Kodi ni sheria, sio matamko. Bunge, TRA na CAG Wanahusika!

tajirijasiri

JF-Expert Member
Oct 13, 2012
2,864
3,851
Mwanasiasa hupenda sifa na kufurahisha watu anaowaongoza. Sheria za kodi hutungwa na Bunge na baadae kusimamiwa na TRA. Ukubwa au unafuu wa kodi ni lazima uwe katika viwango na utetezi wa sheria na uhalisia. Majadiliano ya kikodi kati ya Afisa wa kodi na Mlipakodi ni haki na wajibu wa pande zote mbili.

Endapo Serikali inataka kodi halali yenye mizania sawa, basi itunge sheria, kanuni na miongozo rafiki, ili huyo mkusanya kodi, aenende vile Mamlaka inavyotaka.

Ukubwa au unafuu wa makadirio hutegemea sana ulipaji kodi wa hiari wa mlipakodi. Ukwepaji kodi wa muda mrefu hupelekea malimbikizo ya kodi, riba na adhabu na hivyo kodi kuwa kubwa.

Endapo Afisa wa kodi akapunguza kiwango cha kulipa, chini ya kiwango halisi anachostahili mlipakodi, basi serikali hiyo hiyo itambana tena kupitia CAG/NAOT. Na pengine kodi ikaongezeka tena au muda mreeeefu wa utetezi ukachukua muda wa Afisa na Mlipakodi katika kujibu hoja.

Tunapotamka kodi, hatuishii kwa TRA/ Afisa wa kodi pekee yake, hata CAG/ Mkaguzi na Bunge wahusishwe pia.
 
Usiwatetee TRA.

Kicheere, Mkuu wa TRA ni mtu hopeless. Hata wafanyakazi wengi pale TRA wanatamani kuondoka.

Hizo taratibu mbona zilikuwapo Awamu zote zilizopita?

Tujiulize sababu za watu kufunga biashara na hivyo tax base kupungua sana.

Msimamo kuwa mfanyabiashara ni mpiga dili hivyo apigwe kodi za kienda wazimu, matokeo yake tunayaona sasa.
 
Ukiwa Mfanyabiashara utaelewa alichoongea jiwe kinachotakiwa ni urafiki kati ya wakusanya kodi na walipa kodi sio kama sasa wamekua maadui na kulipishana kodi kubwa ambayo wengine hawawezi kuilipa wanaishia kufunga duka.

Kwenye Income Tax act kuna baadhi ya section zinazungumzia TRA kutoa Elimu ya kutosha kwa walipa kodi ni jukumu lao na pia kinachoendelea kwenye makadirio ni kwamba kila mwaka wao wanaamini biashara yako imekua kwa hiyo unapandishwa kiwango cha kulipa kodi kwa mwaka.

Sasa maafisa wa kodi wasio waaminifu wanachukua mpunga kwa kukadiria ambayo mfanyabiashara ana uwezo nayo wakati kimsingi bila hata rushwa alitakiwa alipe hiyo hiyo wakishindana kwa haki wengine wanafunga fremu.

Ili kupata wigo mpana wa kukusanya kodi ni kuwa na wafanyabiashara wengi wanaolipa kidogo na kati sio kama sasa wengi fremu wamefunga wamekua machinga na kodi hawalipi na wana mitaji mikubwa bara barani...
 
Huyo Jamaa ni zero brain zaidi ya ubabe wa kuwakomoa wafanyabiashara kutaka sifa kwa bosi mpitaji, ajui ushawishi wa kulipa kodi,ktk uongozi wake ndipo maduka na biashara nyingi sana watu wamefunga kuhamisha nje biashara zao.
Usiwatetee TRA.
Kichere mkuu wa TRA ni mtu hopeless.
Hata wafanyakazi wengi pale TRA wanatamani kuondoka.

Hizo taratibu mbona zilikuwapo Awamu zote zilizopita?

Tujiulize sababu za watu kufunga biashara na hivyo tax base kupungua sana.

Msimamo kuwa mfanyabiashara ni mpiga dili hivyo apigwe kodi za kienda wazimu, matokeo yake tunayaona sasa.
 
