Kodi ya laini za simu (simcard tax) ilihamishiwa hapa

tpaul

JF-Expert Member
Feb 3, 2008
21,776
18,192
Serikali imefuta kodi ya ushuru ya Shilingi 1,000 kwa kadi ya simu kwa kila mwezi na kupandisha kiwango cha ushuru wa huduma za mawasiliano kutoka asilimia 14.5 hadi asilimia 17, kuanzia Januari mwakani.

Akiwasilisha Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Ushuru wa Bidhaa ya mwaka 2013, bungeni jana kwa hati ya dharura, Kaimu Waziri wa Fedha, Saada Mkuya Salum, alisema utaratibu huo uliopendekezwa utamwezesha kila mtumiaji wa huduma za mawasiliano kulipa ushuru unaolingana na matumizi yake.

Akifafanua alisema, “mtu atakayetumia kidogo atalipa kidogo na mtu anayetumia zaidi atalipa zaidi tofauti na mfumo wa kulipa kiwango kimoja bila kuzingatia kiasi cha matumizi.”

Aliwaeleza wabunge kuwa pendekezo hilo lina lengo la kupanua wigo wa kutoza ushuru huo kwa kujumuisha huduma zote za mawasiliano ya kielektroniki, huduma za kusafirisha mawasiliano kwa njia ya waya, optical fibre, njia zisizotumia waya na teknolojia nyingine yoyote ya aina hiyo, huduma za usambazaji wa mitandao, huduma za kusafirisha data, huduma za nukushi na huduma zingine za kielektroniki za namna hiyo.

“Aina zote mbili zinatarajia kuipatia Serikali kiasi cha Sh. bilioni 148. Aidha, shilingi bilioni 30 zitalipwa na makampuni ya simu ili kukamilisha makadirio ya mapato ya ushuru wa huduma za mawasiliano katika mwaka wa fedha 2013/13 ili kukamilisha mafungu ya bajeti iliyopitishwa ya maji na umeme vijijini,” alisema na kuongeza, hatua hiyo inatarajiwa kuipatia Serikali mapato ya Sh. bilioni 178,414.

Alisisitiza kwamba mapato yanayotokana na kodi hiyo hayajabadilishwa matumizi yake ya kugharimia huduma za maji na umeme vijijini kama ilivyopitishwa katika Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2013/14.

Hata hivyo, alisema kutokana na changamoto zilizojitokeza, Serikali itaendelea kuangalia namna bora ya kuongeza mapato ya ndani katika bajeti ya mwaka 2014/15.

Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM) alisema hali ya mapato ya nchi si shwari hali ambayo inalifanya taifa kuwa tegemezi na hivyo kutegemea misaada na mikopo.

Mbunge wa Mbozi Magharibi, David Silinde (Chadema), alisema malengo ya kodi hiyo ni mazuri lakini wananchi wanatakiwa kuona fedha zinazokusanywa zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.

Mbunge wa Kuteuliwa, James Mbatia (NCCR-Mageuzi), alitaka katika bajeti ya mwaka ujao, Serikali iangalie namna ya kupunguza gharama ushuru wa huduma hizo za mawasiliano ili zilingane au kufanana na nchi zingine za Afrika Mashariki ambazo alisema ni ndogo.

Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba, (CCM), alisema sekta ya mawasiliano ni muhimu na kiini katika maendeleo ya nchi hivyo ni Watanzania ni lazima waelimishwe kulipa kodi.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI :israel:
 
Kambi rasmi ya upinzani bungeni, imesema haiko tayari kuunga mkono Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Ushuru wa Bidhaa ya mwaka 2013, pamoja na kuongeza mapato ya Serikali - utaongeza mzigo wa kodi kwa wananchi wa kawaida ambao tayari wanaelemewa na mzigo mkubwa wa hali ngumu za maisha, vipato vya chini na umaskini mkubwa.

Imesema inaitaka Serikali ya CCM ihakikishe ushuru wa huduma za mawasiliano unaopendekezwa kwenye muswada huu, hautaongeza gharama za matumizi ya simu ambazo tayari ni kubwa sana.

Akisoma maoni ya kambi hiyo bungeni jana, Mbunge wa Viti Maalum, Christine Lissu, alitaka muswada huo kuwa na kifungu kitakachokataza makampuni ya simu kuhamishia gharama za ushuru wa huduma za mawasiliano kwa watumiaji wa huduma hizo na hivyo kuongeza gharama za matumizi ya simu.

