Elections 2010 Kokotoa hapa..!!

zumbemkuu

JF-Expert Member
Sep 11, 2010
10,831
8,621
Ndugu wana JF, naamini wanafunzi 60,000 waliochakachuliwa kwa makusudi na mafedhuli ni mtaji tosha kwa ukombozi wa nchi yetu, bilashaka ni mipango ya Mwenyezi Mungu kuwafunga wenye mamlaka ufahamu wao ili wanafunzi hawa wawe chachu ya mabadiliko.
kwa hesabu za harakaharaka wanafunzi 60,000 watakuwa wamesambaa karibia kila kata ya wanawainchi hii. katika hao tutoe 10,000 au 20,000 ambao either kwa kutokuwa na ufaham wa kutosha au kwa kufaidika na mfumo wa kifisadi watakuwa na kasumba ya ki'ccm. waliobaki 40,000 au 50,000 wakiwa na hasira ya kuchakachuliwa kutokupiga kura wanaweza wakawashawishi watu zaidi ya 50 kuipigia kura CHADEMA. kama hiyo ikitokea, hao 50 walioshawishiwa kuipigia kura CHADEMA nao watawashawishi wenzao kuingia kwenye hilo kundi la ukombozi, hao nao watawashawishi wengine na wengine na wengine..................

:- 50,000 x 50 x 50 x 50 x ....................................hadi apo ukombozi haujapatikana?
kwa mazingira ya sasa naamini kila mwnfnz hakosi kilongalonga (simu). kilichobaki ni ku'design msg ya kuwakumbusha wajibu wao huko walipo na watambue kuwa kura moja waliokosa inaweza kuzaa kura 1000 au zaidi.
au mnaonaje wenzangu?
 
Watumiwe ujumbe kwamba sasa wafanye kampeni ya kufa mtu kila kona ya nchi waliyokuwepo ili kuhakikisha chama filisi hakirudi madarakani.
 
Watumiwe ujumbe kwamba sasa wafanye kampeni ya kufa mtu kila kona ya nchi waliyokuwepo ili kuhakikisha chama filisi hakirudi madarakani.

huo ujumbe inabidi uwe na chumvi ya kuwapandisha hasira ili wapige kampain ya kufa mtu.
 
Kuna maamuzi mawili ambayo ccm wameyafanya wakidhania kuwa yangewasaidia wao kumbe ndio yatawadhulu. Kwanza ni ule uamuzi wa kuwakataza wagombea wao wasishiriki midahalo ambapo wamekosa nafasi ya kutetea sera zao na pia kuonekana vihiyo mbele ya wananchi. Pili ni huu uamuzi wa kutofungua vyuo vikuu kabla ya uchaguzi; hili litawapa nafasi wanafunzi kuwashawishi watu wengi wapigie kura upinzani kwani wao wanaona hiyo ilikuwa mbinu ya kuwadefranchize!! I have no doubt these two decisions will help in the emancipation of our country.
 
Jana niliambiwa na kiongozi mmoja wa wanachuo eti serekali inaandaa utaratibu ili kuwawezesha wapige kura. Ntaleta news zaidi later kwani leo marais wa wanavyuo wanakutana kujadili hii issue.
 
Back
Top Bottom