Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Klabu ya Yanga kupitia Msemaji wake Dismass Ten imefunguka na kuomba msaada kwa wadau mbalimbali wa soka nchini kuwasaidia vifusi vya mchanga ili waweze kurekebisha kiwanja chao cha Kaunda kilichopo Jangwani, Dar es salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari leo kwenye makao makuu ya Klabu hiyo Dismass amesema kulingana na ukubwa wa uwanja huo wanahitaji watu ambao wataweza kujitolea ili waweze kukamilisha zoezi la ujenzi.
"Taratibu za awali zimeanza kufanyika za ujenzi wa uwanja wetu wa mpira hapa Kaunda kwa sababu tunahitaji sehemu nzuri na tulivu ya kufanyia mazoezi. Kwa hivyo ambao watapata nafasi ya kupita Makao Makuu ya Klabu Jangwani, wataona vifusi vya mchanga vikimwaga", amesema Dismass
Aidha, Dismass amesema Wanakarabati uwanja huo kwa maelekezo mazuri kutoka kwa wataalamu wa ujenzi ili timu yao iweze kupata sehemu ya kufanyia mazoezi.
"Bado tunahitaji kifusi kwa ajili ya ujenzi huu kwa sababu eneo ni kubwa, wale wote ambao wanaweza kutusaidia kwenye eneo hili tunawakaribisha kutokana Wanayanga wanahitaji kujenga Yanga yao, kwa maana timu iweze kupata sehemu maalumu ya kufanyia mazoezi. Pia niwashukuru wale ambao wameshaanza kutusaidia katika hili kwa namna moja ama nyingine", amesisitiza Dismass.
Klabu ya Yanga inatarajia kushuka dimbani kesho kuwavaa Mtibwa Sugar katika michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara huku ikimkosa mchezaji wake wa Kimataifa, kiungo Tshishimbi Kabamba anayetumikia adhabu ya kukosa mechi moja baada ya kupata kadi 3 za njano katika mechi 3 zilizopita.
Akizungumza na waandishi wa habari leo kwenye makao makuu ya Klabu hiyo Dismass amesema kulingana na ukubwa wa uwanja huo wanahitaji watu ambao wataweza kujitolea ili waweze kukamilisha zoezi la ujenzi.
"Taratibu za awali zimeanza kufanyika za ujenzi wa uwanja wetu wa mpira hapa Kaunda kwa sababu tunahitaji sehemu nzuri na tulivu ya kufanyia mazoezi. Kwa hivyo ambao watapata nafasi ya kupita Makao Makuu ya Klabu Jangwani, wataona vifusi vya mchanga vikimwaga", amesema Dismass
Aidha, Dismass amesema Wanakarabati uwanja huo kwa maelekezo mazuri kutoka kwa wataalamu wa ujenzi ili timu yao iweze kupata sehemu ya kufanyia mazoezi.
"Bado tunahitaji kifusi kwa ajili ya ujenzi huu kwa sababu eneo ni kubwa, wale wote ambao wanaweza kutusaidia kwenye eneo hili tunawakaribisha kutokana Wanayanga wanahitaji kujenga Yanga yao, kwa maana timu iweze kupata sehemu maalumu ya kufanyia mazoezi. Pia niwashukuru wale ambao wameshaanza kutusaidia katika hili kwa namna moja ama nyingine", amesisitiza Dismass.
Klabu ya Yanga inatarajia kushuka dimbani kesho kuwavaa Mtibwa Sugar katika michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara huku ikimkosa mchezaji wake wa Kimataifa, kiungo Tshishimbi Kabamba anayetumikia adhabu ya kukosa mechi moja baada ya kupata kadi 3 za njano katika mechi 3 zilizopita.