"Ni dhahiri Kambi Rasmi ilipinga kuongeza ushuru kutoka asilimia 12 hadi asilimia 14.5, sasa muswada huu ambao umeletwa kwa hati ya dharura unaongeza ushuru kutoka asilimia 14.5 hadi asilimia 17.

"Ni Ushuru huu unaongezeka tena na ongezeko hili linaenda kwa watumiaji na sio kwa wamiliki wa makampuni ya simu," alisema.

Alisema kambi ya Upinzani inatambua ukweli kwamba, kwa sababu ya mapungufu ya kisheria yaliyopo sasa, makampuni ya simu yamekuwa yanalipia ushuru wa kupiga na kupokea simu tu, wakati makampuni hayo yakipata mapato makubwa kutokana na huduma za mawasiliano ambazo hazitozwi kodi.

Alisema kwa sababu hiyo, kambi hiyo inaelewa haja ya huduma za mawasiliano kuchangia ipasavyo katika mapato ya Serikali, kwa kupanua wigo wa huduma za mawasiliano zinazotozwa kodi.

Pamoja na kupinga, bunge lilipitisha muswada huo ambayo utaanza kutumika Januari mwakani.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
 
tunakabwa kila kona
_gas ya kupikia bei juu
_nauli ya hiace bei juu
_simu bei juu
_mashine za efd
___umeme bei juu
na maendeleo hayaonekani
 
Tutakamuliwa na kubebeshwa mizigo ya kodi mpaka tukome!

kodi.jpg

CCM wataiua nchi.jpg
 
tunakabwa kila kona
_gas ya kupikia bei juu
_nauli ya hiace bei juu
_simu bei juu
_mashine za efd
___umeme bei juu
na maendeleo hayaonekani
Tumefanywa majuha tu, tuliambiwa TRC ikibinafsishwa huduma zitaboreka zaidi. Hivi sasa ni majanga tu. Tukaambiwa gesi ikipatikana bei ya umeme itapungua kwa wateja. Hivi sasa ndio kwanza TANESCO hailali kwa kutaka kupandisha bei kwa mteja. Tukaambiwa waya wa 'optic' utapunguza bei kwa wateja. Hizi sasa serikali inahangaika kuongeza bei kwa mteja. Tutafanywa majuha mpaka lini?
 
Umesahau payee inakamua kila unapoongezwa senti na mwajiri,na benefits mbalimbali unazopata kwa mwajiri.halafu kuna watu 320 wasio lipa kodi ingawa sina hakika na sikia wachaguliwa wetu hawajui kitu kinaitwa payee.
 
This time around lazima hizi bei mpya zitawaamsha wananchi majuha waliolala usingizi wa pono unless kama wamelala kama maiti. 2015 lazima kitaeleweka tu.
 
Ili masikini aweze kuamka na kudai haki yake ni lazima akose namna y akuweza kujikimu, ili watanzania waweze kujua nchi ina tatizo ni lazima ifike siku watu wanakosa hela hata ya kununua mkate/chai/mlo mmoja, pesa zote wamechukua mabwana kodi.
Siku hiyo ikifika ndio "tipping point" ya maendeleo ya nchi itakapofikiwa.tulipo sana bado sana, tunalalamika lakini hatujafikia life and death situation,wanasema ukitaka kumjua paka funga mlango, so far CCM wameacha upenyo kidogo. Tuombe mungu waunfunge,Then watatujua sie "paka" tunamaanisha au laa tunaposema maisha magumu.
 
Ili masikini aweze kuamka na kudai haki yake ni lazima akose namna y akuweza kujikimu, ili watanzania waweze kujua nchi ina tatizo ni lazima ifike siku watu wanakosa hela hata ya kununua mkate/chai/mlo mmoja, pesa zote wamechukua mabwana kodi.
Siku hiyo ikifika ndio "tipping point" ya maendeleo ya nchi itakapofikiwa.tulipo sana bado sana, tunalalamika lakini hatujafikia life and death situation,wanasema ukitaka kumjua paka funga mlango, so far CCM wameacha upenyo kidogo. Tuombe mungu waunfunge,Then watatujua sie "paka" tunamaanisha au laa tunaposema maisha magumu.

mkuu, kamba ya ugumu wa maisha imekaba koo la kila mtanzania sawa sawa. mwaka 2015 lazima kitaeleweka tu.
 
Back
Top Bottom