Kocha wa taifa star afuate nyayo za maadam ritha wa bongo star search au tusker proje

Lu-ma-ga

JF-Expert Member
Sep 21, 2010
4,780
3,227
Watanzania ni vema tukampatia ushauri wa bure kocha wetu wa timu ya taifa ili afuate nyayo za Maadam Ritha anavyofanya katika kutafuta vipaji badala ya kutegemea wachezaji waliochwa na MAXIMO.
Ni vema kocha wetu akafanya zoezi la kuzunguka nchi nzima kutafuta vipaji vya kweli ili aweze kupata wachezaji wenye vipaji vya akina Lunyamila, Hussein Masha, Mao Mkami, George Masatu na kama akina Charles Mkwasa.

Nimekuwa nikishuhudia jinsi vipaji vya waimbaji wa muziki wanavyopatikana kutokana na ubunifu wa Maadam Rirtha alivyoweza kuwaibua akina RODGERS, MISOJI NKWABI, LEAH MOOD, PASCHAL CASSIAN na kijana machachari Msechu anayetikisa TUSKER FAME PROJECT ya EA.

Ninamshauri kocha wetu atembee nchi nzima afanye utaratibu wa kuwaita vijana katika kila mkoa na kuwafanyia majaribio ya kumiliki mpira kama vile danadana, kupiga vichwa na umilikaji kwa ujumla.Hii ingemsaidia kukusanya japo vijana 10 kila mkoa na baadae angefanya zoezi la kuwakusanya kambini na kuwachuja na kubaki na idadi anayohitaji kwa kuwatumia makocha mabalimbali kama majaji wa kutoa maksi kwa kila kijana wakati wa mchujo ili baadae anabaki na wachache kulingana na jinsi watakavyofaulu kufikia viwango walivyojiwekea.
hAPO atapata timu ya taifa yenye uwakilishi wa kila kona ya nchi kama anavyofanya MAADA Rirtha wa BONGOSTAR SEARCH.

Karibu tujadili
 
hata hao unaowasema hamna la maana walilofanya zaidi ya kutoa burudani kwenye tv. Ni msanii yupi aliyeshinda hayo mashindano na akawa msanii wa kweli?J4? Nkwabi? Casian? Nadhani hapa huwa tunaona temporary talents na sio uhalisia. Kwani mpira ni danadana au vichwa?
Labda ungezungumzia umakini wa kummarki adui,kasi,stamina,uwezo wa kutoa pasi sahihi,nidhamu nk.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom