Kongo wapinzani wameweza, Tanzania tunasubiri nini?

Mnakosea sana mnapodhani kuwa hatima ya taifa hili iko mikononi mwa wapinzani. Hivi mnaamini kabisa kuwa jukumu la kuhakikisha katiba mpya au tume huru inapatikana ni la wapinzani?
Huu ni muelekeo mbovu na finyu kifikra sababu masuala haya mawili yanabeba maslahi ya taifa, taifa ambalo lina watu chungu nzima wasio na chama wala kupenda siasa.
Kudhani hivyo ni sawa na kuharibikiwa na gari nyumbani halafu ukae pembeni huku ukisema eti fundi ndiyo anapaswa kuja kutoka huko aliko alikokote yeye mpaka lifike gereji wakati kumbe wewe unaweza kufanya yote hayo na yeye akawa na jukumu lake la kulitengeneza tu.
Kitakachobadili mambo hapa ni mass movement ya watu waliopevuka fikra na kuona kuwa sasa imetosha hatuwezi kuendelea kupita njia ile ile ambayo mbele imezibwa na kwamba ni lazima wananchi wenyewe kwa wingi wao washike usukani.
Wapinzani wana mchango wao lakini si sahihi kutegemea kuwa mabadiliko ya nchi hii yako mikononi mwao na sisi wengine ni watazamaji tu. Hii ni vita ya kila mtu sababu matokeo yake yana manufaa kwa maisha ya kila mtu, mwenye chama na asiye na chama.
 
Tuombe maandamano ya amani ya kudai tume huru ya uchaguzi.
Kama tunaogopa virungu na washawasha tutatawaliwa na ccm milele.
 
Tanzania hakuna wapinzani ila
kuna madalali na matapeli ya
Kisiasa watu gani hawana msimamo hawajui hata wanasimamia nini
kweli kabisa wapinzani wengi wapo kibiashara na hakuna mfumo wa kuachiana madaraka sasa wakipewa hii inchi watakubali kutoka kweli kama mtu amekua mwenyekiti wa chama tangu kina anzishwa mpaka sasa bila kuachia madaraka mimi kwa uelewa wangu naona bado tuna safari ndefu sana wengine wako kifamilia na kiukanda katika uongozi wao
 
Tanzania hakuna wapinzani ila
kuna madalali na matapeli ya
Kisiasa watu gani hawana msimamo hawajui hata wanasimamia nini
Mkuu umesahau kua hapa TZ hakuna uongozi wa wananchi bali kuna kundi la wezi na wahuni ndio wapo ofisi kuu
 
Tume huru ya uchaguzi ni matakwa ya wananchi kwa sasa
Kama ilivyo Kongo matakwa yao ni kabila kuondoka madarakani
Wananchi wapo wangapi?. Wenzako wanashughulikia upatikanaji wa maji safi na elimu bora, wewe unayekaa mjini unahangaika na taratibu za kuongoza nchi!!.
 
Katika nchi za kiafrica ambazo zinaongoza kwa unafiki moja wapo ni Tanzania, hii ni kwa wananchi na viongozi pia.
Watanzania tumejaa maneno mengi mdomoni na sio vitendo, kila mmoja anakumbuka operesheni ngapi zimeazishwa na wapinzani na zikasitishwa baada ya kutishwa na serikali. Hayo ni mambo yanayotokea Tanzania tu.
Naamini katika ukweli na kujiamin kama unachokifanya unaamin kipo kisheria kwanini uogope kwa maneno tu.

Hakika uhuru wa mtanzania itachukua muda sana kupatikana.
Nazani inabidi wasitishe kwa sababu labda hata wananch hawapo tayari kujitoa ufaham.
 
Tanzania hakuna wapinzani ila
kuna madalali na matapeli ya
Kisiasa watu gani hawana msimamo hawajui hata wanasimamia nini
Hii movie ya vyama vingi kuna watu wametajilika sana,sisi wananchi tumebakia kuwasapoti tu bila kujua,huu ni ushenzi wa hali ya juu sana na bado tuna safari ndefu.
 
Ni ujinga kutegemea vyama vya upinzani kutuletea katiba mpya. Hili ni jumkumu la kila mtanzania. Kama kweli tunataka katiba mpya kila mtu ashiriki kwa ukamilifu kabisa. Wewe unadhani haya yanayofanyika hapa nchini hivi sasa anayeathirika ni mwanasiasa kama Mbowe, Lissu na wengineo? La Hasha ni walala hoi ndio wanaotaabika.
 
Ni ujinga kutegemea vyama vya upinzani kutuletea katiba mpya. Hili ni jumkumu la kila mtanzania. Kama kweli tunataka katiba mpya kila mtu ashiriki kwa ukamilifu kabisa. Wewe unadhani haya yanayofanyika hapa nchini hivi sasa anayeathirika ni mwanasiasa kama Mbowe, Lissu na wengineo? La Hasha ni walala hoi ndio wanaotaabika.
Umeongea kweli Mkuu
 
Mbona Tanzania Ipo vizuri sana ukilinganisha na Kongo? Nyie wapinzani kazi kudandia tu hata lisilowahusu. Basi nendeni Congo mwone kama Kesho yenu mtaiona.
 
Tena huyo Lowasa ndo alituharibia mchakato wa katiba mpya. Halafu anadai katiba mpya kama sio unafiki ni nini? Angeshinda uraisi angebadili katiba?
Nadhani mkuu hilo swali ni la muhimu kuliko hata uzi wenyewe.. Tafakuri ya jambo hili ingeanzia hapo ili waumini wa mabadiliko ya kuviringisha mikono waweze kuuhakikishia umma wa watanzania ni kwa jinsi gani lowasa angeweza kuyafanya hayo yote.
 
Uoga ni dhambi kubwa sana,na ndio maana wananchi ni masikini,umasikini mkubwa ni wa akili,na uoga,ndio maana tunatawaliwa na kikundi cha watu wachache
 
Back
Top Bottom