Yaani ule uhuni aliyofanya Magufuli na vikaragosi vyake ndio unaita uchaguzi na ndio mnauchukulia kama kipimo cha kukubalika, ngojeni Mungu aitwe Mungu kwani kazi yake haina makosa.Siku zote kipimo cha ridhaa ya wananchi ni kura. Ajenda ya katiba mpya haikuwepo kwenye ilani ya uchaguzi ya CCM ya 2020 na wananchi kwa mamilioni mengi wakaichagua ilani hiyo isiyo na ajenda ya katiba mpya.
Hivyo huhitaji akili kubwa kung'amua kuwa hili siyo ajenda ya wananchi. Sisi wananchi kwa sasa tunahitaji maji, afya, elimu bora, miundombinu ya uhakika na maisha bora.