Kongamano la CHADEMA

Albedo

JF-Expert Member
Feb 24, 2008
5,559
1,452
Jamani nimesoma kupitia vyombo vya habari kwamba leo CHADEMA watakuwa DDC Mlimani City na Kongamano la Wasomi wa vyuo vikuu!
Kama lipo tupeane updates ya nini kinaendelea!
 
He hamna wana CHADEMA huko au kongamano limefulia?
 
Wakati mnaenda kongamano la wasomi DDC Mlimani City, CCM wanaenda vijijini kwa wananchi. Hapo kweli mtaweza kushindana na CCM?

Wapiga kura wako wilayani na vijijini na wala sio hao wajanja wa mjini.
 
halafu mnaenda DDC wakuu?
si mngeenda hata N'KURUMAH HALL PALE?
 
Kule Nkrumah hall itakuwa vigumu sana na pia kumbuka hata sheria ambayo inakataza siasa katika vyuo vikuu lakini naona hata sheria yetu ni hafifu sana katika kujua na hata kutambua umuhimu wa siasa kwenye vyuo vyetu
 
Kule Nkrumah hall itakuwa vigumu sana na pia kumbuka hata sheria ambayo inakataza siasa katika vyuo vikuu lakini naona hata sheria yetu ni hafifu sana katika kujua na hata kutambua umuhimu wa siasa kwenye vyuo vyetu
....mbona enzi zile muungwana aliwahi kwenda,akaenda muzumbe university na aliuza sana kadi za UVCCM?
 
Wakati mnaenda kongamano la wasomi DDC Mlimani City, CCM wanaenda vijijini kwa wananchi. Hapo kweli mtaweza kushindana na CCM?

Wapiga kura wako wilayani na vijijini na wala sio hao wajanja wa mjini.

lazima uende kwa wasomi ili kuattract able people kuja kwenye chama chako na sio kutegemea viongozi makanjanja.
unahitaji watu wenye uwelewa kuwashauri watu (wapiga kura), ccm wao wanasimamisha mtu yeyote na pesa ndio inafanya kazi.

kama ushindi dar basi huwezi kushinda TZ, mabadiliko yanaanzia mjini. ndio maana NCCR kilikuwa maarufu kwa ajili kilikuwa maarufu dar. ccm leo hii hawaachii hata jimbo moja la dar kwa ajili wanajua kitaeneza chama mpaka mikoa mingine, watu wa mikoani look up to what dar is doing.
 
lazima uende kwa wasomi ili kuattract able people kuja kwenye chama chako na sio kutegemea viongozi makanjanja.
unahitaji watu wenye uwelewa kuwashauri watu (wapiga kura), ccm wao wanasimamisha mtu yeyote na pesa ndio inafanya kazi.

kama ushindi dar basi huwezi kushinda TZ, mabadiliko yanaanzia mjini. ndio maana NCCR kilikuwa maarufu kwa ajili kilikuwa maarufu dar. ccm leo hii hawaachii hata jimbo moja la dar kwa ajili wanajua kitaeneza chama mpaka mikoa mingine, watu wa mikoani look up to what dar is doing.

Kama kuna wasomi na able people ambao bado mpaka leo hawaijui CHADEMA, basi mna kazi.

Tatizo sio kwa wasomi, tatizo ni huko wilayani na vijijini.

Wasomi wengi ni opportunists na wanaangalia upepo. Wakiona chama kina nafasi ya kushinda, watakuja wengi tu. Kumbuka NCCR ya Mrema 1995.

Nawatakia mafanikio mema kwenye kongamano lenu.
 
....mbona enzi zile muungwana aliwahi kwenda,akaenda muzumbe university na aliuza sana kadi za UVCCM?
Jaribu kutazama uone jinsi gani CCM waliweza kufanya siasa katika vyuo vikuu na siyo vyama vya upinzania na hivyo ndio unaweza kuona kuwa CCm wanatumia nafasi yao katika kubana demokrasia, Katika Nchi za mwezetu kuna club ya Republican, Democratic katika vyuo karibu vyote America na hii ndio unaweza kupata viongozi bora. Labda mzee alijua kuwa hata kama akisema kuwa anataka kadi ya CCM hakuna mtu wa kumuliza
 