Unachoongea siyo kweli.
Maafisa wa TRA WANAPANGIWA MALENGO ya kukusanya kodi.
Hiyo kodi wanaipataje toka kwa "wapiga dili" wanajua wenyewe.
Na msimamo huo sasa umebuma rasmi.
Mkuu hakuna unachokijua wanapangiwa kwa ujumla na kwa kila kipindi na wamepanga kodi kwa kila eneo mfano duka la nguo likiwa mjini kodi yake ni tofauti na duka la nguo lililopo nje ya mji kiwango cha kukusanya kodi Namanga malengo waliyowekewa ni tofauti na Tunduma,Kasumuru au holili boarder maafisa TRA ndio chanzo cha kuua biashara Tanzania...
 
Mwanasiasa hupenda sifa na kufurahisha watu anaowaongoza. Sheria za kodi hutungwa na Bunge na baadae kusimamiwa na TRA. Ukubwa au unafuu wa kodi ni lazima uwe katika viwango na utetezi wa sheria na uhalisia. Majadiliano ya kikodi kati ya Afisa wa kodi na Mlipakodi ni haki na wajibu wa pande zote mbili.

Endapo Serikali inataka kodi halali yenye mizania sawa, basi itunge sheria, kanuni na miongozo rafiki, ili huyo mkusanya kodi, aenende vile Mamlaka inavyotaka.

Ukubwa au unafuu wa makadirio hutegemea sana ulipaji kodi wa hiari wa mlipakodi. Ukwepaji kodi wa muda mrefu hupelekea malimbikizo ya kodi, riba na adhabu na hivyo kodi kuwa kubwa.

Endapo Afisa wa kodi akapunguza kiwango cha kulipa, chini ya kiwango halisi anachostahili mlipakodi, basi serikali hiyo hiyo itambana tena kupitia CAG/NAOT. Na pengine kodi ikaongezeka tena au muda mreeeefu wa utetezi ukachukua muda wa Afisa na Mlipakodi katika kujibu hoja.

Tunapotamka kodi, hatuishii kwa TRA/ Afisa wa kodi pekee yake, hata CAG/ Mkaguzi na Bunge wahusishwe pia.

Mfano ni tamko la Waziri la msamha wa 'riba na adhabu'

Tamko la waziri linasema msahamaha ni wa muda wa mwaka mmoja, na kodi(principal) italipwa kabla ya June 30 2019. Lakini sheria ya TRA hairuhusu installments kulipwa nje ya miezi 6.

Yaani ni kizungumkuti.....
 
Ukweli ni kwamba inabidi sheria zibadilishwe sio kuongea ongea jukwaani tu, kufurahisha watu wasio na uelewe fikiria unanunua gari $2500 unatakiwa ulipe kodi $3000 au unakuta hio gari ulionunua weww $2500 upande wa TRA wao Customs Value yao ipo $4200 mfano halisi gari ya bei nafuu 2006 BMW 320i ya 2006 ushuru wake ni milioni 10 haijalishi umenunua milioni 1,2,au 4 bei wanapanga wao, Tanzania kuna kodi kandamizi nyingi sana
 
Ukiwa Mfanyabiashara utaelewa alichoongea jiwe kinachotakiwa ni urafiki kati ya wakusanya kodi na walipa kodi sio kama sasa wamekua maadui na kulipishana kodi kubwa ambayo wengine hawawezi kuilipa wanaishia kufunga duka.

Kwenye Income Tax act kuna baadhi ya section zinazungumzia TRA kutoa Elimu ya kutosha kwa walipa kodi ni jukumu lao na pia kinachoendelea kwenye makadirio ni kwamba kila mwaka wao wanaamini biashara yako imekua kwa hiyo unapandishwa kiwango cha kulipa kodi kwa mwaka.

Sasa maafisa wa kodi wasio waaminifu wanachukua mpunga kwa kukadiria ambayo mfanyabiashara ana uwezo nayo wakati kimsingi bila hata rushwa alitakiwa alipe hiyo hiyo wakishindana kwa haki wengine wanafunga fremu.

Ili kupata wigo mpana wa kukusanya kodi ni kuwa na wafanyabiashara wengi wanaolipa kidogo na kati sio kama sasa wengi fremu wamefunga wamekua machinga na kodi hawalipi na wana mitaji mikubwa bara barani...
Tatizo lake anataka kupendwa na machinga , badala ya kuweka utaratibu wa kujenga masoko maalum kwa vijana kufanya biashara yeye anasema vijana wafanye biashara hata barabatani.

