Kongole AirTanzania, mnaimarika katika kuitekeleza ndoto ya Rais Magufuli

Hovyoooo! kwa lipi toka awe Rais sijanufaika kwa lolote nilokuwa nayapata enzi za JK ni yaleyale, yani jamii yangu yoteee hatuoni lolote we're still the same.
.
2020 nendeni nae gamboshi mkaloge sio Ikulu
Unataka akupakulie chakula akuletee ukale na wanao? Bilashaka ni mhanga wa vyeti feki, mshahara hewa, madawa ya kulevya, deals za utakatishaji was fedha. Hayo ndo mlikuwa mnampendea Kikwete. Nchi ilibakia sekunde ihuzwe
 
Wanaofaidika na biashara ya anga ni makampuni ya kutengeneza ndege na nchi ambazo zina viwanda vya kutengeneza hizi ndege kwani serikali katika hizo nchi zinakusanya kodi kutoka kwa hawa watengenezaji(viwanda) na si makampuni yanayonunua ndege kufanya biashara ya anga kwani makampuni mengi yanaripotiwa kuendeshwa kwa hasara tu.

Ukiangalia kwa jicho la tatu, utagundua hii biashara ya anga ni aina mojawapo ya kutawaliwa na kunyonywa na mabeberu hivyo ni bora hii biashara ikfanywa zaidi na makampini binafsi na sio serikali hasa hizi serikali za nchi masikini.

Kama hii biashara ni ya hasara kwa nchi nyingi,basi ni vizuri serikali zikaacha makampuni binafsi yafanye hii biashara na serikali zijikite kukusanya mapato yatokanayo na hii biashara kwasababu serikali teyari zina majukumu mengi yanayohitaji fedha kuhudumia raia wake mbali na kukabiliwa na mzigo mkubwa wa madeni.

Tukiandika majina ya mashirika yetu ya ndege kwenye hizi ndege tunaona ndio kutangaza nchi(kwasababu tumeaminishwa hivyo)i na pia ni ufahari wa aina fulani ila kwakuwa ni biashara ya hasara,basi huku ni kutekwa akili na wazungu bila kujijua.

Ngege zinauzwa bei juu,services zake ni gharama kubwa tena sometimes zinafanyikia huko huko tulikozinunua(tunaendelea kuwalipa)n,k hivyo utaona hata sehemu ya hela tunayokusanya japo kwa shida, baada ya muda bado tena tunawapelekea wao.

Kwa kifupi, utaona ni biashara fulani kama ya kinyonyaji hivi ila hatuoni na ndio maama mimi binafsi naona ni bora hii biashara ikafanywa zaidi na makampuni binafsi na si serikali zetu hizi za nchi masikini.

Kama kuna mashirika mengi ya kiserikali duniani,hasa ya nchi za kiafrika, yanayotengeneza faida kutokana na hi biashara,basi nitafuta maneno yangu haya niliyoyaandika hapo juu.

Najua hapa si rahisi kueleweka na hii ni kwasababu wazungu wameshatuteka akili.

Mimi binafsi napanda hizi ndege zilizonunuliwa na Magufuli/serikali, na mambo yakiwa mazuri, nitapanda tena mwezi wa kumi mwaka huu ila ni lazima tuseme ukweli.
 
Kweli tatizo nauli zao si rafiki wajaribu ku adjust kidogo mbona wenzao fast jet walimudu kwa nauli rafiki ambapo wengi tulifaidika? Sasa ATCL mpaka mtu wa kawaida mnyonge na masikini wa Magufuli ukune kichwa sana kumudu nauli zao
Fastjet ilikuwa ni Low Budget Airline na ndiyo maana imeshindwa kwani operational costs ziko juu mno na ndiyo maana walishindwa.
 
Kwa nyongeza tu kama nyie ndo wanasheria tunaowategemea kwenye nch hii naiman kuna jambo haliko sawa haiwezekan hata wewe msomi tunakutegemea leo unasema jiwe anatimiza ndoto zake c kwel kbs
 
Waungwana wa JF nawasalimu,

Nipo safarini kuelekea Kigoma kikazi. Hivi sasa tunatua Uwanja wa Ndege wa Tabora kwakuwa tunapitia hapa kwenda Kigoma. Tupo na Ndege TC 128 aina ya bombardier. Nalazimika kulipongeza Shirika letu la Ndege kwa kuimarisha huduma.

Nimekuwa nikisafiri na Ndege za AirTanzania kwa muda mrefu hapa nchini na hata nje ya nchi. Nikiri kuwa kwa safari za ndani ya nchi,huduma zimeimarika sana. Kuanzia Cabin Crew, Marubani na Watumishi wengine wa AirTanzania, ukarimu na umakini unatamalaki.

Kwa safari zangu za Kigoma kwa Ndege za kuelekea Burundi na kupitia Tabora, leo nimeshuhudia Ndege yetu ikibakiwa na siti tupu tatu tu. Ni jambo la kutia faraja na kuonyesha wananchi kuridhishwa na huduma za AirTanzania. Kongole sana kwenu AirTanzania!

Kuimarika kwa huduma za AirTanzania ni kuisimamia kwa vitendo ndoto ya Rais wetu Dr. John Pombe Magufuli aliyejitoa kwa uwezo na maarifa yake yote kuhakikisha AirTanzania inaimarika na kuwa nembo yetu kitaifa.