Jamani nimesoma kupitia vyombo vya habari kwamba leo CHADEMA watakuwa DDC Mlimani City na Kongamano la Wasomi wa vyuo vikuu!
Kama lipo tupeane updates ya nini kinaendelea!
Kongamano linaendelea Kamanda MBOWE amewakabidhi kadi wanachama wapya zaidi ya 500.. Ukumbi umefurika wanavyuo toka UDSM,UDOM,SUA,MZUMBE na vyuo vingine wamefika..Wana UDSM Tumeapa kumpigania Prof.Baregu..Sasa TUNDU LISSU anaongea...Mapambano yanaendelea..
 
Kongamano linaendelea Kamanda MBOWE amewakabidhi kadi wanachama wapya zaidi ya 500.. Ukumbi umefurika wanavyuo toka UDSM,UDOM,SUA,MZUMBE na vyuo vingine wamefika..Wana UDSM Tumeapa kumpigania Prof.Baregu..Sasa TUNDU LISSU anaongea...Mapambano yanaendelea..

Tunashukuru sana tunaomba uendelee kutupa habari zaidi wengine tuko mbali lakini tu pamoja.
 
Kongamano linaendelea Kamanda MBOWE amewakabidhi kadi wanachama wapya zaidi ya 500.. Ukumbi umefurika wanavyuo toka UDSM,UDOM,SUA,MZUMBE na vyuo vingine wamefika..Wana UDSM Tumeapa kumpigania Prof.Baregu..Sasa TUNDU LISSU anaongea...Mapambano yanaendelea..

Asante sana Jambo, endelea kutujuza na kama ukiweza weka picha za Kongamano hapa

Asante sana mkuu
 
halafu mnaenda DDC wakuu?
si mngeenda hata N'KURUMAH HALL PALE?

Mkuu Geoff
Mimi nafikiri cha msingi hapa tuangalie mada zenyewe si wapi zimetolewa, unaweza kutoa mada ghorofani isifae na iliyotolewa chini ya mti ikawa ndiyo muhimu zaidi.
 
Kama kuna wasomi na able people ambao bado mpaka leo hawaijui CHADEMA, basi mna kazi.

Tatizo sio kwa wasomi, tatizo ni huko wilayani na vijijini.

Wasomi wengi ni opportunists na wanaangalia upepo. Wakiona chama kina nafasi ya kushinda, watakuja wengi tu. Kumbuka NCCR ya Mrema 1995.

Nawatakia mafanikio mema kwenye kongamano lenu.
Kusubiri kanga ,Tshirt na kofia? Hayo sio makusudio ya Chadema.
 
Kama kuna wasomi na able people ambao bado mpaka leo hawaijui CHADEMA, basi mna kazi.

Tatizo sio kwa wasomi, tatizo ni huko wilayani na vijijini.

Wasomi wengi ni opportunists na wanaangalia upepo. Wakiona chama kina nafasi ya kushinda, watakuja wengi tu. Kumbuka NCCR ya Mrema 1995.

Nawatakia mafanikio mema kwenye kongamano lenu.
ungenisoma vizuri, sijasema wasomi hawaijui chadema bali kuwa attract (nimeji qoute hapo chini). kukijua chama ni kitu kingine na kuwavutia waingie kwenye chama ni kitu kingine.
hata hao ccm wanaoenda vijijini sio kama wananchi wa vijijini hawaijui ccm hapana, bali ccm wanaenda kuwavutia.
by the way mimi sio mwanachadema ni mtu ambaye napenda upinzani ukue TZ.

lazima uende kwa wasomi ili kuattract able people kuja kwenye chama chako na sio kutegemea viongozi makanjanja.
unahitaji watu wenye uwelewa kuwashauri watu (wapiga kura), ccm wao wanasimamisha mtu yeyote na pesa ndio inafanya kazi.

kama ushindi dar basi huwezi kushinda TZ, mabadiliko yanaanzia mjini. ndio maana NCCR kilikuwa maarufu kwa ajili kilikuwa maarufu dar. ccm leo hii hawaachii hata jimbo moja la dar kwa ajili wanajua kitaeneza chama mpaka mikoa mingine, watu wa mikoani look up to what dar is doing.
 
Back
Top Bottom