security guard
JF-Expert Member
- Sep 27, 2011
- 799
- 603
Nipo katika kongamano la vijana wa mkoa maalum wa vyuo vikuu wa chama cha mapinduzi unguja-Zanzibar. Kongamano limehudhuriwa na vijana wasomi makini wengi mno, mpaka mgeni rasmi makamu wa pili wa serikali ya mapinduzi zanzibar na mjumbe wa kamati kuu ya ccm balozi Seif Ally Iddy ashangaa kuona umati mkubwa wa wanavyuo kuwahi kutokea Zanzibar.
Katika Kongamano hilo ambapo wasomi wa Zanzibar wanapata kujikunbusha na kujifunza tunu za Mapinduzi na historia iliyotukuka ya visiwa vya Zanzibar, limechukua sura mpya baada ya watoa mada wakiongozwa na msaidizi wa makamu wa Rais Ndugu Suleyman Haji, Steven Masatu Wassira na Wilmo Mihayo mmiliki wa Kampuni ya Uhuru one kueleza umuhimu wa wasomi katika maendeleo ya jamii.
Mmoja wa wageni waalikwa ndugu Masauni Hamad Yusuph alieleza kwanini hatuwezi kuzungumza historia ya zanzibar na maendeleo yake bila kuitaja na kutambua nafasi na mchango wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ndipo ukumbi ulipolipuka kwa shangwe na nyimbo za kuisifu CCM.
Kwa hali niliyoiona Upinzani hasa kwa Zanzibar bado wanasafari ndefu ambayo haina uhakika wa kufika katika kituo chao.
Kidumu Chama Cha Mapinduzi.
Katika Kongamano hilo ambapo wasomi wa Zanzibar wanapata kujikunbusha na kujifunza tunu za Mapinduzi na historia iliyotukuka ya visiwa vya Zanzibar, limechukua sura mpya baada ya watoa mada wakiongozwa na msaidizi wa makamu wa Rais Ndugu Suleyman Haji, Steven Masatu Wassira na Wilmo Mihayo mmiliki wa Kampuni ya Uhuru one kueleza umuhimu wa wasomi katika maendeleo ya jamii.
Mmoja wa wageni waalikwa ndugu Masauni Hamad Yusuph alieleza kwanini hatuwezi kuzungumza historia ya zanzibar na maendeleo yake bila kuitaja na kutambua nafasi na mchango wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ndipo ukumbi ulipolipuka kwa shangwe na nyimbo za kuisifu CCM.
Kwa hali niliyoiona Upinzani hasa kwa Zanzibar bado wanasafari ndefu ambayo haina uhakika wa kufika katika kituo chao.
Kidumu Chama Cha Mapinduzi.