Najivunia AirTanzania, najivunia kuwa mtanzania!
Hivi ndoto za Magufuli ni ndoto za taifa, wananchi wa kawaida?
 
Waungwana wa JF nawasalimu,

Nipo safarini kuelekea Kigoma kikazi. Hivi sasa tunatua Uwanja wa Ndege wa Tabora kwakuwa tunapitia hapa kwenda Kigoma. Tupo na Ndege TC 128 aina ya bombardier. Nalazimika kulipongeza Shirika letu la Ndege kwa kuimarisha huduma.

Nimekuwa nikisafiri na Ndege za AirTanzania kwa muda mrefu hapa nchini na hata nje ya nchi. Nikiri kuwa kwa safari za ndani ya nchi,huduma zimeimarika sana. Kuanzia Cabin Crew, Marubani na Watumishi wengine wa AirTanzania, ukarimu na umakini unatamalaki.

Kwa safari zangu za Kigoma kwa Ndege za kuelekea Burundi na kupitia Tabora, leo nimeshuhudia Ndege yetu ikibakiwa na siti tupu tatu tu. Ni jambo la kutia faraja na kuonyesha wananchi kuridhishwa na huduma za AirTanzania. Kongole sana kwenu AirTanzania!

Kuimarika kwa huduma za AirTanzania ni kuisimamia kwa vitendo ndoto ya Rais wetu Dr. John Pombe Magufuli aliyejitoa kwa uwezo na maarifa yake yote kuhakikisha AirTanzania inaimarika na kuwa nembo yetu kitaifa.

Najivunia AirTanzania, najivunia kuwa mtanzania!

Tiketi hiyo umelipiwa na serikali; meaning binafsi most likely hutamudu. Which in turn means, ATCL inaendeshwa kwa pesa za walipa kodi (kwa lugha nyepesi: INAENDESHWA KWA HASARA na KAMWE haitaweza kujiendesha yenyewe).

Enough said!
 
Hivi fastjet alikuwepo hapa Tanzania kwa miaka mingapi huku ATC akiwa hoi na hakuweza kutupa huduma zaidi ya kuchangua njia zenye abiria wengi tu Mwanza, Mbeya, Kilimanjaro? Wajinga ndio waliwao.

Hiyo ndio maana halisi ya kujiendesha kibiashara. Ni uzwazwa kupeleka ndege kwenye route isiyokuwa na watu. And basically that's what Magufuli is doing.
 
Chadema njooni haraka tupingeeeeee
Wacha kiherehere Chadema inatoka wapi hapa?
tapatalk_1564893878930.jpeg
 
Unataka akupakulie chakula akuletee ukale na wanao? Bilashaka ni mhanga wa vyeti feki, mshahara hewa, madawa ya kulevya, deals za utakatishaji was fedha. Hayo ndo mlikuwa mnampendea Kikwete. Nchi ilibakia sekunde ihuzwe
Hahahaha ihuzwe ndio nini?
Nilijua tu mtakuja na hili, nani kasema anataka aletewe chakula?
.
Nataka kuona maendeleo yanifuate nilipo sio niyafuate yalipo huu ndio ujinga magu anaowalisha yani mimi nitoke huku nilipo nifate maendeleo Chato au Dar like seriously?
.
Nikisema hajafanya lolote kwangu na kwa jamii yangu utabisha? Sisi ndio tunaona kazi yake ni kubwabwaja kwenye media tu hatuoni analofanya kwenye jamii yetu, hata kwangu binafsi, hatuna haja ya kazi za serikalini sisi na hatujawahi kuzitaka.
.
Kwenye jamii nayoishi hawajawahi kuwa na tatizo la kutokupeleka watoto shule eti kisa hawana ada Tunataka maendeleo yatufate sio sisi tuyafate Magu ni big lier
 
Hebu tueleze mwenzetu hizo safari za nje ya nchi na Air Tanzania ambazo umekuwa ukisafiri ni lini na kwenda wapi? Maana tunavyoelewa Air Tanzania hawajafanya safari za nje ya nchi kwa zaidi ya miaka kumi.
Kabla ya miaka hiyo kumi je? Hujui kuna route ya India Mkuu?
 
Kabla ya miaka hiyo kumi je? Hujui kuna route ya India Mkuu?
Hahaha! Mkuu acha kunikoroganya kisheria. Ulitoa reasonable implication kwamba ulikuwa ukisafiri na Air Tanzania ndani na nje ya nchi kabla ya mageuzi ya ATC ya Raisi Magufuli, na hivyo ulikuwa ukifanya mlinganisho wa wakati huo na sasa! Kabla ya miaka hiyo kumi ulikuwa unasafiri kikazi kweli? Na kama ni safari za sasa za ATC kwenda India, basi huwezi ku-qualify kauli kuwa umekuwa ukisafiri kwenda nje na ATC "kwa muda mrefu". Angalia Mkuu, humu JF tupo watu makini katika kusoma statements.
 
Hovyoooo! kwa lipi toka awe Rais sijanufaika kwa lolote nilokuwa nayapata enzi za JK ni yaleyale, yani jamii yangu yoteee hatuoni lolote we're still the same.
.
2020 nendeni nae gamboshi mkaloge sio Ikulu
Eti toka aingie hujanufaika na chochote..

Mkuu endelea kupanua mdomo atakuja kukuingizia tonge mdomoni kwako.
 
Back
Top Bottom