ChikoTz
Member
- Feb 26, 2019
- 37
- 33
Mkongomana wa Yanga ambae ndiye Kocha Mkuu Mwinyi Zahera amefunguka na kuipa asilimia 60 klabu ya Simba kufuzu hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Aidha ametoa asilimia 40 kwa klabu ya AS Vita kufuzu robo fainali katika kundi D ambalo lina timu zingine ambazo ni Al Ahly na JS Saoura.
Mkongomani huyo amedai Vita hata akishinda mchezo wake dhidi ya Al Ahly na Simba ikapoteza mbele ya Saoura bado itakuwepo.
Ameenda mbali zaidi na kusema kuwa Simba wana nafasi kubwa ya kushinda mchezo wa mwisho na kuweza kufuzu robo fainali dhidi ya Vita itakayopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Tayari kikosi cha Simba kipo angani hivi sasa kikielekea Algeria kwa ajili ya mechi na Saoura ukiwa ni mchezo wa pili baada ya ule wa kwanza Simba kushinda mabao 3-1
Sent using Jamii Forums mobile app
Aidha ametoa asilimia 40 kwa klabu ya AS Vita kufuzu robo fainali katika kundi D ambalo lina timu zingine ambazo ni Al Ahly na JS Saoura.
Mkongomani huyo amedai Vita hata akishinda mchezo wake dhidi ya Al Ahly na Simba ikapoteza mbele ya Saoura bado itakuwepo.
Ameenda mbali zaidi na kusema kuwa Simba wana nafasi kubwa ya kushinda mchezo wa mwisho na kuweza kufuzu robo fainali dhidi ya Vita itakayopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Tayari kikosi cha Simba kipo angani hivi sasa kikielekea Algeria kwa ajili ya mechi na Saoura ukiwa ni mchezo wa pili baada ya ule wa kwanza Simba kushinda mabao 3-1
Sent using Jamii Forums mobile app