Hawa vijana hawalipi kodi na hata wanayosema watawapa vitambulisho bado wafanya biashara wakubwa watawatumia machinga kukwepankodi.

Tatizo matamko yake ndio yametufikisha hapa.
 
Sheria za kodi huandaliwa na maafisa wa kodi na kupelekwa bungeni kupitishwa na kusainiwa na raisi kuwa sheria! Kodi kama ni kubwa au haziendani na uhalisia wa uchumi au bishara wa kulaumiwa ni TRA hilo hawezi kwepa.Hao wengine wote wana base kwenye proffession za watu wa TRA
 
Mwanasiasa hupenda sifa na kufurahisha watu anaowaongoza. Sheria za kodi hutungwa na Bunge na baadae kusimamiwa na TRA. Ukubwa au unafuu wa kodi ni lazima uwe katika viwango na utetezi wa sheria na uhalisia. Majadiliano ya kikodi kati ya Afisa wa kodi na Mlipakodi ni haki na wajibu wa pande zote mbili.

Endapo Serikali inataka kodi halali yenye mizania sawa, basi itunge sheria, kanuni na miongozo rafiki, ili huyo mkusanya kodi, aenende vile Mamlaka inavyotaka.

Ukubwa au unafuu wa makadirio hutegemea sana ulipaji kodi wa hiari wa mlipakodi. Ukwepaji kodi wa muda mrefu hupelekea malimbikizo ya kodi, riba na adhabu na hivyo kodi kuwa kubwa.

Endapo Afisa wa kodi akapunguza kiwango cha kulipa, chini ya kiwango halisi anachostahili mlipakodi, basi serikali hiyo hiyo itambana tena kupitia CAG/NAOT. Na pengine kodi ikaongezeka tena au muda mreeeefu wa utetezi ukachukua muda wa Afisa na Mlipakodi katika kujibu hoja.

Tunapotamka kodi, hatuishii kwa TRA/ Afisa wa kodi pekee yake, hata CAG/ Mkaguzi na Bunge wahusishwe pia.
tajirijasiri, ni kitu gani siyo sheria? ni kweli kabisa makadirio ya kodi ni makubwa sana. AIDHA watumishi wa TRA ni miungu watu NA WEZI KWA KUTUMIA MGONGO WA SHERIA imeawapa mamalaka
 
Tatizo lake anataka kupendwa na machinga , badala ya kuweka utaratibu wa kujenga masoko maalum kwa vijana kufanya biashara yeye anasema vijana wafanye biashara hata barabatani.

Hawa vijana hawalipi kodi na hata wanayosema watawapa vitambulisho bado wafanya biashara wakubwa watawatumia machinga kukwepankodi.
.
Machinga ndie pekee anayejua maana ya Customer care.Anamfuata mteja aliko tofauti na hao wakaa masokoni na madukani wakiwa wametoa macho kwenye fremu zao kama mjusi aliyefiwa na mkwewe wakisubiri mteja wasiemjua aje anunue!!!!

Biashara kubwa wanaofanya iende ni machinga vinginevyo bidhaa nyingi zingewadodea wafanyabiashara.Machinga ndio hata wana introduce bidhaa mpya kwa wateja ambayo bila wao wateja wasingeijua.Ukiwa na bidhaa ukitaka i move faster mkabidhi machinga.Raisi kuRuhusu machinga ni kuwasaidia wafanyabiashara biashara zao zitoke ziuzike.Hawa machinga si tishio kwa wafanyabiashara sababu bidhaa wanazouza wanatoa kwa wafanyabiashara wenyewe waagizaji nje nk

Kukaa dukani ukisubiri wateja ushamba labda uwe unauza mabomu
 
Hivi huu msamaha wa kodi unaendelea?
Mfano ni tamko la Waziri la msamha wa 'riba na adhabu'

Tamko la waziri linasema msahamaha ni wa muda wa mwaka mmoja, na kodi(principal) italipwa kabla ya June 30 2019. Lakini sheria ya TRA hairuhusu installments kulipwa nje ya miezi 6.

Yaani ni kizungumkuti.....
 
Machinga ndie pekee anayejua maana ya Customer care.Anamfuata mteja aliko tofauti na hao wakaa masokoni na madukani wakiwa wametoa macho kwenye fremu zao kama mjusi aliyefiwa na mkwewe wakisubiri mteja wasiemjua aje anunue!!!!

