Raia Mwema - Gazeti Jipya Kabisa la Kiswahili Kuingia Tanzania Kuanzia Tarehe 31 Oktoba

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,460
39,928
Gazeti jipya kabisa la Kiswahili linatarajiwa kuingia katika vibanda, maofisi, na mitaa ya Tanzania kuanzia tarehe 31 Oktoba mwaka huu. Jarida hilo la "Raia Mwema" litakuwa na habari mbalimbali zikiwemo za uchunguzi, utafiti, siasa, biashara, maoni n.k Jarida hilo liitwalo "Raia Mwema" limeanzishwa kutokana michango ya hali, mali, na vipaji ambavyo vimekusanywa chini ya Mhariri wake Mtendaji John Bwire

Kuanzishwa kwa jarida hilo ni alama ya kuvunjika rasmi kwa ndoa ya gazeti lililosifika sana nchini miaka hiyo la "Rai".
Waandishi waanzilishi wa gazeti la Rai - ukiondoa Dr. Shoo na Salva - na waandishi wengine ndani na nje ya Tanzania wamefikia uamuzi wa kuanzisha gazeti hilo wakizingatia haja ya kupanua uhuru wa maoni, habari na mawazo na kuchangia kwa namna ya pekee kuhamasisha kizazi kipya cha "Raia Wema".

Gazeti hilo litajumuisha waandishi mbalimbali wakiwemo:

Jenerali Ulimwengu
Issa Shivji
Padre Karugendo
Prof. Haroub Othman
Maggid Mjenga
Joseph Mihangwa

na wenu mtiifu, na wengine wengi ambao mtapata bahati ya kusoma kazi zao kwenye gazeti hilo ambalo litapatikana pia kwenye mtandao wakati huo.

Napenda kutoa pongezi kwa ushirikiano wote wa wale ambao wamewezesha gazeti hili kupata mtaji, kibali, na nyenzo za kutendea kazi.. Natarajia kuwa toleo la kwanza litaiweka fani ya uandishi katika ngazi nyingine kabisa nchini.

Tafadhali copy na watumie wabongo walioko kwenye orodha yako ya anuani.

Ndugu yenu,

M. M.
 
Haya Mzee mtiifu weka mambo. Good work, unafahamu unapofanya kazi nzuri usingoje kulipwa hapa duniani.
 
..tulikuwa tumeshakosa yale tuliyohitaji kwenye rai!

..hiyo list hapo inaashiria kwamba habari makini zitaendelea kupatikana!

..kazi nzuri na kila la heri!

..tanzania inahitaji raia watiifu kwa maslahi ya nchi yao!
 
Gazeti jipya kabisa la Kiswahili linatarajiwa kuingia katika vibanda, maofisi, na mitaa ya Tanzania kuanzia tarehe 31 Oktoba mwaka huu. Jarida hilo la "Raia Mwema" litakuwa na habari mbalimbali zikiwemo za uchunguzi, utafiti, siasa, biashara, maoni n.k Jarida hilo liitwalo "Raia Mwema" limeanzishwa kutokana michango ya hali, mali, na vipaji ambavyo vimekusanywa chini ya Mhariri wake Mtendaji Francis Chirwa.

Kuanzishwa kwa jarida hilo ni alama ya kuvunjika rasmi kwa ndoa ya gazeti lililosifika sana nchini miaka hiyo la "Rai".
Waandishi waanzilishi wa gazeti la Rai - ukiondoa Dr. Shoo na Salva - na waandishi wengine ndani na nje ya Tanzania wamefikia uamuzi wa kuanzisha gazeti hilo wakizingatia haja ya kupanua uhuru wa maoni, habari na mawazo na kuchangia kwa namna ya pekee kuhamasisha kizazi kipya cha "Raia Wema".

Gazeti hilo litajumuisha waandishi mbalimbali wakiwemo:

Jenerali Ulimwengu
Issa Shivji
Padre Karugendo
Prof. Haroub Othman
Maggid Mjenga
Joseph Mihangwa

na wenu mtiifu, na wengine wengi ambao mtapata bahati ya kusoma kazi zao kwenye gazeti hilo ambalo litapatikana pia kwenye mtandao wakati huo.

Napenda kutoa pongezi kwa ushirikiano wote wa wale ambao wamewezesha gazeti hili kupata mtaji, kibali, na nyenzo za kutendea kazi.. Natarajia kuwa toleo la kwanza litaiweka fani ya uandishi katika ngazi nyingine kabisa nchini.

Tafadhali copy na watumie wabongo walioko kwenye orodha yako ya anuani.

Ndugu yenu,

M. M.


mmkjj.....

gud job,kuweni makini msije mkafa kifo cha mende.
 
wataanza vizuri na kwa vishindo then itakuwa kama magazeti ya kawaida. Lakini thats a good start though.
 
Hiyo orodha ya waandishi wa gazeti hilo imetulia. Naamini tutapata mengi.. keep on!
 
Hii ni habari njema kwa kweli. In July 2007, I went back to my beloved country Tanzania to greet the sons and daughters of the land. I bought "RAI" thinking it was carrying the same weight it used to have, Loh! what a disappointment. Welcome "RAIA MWEMA"
 
Mwanakijiji,

Hongera kwa juhudi zenu za kuanzisha gazeti. Ushauri tu, jieupusheni na wanasiasa wa pande zote. Mkitaka kuliua gazeti lenu baada ya muda mfupi basi kuweni BIASED kwenye haya mambo ya siasa.

Mkitumia usemi wa FMES, "Kumkoma Nyani Giladi" naona mtafanikiwa.

Jambo baya ni baya tu bila kujali limefanywa na CCM au Upinzani, huo ndio msimamo ambao baadhi yetu tungetaka magazeti ya maana TZ yaufuate.

