzifuta katika ramani ya dunia Japan na Korea Kusini

STRUGGLE MAN

JF-Expert Member
May 31, 2018
8,638
16,566
"TUTAANZA KWA KUZIFUTA JAPAN NA KOREA KUSINI KWENYE USO WA DUNIA", Kim Jong Un

Akihutubia Kongamano la Chama cha wafanyakazi Jijini Pyongyang, Kiongozi wa Korea kaskazini Kim Jong Un, Amewatahadharisha NATO na Mkuu wa US wasijaribu kueneza chokochoko Karibu na Jamhuri yake kwa Kufanya Mazoezi na Kusogeza silaha katika Nchi za Japan na south Korea.

"Ndiyo wanafanya Mazoezi, ni Kitisho tu, tena kutoka kwa wajinga na waoga, Sisi tumeshakuwa Tayari miaka 10 ama 15 kabla ya Leo, tuna silaha za kutisha...na mtu yeyote ajaribu"...mwenrndo wao wa uchokozi sasa umefika pabaya, Lakini kama ni kutuvamia Basi wamechelewa, Ma comrades wetu wapo macho na Wataalam wangu wameunda silaha hazijawahi kufikiriwa Ulimwenguni"...

"Wamo KWENYE Mipaka ya Mabepari wenzao, wamo Japan na wanatishia kwa kuleta Mazoezi, Nawaambia Kabla risasi yao moja haijatua kwenye Ardhi ya Jamhuri hii, Japan na Korea zitakuwa zimefutika kwenye USO, tutazifuta kabisa, naam zitafutika ili hao majangili wakose pa kudai wanafanya Mazoezi"...

" Silaha zetu ni za kutisha na bahati njema hazizuiliki na mfumo wowote, na kwa namna ya ubora wake, haitatuchukua dakika 30 kuvifuta kabisa visiwa vya hawa wachokozi"...Na Mimi sitanii, na tena sisemi neno bure, wajaribu"...

Bwana Kim pia aliongelea suala la Covid-19 na kudai kuwa nao ilikuwa ni silaha ya uchokozi kwa watu wa Korea Lakini hatua stahiki na za upesi zimesaidia kukabili ugonjwa huo...

FB_IMG_1658152185654.jpg
 
Huo uwezo hana, hiyo ni mikwara tu.
Na Urusi mliwahi kusema hivyohivyo alipokua akitishia kufanya operations zake, Iran mliwahi kusema kuwa haitothubutu kuishambulia marekani wakati walipomuua Generali Qaseem kwa sababu ni member wa nato matokeo yake kambi zao zimepigwa ballistics missiles kugeuzwa kifusi na mikwala ikapigwa kuwa hicho ni kikofi chauso tu, Jua kwamba NKorea ndio tishio zaidi na anao uwezo wa kufanya hicho kitu
 
Back
Top Bottom