Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,906
- 22,038
Kocha Ivory Coast: Nipeni Taifa Stars
Kocha wa timu ya taifa ya Ivory Coast Vahid Halilhodzic ambaye ametangaza nia yake ya kutaka kubeba mikoba ya Marcio Maximo ambaye anatarajia kumaliza mkataba wake wa kuinoa timu ya Taifa stars hivi karibuni.
Vicky Kimaro
KOCHA wa timu ya taifa ya Ivory Coast, 'The Elephants' Vahid Halilhodzic amesema yupo tayari kubeba mikoba ya Marcio Maximo iwapo Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), litamuhitaji.
Kocha huyo aliiongoza nchi hiyo kucheza fainali za Afrika zinazoanza kesho nchini Angola na Kombe la Dunia baadaye Juni. Timu hiyo iliyoweka kambi nchini, iliondoka jana kwenda Angola.
Akizungumza na waandishi wa habari juzi mara baada ya mechi yao na Rwanda ambayo Ivory Coast walitoka kifua mbele kwa mabao 2-0, Halilhodzic alisema mkataba wake na Ivory Coast unamalizika mara baada ya fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika nchini Afrika Kusini.
"Mkataba wangu unamalizika baada ya Kombe la Dunia, nimeshapata maombi mengi sana, Tanzania kama nao wataomba naweza kuwafikiria nikaja kufundisha.
"Nimeiona ni nchi nzuri yenye amani,"alisema Holilhodzic raia wa Bosnia alipoulizwa swali iwapo atakuwa tayari kuja kurithi mikoba ya Mbrazil Marcio Maximo ambaye mkataba wake unamalizika mwishoni mwa Juni.
Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, kwa kushirikiana na serikali wameanza mchakato wa kumsaka kocha atakayerithi mikoba ya Mbrazil huyo.
Akizungumzia kiwango cha wachezaji wa Tanzania Holilhodzic ambaye ameshahaidi kurudi nchini kulipeleka Kombe la Mataifa ya Afrika kileleni mlima Kilimanjaro iwapo watalitwaa, alisema: "Tanzania ina uwanja mzuri lakini haina wachezaji wazuri, kama mnataka mafanikio ni lazima mfanye kazi sana, wa ya ziada, wachezaji wenu wamekosa mbinu na uwezo wa kujiamini.
"Tengenezeni safu ya ushambuliaji kuwe na washambuliaji watatu au wanne, badala ya kuishia kulinda goli, timu kama Ivory Coast inatumia washambuliaji watatu, mnapokutana na timu kama hii ni ngumu sana kushinda.
"Ni lazima mfungwe kwa sababu inashambulia sana, mnabaki mkilinda goli," alisema.
Akizungumzia mchezo wao na Rwanda, Holilhodzic alisifu kiwango cha Rwanda ingawa alidai vipo sawa na Tanzania kwani haikuwa rahisi kwao kushinda mchezo huo kwani wachezaji wake walitengeneza nafasi nyingi lakini kuna wakati washambuliaji wake walimuangusha.
Alisema ushindi wa mechi hiyo, umempa faraja kubwa kwani ni mechi yake ya 10 kushinda kati ya mechi za kirafiki walizocheza na hawajapoteza mchezo hata mmoja, hivyo anatumaini kufanya vizuri kwenye michuano ya Mataifa ya Afrika
Kocha wa timu ya taifa ya Ivory Coast Vahid Halilhodzic ambaye ametangaza nia yake ya kutaka kubeba mikoba ya Marcio Maximo ambaye anatarajia kumaliza mkataba wake wa kuinoa timu ya Taifa stars hivi karibuni.
Vicky Kimaro
KOCHA wa timu ya taifa ya Ivory Coast, 'The Elephants' Vahid Halilhodzic amesema yupo tayari kubeba mikoba ya Marcio Maximo iwapo Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), litamuhitaji.
Kocha huyo aliiongoza nchi hiyo kucheza fainali za Afrika zinazoanza kesho nchini Angola na Kombe la Dunia baadaye Juni. Timu hiyo iliyoweka kambi nchini, iliondoka jana kwenda Angola.
Akizungumza na waandishi wa habari juzi mara baada ya mechi yao na Rwanda ambayo Ivory Coast walitoka kifua mbele kwa mabao 2-0, Halilhodzic alisema mkataba wake na Ivory Coast unamalizika mara baada ya fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika nchini Afrika Kusini.
"Mkataba wangu unamalizika baada ya Kombe la Dunia, nimeshapata maombi mengi sana, Tanzania kama nao wataomba naweza kuwafikiria nikaja kufundisha.
"Nimeiona ni nchi nzuri yenye amani,"alisema Holilhodzic raia wa Bosnia alipoulizwa swali iwapo atakuwa tayari kuja kurithi mikoba ya Mbrazil Marcio Maximo ambaye mkataba wake unamalizika mwishoni mwa Juni.
Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, kwa kushirikiana na serikali wameanza mchakato wa kumsaka kocha atakayerithi mikoba ya Mbrazil huyo.
Akizungumzia kiwango cha wachezaji wa Tanzania Holilhodzic ambaye ameshahaidi kurudi nchini kulipeleka Kombe la Mataifa ya Afrika kileleni mlima Kilimanjaro iwapo watalitwaa, alisema: "Tanzania ina uwanja mzuri lakini haina wachezaji wazuri, kama mnataka mafanikio ni lazima mfanye kazi sana, wa ya ziada, wachezaji wenu wamekosa mbinu na uwezo wa kujiamini.
"Tengenezeni safu ya ushambuliaji kuwe na washambuliaji watatu au wanne, badala ya kuishia kulinda goli, timu kama Ivory Coast inatumia washambuliaji watatu, mnapokutana na timu kama hii ni ngumu sana kushinda.
"Ni lazima mfungwe kwa sababu inashambulia sana, mnabaki mkilinda goli," alisema.
Akizungumzia mchezo wao na Rwanda, Holilhodzic alisifu kiwango cha Rwanda ingawa alidai vipo sawa na Tanzania kwani haikuwa rahisi kwao kushinda mchezo huo kwani wachezaji wake walitengeneza nafasi nyingi lakini kuna wakati washambuliaji wake walimuangusha.
Alisema ushindi wa mechi hiyo, umempa faraja kubwa kwani ni mechi yake ya 10 kushinda kati ya mechi za kirafiki walizocheza na hawajapoteza mchezo hata mmoja, hivyo anatumaini kufanya vizuri kwenye michuano ya Mataifa ya Afrika