Mafanikio mema.
 
Ninahakika litapendwa sana, kwa sababu watu walio kwenye gazeti hilo si mchezo
 
Hii ni habari njema. Kipaji cha Ulimwengu na umahiri wa akina Shivji na Othman ni vema umepata platform.

Nimepata hisia kwamba Rostam kanunua mbuzi kwenye gunia.
 
Gazeti jipya kabisa la Kiswahili linatarajiwa kuingia katika vibanda, maofisi, na mitaa ya Tanzania kuanzia tarehe 31 Oktoba mwaka huu. Jarida hilo la "Raia Mwema" litakuwa na habari mbalimbali zikiwemo za uchunguzi, utafiti, siasa, biashara, maoni n.k Jarida hilo liitwalo "Raia Mwema" limeanzishwa kutokana michango ya hali, mali, na vipaji ambavyo vimekusanywa chini ya Mhariri wake Mtendaji Francis Chirwa.[/QUOTE]

Habari nilizozipata ni kwamba Mhariri Mtendaji anatarajiwa kuwa John Bwire, ambaye alikua kinara wa RAI na bahati mbaya sana Francis Chirwa bado yuko Habari Corporation. Upo uwezekano naye akaacha kazi huko soon.
 
Hio orodha ya wachangiaji inavutia sana, nadhani litakuwa ni gazeti makini sana. Ila sasa Mwanakijiji hujasema kama ni la kila siku ama la kila wiki.
Tupo tayari kulipokea.
 
Habari nilizozipata ni kwamba Mhariri Mtendaji anatarajiwa kuwa John Bwire, ambaye alikua kinara wa RAI na bahati mbaya sana Francis Chirwa bado yuko Habari Corporation. Upo uwezekano naye akaacha kazi huko soon.

Need I say more?
 
Gazeti jipya kabisa la Kiswahili linatarajiwa kuingia katika vibanda, maofisi, na mitaa ya Tanzania kuanzia tarehe 31 Oktoba mwaka huu. Jarida hilo la "Raia Mwema" litakuwa na habari mbalimbali zikiwemo za uchunguzi, utafiti, siasa, biashara, maoni n.k Jarida hilo liitwalo "Raia Mwema" limeanzishwa kutokana michango ya hali, mali, na vipaji ambavyo vimekusanywa chini ya Mhariri wake Mtendaji Francis Chirwa.[/QUOTE]

Habari nilizozipata ni kwamba Mhariri Mtendaji anatarajiwa kuwa John Bwire, ambaye alikua kinara wa RAI na bahati mbaya sana Francis Chirwa bado yuko Habari Corporation. Upo uwezekano naye akaacha kazi huko soon.


Halisi, inawezekana pia Deo Balile akajiunga huko nini? Maana nimeona akiaga kule Tanzania Daima (http://www.freemedia.co.tz/daima/2007/10/21/makala3.php) na kwaba anarejea nchini kutoka UK...najaribu kujumlisha mambo hapa.....
 
Halisi, inawezekana pia Deo Balile akajiunga huko nini? Maana nimeona akiaga kule Tanzania Daima (http://www.freemedia.co.tz/daima/2007/10/21/makala3.php) na kwaba anarejea nchini kutoka UK...najaribu kujumlisha mambo hapa.....

Balile ni mwandishi mzuri sana na pengine angeweza kuwa mmoja wa waandishi waanzilishi lakini sijasikia kwenda huko zaidi ya kusikia kwamba anakwenda kuimarisha Mtanzania kwa kushirikiana na rafiki yake Manyerere Jackton. Balile angefaa sana Raia Mwema kwa kuwa ana historia ya kuanzisha gazeti na kufanikiwa. Balile alikua katika timu iliyoanzisha Mwananchi kwa shida sana na baadaye katika Tanzania Daima. Mengine ambayo si dhahiri hayana nafasi hapa kama ambavyo mwenyewe hakupenda kuyataja, ila kuna mengi yaliyomsukuma kuondoka Tanzania Daima na kwenda Mtanzania. Kwa nia ya kujenga si vyema kujadili sababu za kuondoka kwake zaidi ya kumpongeza na kumtakia kila la kheir ili aweze kutekeleza majukumu yake mapya. Sitashangaa pia kama hatakwenda Mtanzania na akapewa majukumu mengine muhimu zaidi kwani ANASTAHILI na ana UWEZO. Udhaifu mwingine wa kibinaadamu HAUKWEPEKI
 
Kila la heri Mtoto Raia Mwema, nakuombea ukue ukomae haraka kwani uwezo huo unao kutokana na waandishi husika.
Lakini isuje tokea umekomaa wakatokea kina RA wengine wakakununua kwa bei ya juu kwa ajili ya maslahi yao 2010.
 
Halisi nashukuru kwani nilipata correction hiyo late last night too.. ni kweli Mhariri Mtendaji ni John Bwire. Mtanzania, ondoa shaka we are professionals na tunajua maadili ya uandishi wa habari. Ni kweli tuna misimamo tofauti lakini utii wetu wa kwanza kama raia ni kwa Tanzania na Tanzania peke yake!!
 
Akina RA waliweza kulinunua RAI baada ya kumtia jambajmaba na kumsukasuka Generali Ulimwengu kwamba si rai kwa vile aliwa lia deep kwa hoja zake nzito zenye ushahidi wazi.

This time sidhani kama mtu kama RA ataweza kulinunua Raia Mwema hasa ukizingatia hali halisi ya kisiasa Tanzania

Kijiko chaitwa kijiko na Chepeo haliitwi kijiko kikubwa.

Mimi binafsi niko nyuma ya waheshimiwa hawa hata kabla sijaanza kusoma watarajiacho kukiandika.

Mungu Ibariki Tanzania na Watanzania.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom