Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Simba SC, Wekundu wa Msimbazi kutoka Jiji la Dar es salaam, leo Julai 10, 2022 wametangaza kukamilisha usajili wa kiungo wa dimba la katikati Mnigeria Victor Akpan (24) kwa mkataba wa miaka miwili akitokea klabu ya Coastal Union ya Tanga.
Kiungo huyu wa dimba la katikati (Defensore Centrale) amefanya makubwa sana akiwa na Wagosi wa Kaya kwenye Ligi Kuu msimu wa 2021/2022, akiwa amefunga na kutengeneza mabao pamoja na kuzuia.
"Kiungo wa katikati ya dimba mwenye uwezo mkubwa wa kuhimili mechi za aina zote, Victor Akpan ni Mnyama". Imeeleza kwa ufupi taarifa kutoka Simba SC.
Kiungo huyu wa dimba la katikati (Defensore Centrale) amefanya makubwa sana akiwa na Wagosi wa Kaya kwenye Ligi Kuu msimu wa 2021/2022, akiwa amefunga na kutengeneza mabao pamoja na kuzuia.
"Kiungo wa katikati ya dimba mwenye uwezo mkubwa wa kuhimili mechi za aina zote, Victor Akpan ni Mnyama". Imeeleza kwa ufupi taarifa kutoka Simba SC.