Biashara kubwa wanaofanya iende ni machinga vinginevyo bidhaa nyingi zingewadodea wafanyabiashara.Machinga ndio hata wana introduce bidhaa mpya kwa wateja ambayo bila wao wateja wasingeijua.Ukiwa na bidhaa ukitaka i move faster mkabidhi machinga.Raisi kuRuhusu machinga ni kuwasaidia wafanyabiashara biashara zao zitoke ziuzike.Hawa machinga si tishio kwa wafanyabiashara sababu bidhaa wanazouza wanatoa kwa wafanyabiashara wenyewe waagizaji nje nk

Kukaa dukani ukisubiri wateja ushamba labda uwe unauza mabomu
Mkuu umewaza vyema lakini lazima kuwe nantaratibu ili uweze kupata kodi..
 
Ukweli ni kwamba inabidi sheria zibadilishwe sio kuongea ongea jukwaani tu, kufurahisha watu wasio na uelewe fikiria unanunua gari $2500 unatakiwa ulipe kodi $3000 au unakuta hio gari ulionunua weww $2500 upande wa TRA wao Customs Value yao ipo $4200 mfano halisi gari ya bei nafuu 2006 BMW 320i ya 2006 ushuru wake ni milioni 10 haijalishi umenunua milioni 1,2,au 4 bei wanapanga wao, Tanzania kuna kodi kandamizi nyingi sana
Kodi upende wa magari huwa sielewi wanatumia kanuni gani
 
Mkuu umewaza vyema lakini lazima kuwe nantaratibu ili uweze kupata kodi..
Wafanyabiashara wanalipa kodi mzigo haupiti babdarini bila kodi na machinga akienda kununua mitumba yake mitano ya kutembea dukani analipa kodi sasa unataka hata huyo machinga mwenye nguo tano mkononi alipe kodi? Nilishawahi gombana na maafisa wa TRA nilinunua viatu pair kumi nairobi.Vya kuvaa mwenyewe nikaambiwa wakati wa kupanda basi kuwa nivitoe kwenye maboksi yake ili nisipate shida upande wa Tanzania watanilipisha kodi na wataleta usumbufu KWENYE BASI LAO nikakataa kuvitoa kwenye maboxi yake.Wakaniambia sawa ila kukitokea usumbufu sisi basi tutaondoka tukuache na TRA WAKO.Tukafika namanga tukatoa masanduku kukaguliwa nikakutwa na viatu pair 10 kwenye maboxi yake sandukuni wakaniambia nitoe document wapige kodi nikauliza namba ya kamishina wa TRA wakasema unaitaka ya nini? nikawaambia nataka nimuulize mtanzania anatakiwa awe na pair ngapi za viatu vya kuvaa kwa sheria ya TRA? Kuwa akiwa na pair kumi ni mfanyabishara mkubwa wa viatu ambaye akilipa nauli ya Nairobi kwenda na kurudi na kukaa hoteli hizo pair kumi ni biashara kubwa ya faida kwake na kwa TRA? Kilchofuata alikuja bosi wao mzee mmoja akasema nenda tu siku ingine uliza tu taratibu ni mambo tu ya kueleweshana wewe si mungu na sisi si miungu tunaweza kosea au waweza kosea .
Kwa hiyo wewe unataka huyo machinga mwenye nguo tano mkononi alipe TRA?
 
Machinga ndie pekee anayejua maana ya Customer care.Anamfuata mteja aliko tofauti na hao wakaa masokoni na madukani wakiwa wametoa macho kwenye fremu zao kama mjusi aliyefiwa na mkwewe wakisubiri mteja wasiemjua aje anunue!!!!

Biashara kubwa wanaofanya iende ni machinga vinginevyo bidhaa nyingi zingewadodea wafanyabiashara.Machinga ndio hata wana introduce bidhaa mpya kwa wateja ambayo bila wao wateja wasingeijua.Ukiwa na bidhaa ukitaka i move faster mkabidhi machinga.Raisi kuRuhusu machinga ni kuwasaidia wafanyabiashara biashara zao zitoke ziuzike.Hawa machinga si tishio kwa wafanyabiashara sababu bidhaa wanazouza wanatoa kwa wafanyabiashara wenyewe waagizaji nje nk

Kukaa dukani ukisubiri wateja ushamba labda uwe unauza mabomu
Kwa huu ushauri wako serikali itapataje kodi kwa mfanyabiashara?
 
Back
Top Bottom