KLM na Etihad miongoni mwa ndege zilizopigwa marufuku kuingia Nigeria

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,000
9,862
Abiria


Safari za ndege ndani ya Nigeria zilirejelewa
Nigeria imepiga marufuku mashirika ya ndege kutokanchi kadhaa kuhudumu nchini humo kuanzia Jumamosi hii.

Mashirika kumi ya ndege yamezuiliwa kuhudumu- Ikiwemo Air France, KLM kutoka Uholanzi, Lufthansa kutoka Ujerumani, na Etihad Airways ya Milki za kiarabu.
Hii ni kwasababu Wanigeria walio na viza ya watalii hawaruhusiwi kuingia katika nchi hizo.

Nigeria ilisema kwamba italipiza kisasi hatua ya kuwapiga marufuku raia wake kuingia katika nchi hizo.

Baadhi ya mashirika ya ndege yamezuiliwa kuhudumu nchini Nigeria kwasababu nchi zao hazijarejelea safari za abiri kimataifa.

Lakini mashirika 14 ya ndege yataruhusiwa kuhudumu nchini humo mionngo mwa hzo ni British Airways, Virgin Atlantic, Turkish Airlines, Qatar Airways na Ethiopian Airlines.
Abiria wataruhusiwa nchini humo chini ya mashari makali

BBC
 
Back
Top Bottom