Simba Sports Club yamtambulisha Djuma Masoud kuwa kocha mpya msaidizi

Kunguru Mjanja

JF-Expert Member
Aug 22, 2012
2,036
3,929
mrithi mayanja.jpg


Mrithi wa aliyekuwa kocha msaidizi wa Simba, Jackson Mayanja anatarajiwa kutua leo jijini Dar es Salaam.

Djuma Masudi ndiye anayekuja kuchukua nafasi yake na huenda akaiwahi mechi dhidi ya Yanga Oktoba 28 kwenye Uwanja wa Taifa.

Kama humfahamu Djuma enzi zake za uchezaji alikuwa straika wa Inter FC ya Ligi Kuu ya Burundi. Ni kocha kijana mwenye mizuka na uwezo mkubwa wa kupandisha morali ya wachezaji kama alivyo Jamhuri Kihwelu 'Julio' au Ettiene Ndayiragige wa Mbao FC.

Kwa mujibu wa wachambuzi wa soka la Rwanda, Djuma ni kocha mwenye maneno mengi na rafiki wa wachezaji na inapotokea timu imeshinda hupandisha wazimu kama kocha wa Chelsea, Antonio Kante.

Kocha huyo ameipa Rayon Sports ya Rwanda ubingwa msimu uliopita kabla ya kuachia ngazi. Mafanikio yake katika Ligi ya Rwanda msimu uliopita yameivutia Simba na kuona ni mtu sahihi wa kumsaidia kocha wa sasa Joseph Omog.

Mmoja wa mabosi wa juu wa Simba aliliambia Mwanaspoti.com kuwa wamevutiwa na kocha huyo na tayari wamefanya naye mazungumzo ili aje kuziba nafasi ya Mayanja ambaye anaachana na timu hiyo baada ya kufanya kazi kwa miezi 22.

CHANZO: Mwananchi
=========================================================================================
UPDATES

Klabu ya Simba Sports Club ya jijini Dar es salaam leo imemtambulisha rasmi kocha mpya msaidizi Djuma Masoud, akichukua nafasi ya Jackson Mayanja ambaye amejiuzulu nafasi hiyo kutokana na matatizo ya kifamilia.

Msimu uliopita Djuma alikuwa kocha mkuu wa timu ya Rayon Sports ya Rwanda ambayo aliisaidia timu hiyo kutwaa ubingwa wa ligi kuu ambapo baadaye alichanguliwa kuwa kocha bora wa msimu 2016/2017.

Djuma amewahi kuvichezea vilabu vya APR, Rayon Sports, Prince Louis, Inter Star pamoja na timu ya Taifa ya Burundi Intambamurugamba.

 
2aef23b4fc00e217f3d0bd5563b3fdb4.jpg
Klabu ya Simba Sports Club ya jijini Dar es salaam leo imemtambulisha rasmi kocha mpya msaidizi Djuma Masoud, akichukua nafasi ya Jackson Mayanja ambaye amejiuzulu nafasi hiyo kutokana na matatizo ya kifamilia.

Msimu uliopita Djuma alikuwa kocha mkuu wa timu ya Rayon Sports ya Rwanda ambayo aliisaidia timu hiyo kutwaa ubingwa wa ligi kuu ambapo baadaye alichanguliwa kuwa kocha bora wa msimu 2016/2017.

Djuma amewahi kuvichezea vilabu vya APR, Rayon Sports, Prince Louis, Inter Star pamoja na timu ya Taifa ya Burundi Intambamurugamba.
 
Bi Hindu fc kwa sanaa hawajambo, jana kocha msaidizi kajiuzulu kwa matatizo ya kifamilia, leo kocha mpya anatambulishwa!
 
Eti klabu ya simba sports club! Ndio lugha gani hiyo? Mengine hayanihusu mi nipo na chama langu la jangwani tunawangoja Oktoba 28!
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Huyu jamaa alichukua ubingwa Rwanda. Leo kaja kuwa msaidizi matopeni.
Mrundi wa Mbao amekataa habari ya kuwa kocha msaidizi
 
Tanzania ina vituko sn,leo huyu anajiuzulu kesho mwingine anatamvulishwa ama kweli anayejua maana haambiwi maana
 
Back
Top Bottom