Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,261
Kocha huyo wa mabingwa watetezi wa Bundesliga, ametimuliwa ikiwa ni siku moja baada ya kufungwa mabao 3-0 na Paris St Germain (PSG) kwenye ligi ya mabingwa Ulaya Champions League.
"Ningependa kumshukuru Carlo Ancelotti kwa ushirikiano, Carlo ni rafiki yangu na ataendelea kuwa rafiki yangu lakini inabidi tufanye uamuzi kiueledi. Mechi yetu na Paris St Germain imeonyesha wazi kuwa tunapaswa kupima matokeo", amesema Karl-Heinz.
Ancelotti alijiunga na Bayern msimu uliopita na kuchukua ubingwa wa Bundesliga, lakini aliondolewa katika hatua ya robo fainali ya ligi ya mabingwa ya 2016/2017 na timu ya Real Madrid kutoka Hispania.