britanicca
JF-Expert Member
- May 20, 2015
- 15,634
- 30,000
Kuna ka habari kanatrend sehemu kwamba Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP) ofisini kwake kumetokea uhalifu wa kuibiwa kwa CPU za kompyuta zote zenye data.
---
Kamanda wa Kanda Maalum ya Kipolisi, Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, amekiri kwa njia ya simu kwamba tukio hilo ni la kweli.
"Kweli tukio hilo limetokea na polisi tumepokea taarifa Jumanne asubuhi, mpaka sasa hakuna mtu anayeshikiliwa kuhusiana na tukio hilo," alisema Kamanda Mambosasa kwa njia ya simu wakati akizungumza na Nipashe.
Akifafanua zaidi alisema kwa sasa jeshi lake linaendelea na uchunguzi kuhusu tukio hilo.
Hata hivyo, DPP alipopigiwa simu yake ya mkononi mapema jana kuhusu tukio hilo na idadi ya kompyuta zinazodaiwa kuibwa, alisema kwamba yuko kwenye kikao.
"Ndiyo nakusikia kwa sasa niko kwenye kikao," alisema DPP na kukata simu.
Kwa mujibu wa chanzo cha Nipashe Jumanne, Oktoba 15, mwaka huu, asubuhi ilibainika kuibwa kwa kompyuta hizo.
Baadhi ya kesi zilizopo katika hatua ya makubaliano ni ya uhujumu uchumi inayowakabili vigogo wa IPTL, Harbinder Sethi na James Rugemarila, wanaodaiwa kutakatisha zaidi ya Sh. bilioni 309.
Watuhumiwa wengine ni mwandishi wa habari za uchunguzi, Erick Kabendera, anayetuhumiwa kukwepa kodi na kutakatisha jumla ya Sh. milioni 173.
Mtuhumiwa mwingine ni Yusuf Ally, maarufu Mpemba wa Magufuli anayetuhumiwa kusafirisha nyara za serikali zenye thamani zaidi ya Sh. milioni 200.
Chanzo: Nipashe
---
Kamanda wa Kanda Maalum ya Kipolisi, Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, amekiri kwa njia ya simu kwamba tukio hilo ni la kweli.
"Kweli tukio hilo limetokea na polisi tumepokea taarifa Jumanne asubuhi, mpaka sasa hakuna mtu anayeshikiliwa kuhusiana na tukio hilo," alisema Kamanda Mambosasa kwa njia ya simu wakati akizungumza na Nipashe.
Akifafanua zaidi alisema kwa sasa jeshi lake linaendelea na uchunguzi kuhusu tukio hilo.
Hata hivyo, DPP alipopigiwa simu yake ya mkononi mapema jana kuhusu tukio hilo na idadi ya kompyuta zinazodaiwa kuibwa, alisema kwamba yuko kwenye kikao.
"Ndiyo nakusikia kwa sasa niko kwenye kikao," alisema DPP na kukata simu.
Kwa mujibu wa chanzo cha Nipashe Jumanne, Oktoba 15, mwaka huu, asubuhi ilibainika kuibwa kwa kompyuta hizo.
Baadhi ya kesi zilizopo katika hatua ya makubaliano ni ya uhujumu uchumi inayowakabili vigogo wa IPTL, Harbinder Sethi na James Rugemarila, wanaodaiwa kutakatisha zaidi ya Sh. bilioni 309.
Watuhumiwa wengine ni mwandishi wa habari za uchunguzi, Erick Kabendera, anayetuhumiwa kukwepa kodi na kutakatisha jumla ya Sh. milioni 173.
Mtuhumiwa mwingine ni Yusuf Ally, maarufu Mpemba wa Magufuli anayetuhumiwa kusafirisha nyara za serikali zenye thamani zaidi ya Sh. milioni 200.
Chanzo: Nipashe