Ms Judith
JF-Expert Member
- Dec 24, 2010
- 2,563
- 918
Babu Loliondo ajengewa jengo la milioni 100
• Ni mchango wa KKKT, litamwezesha kutibu watu 700 kwa mpigo
na Mwandishi wetu
KATIKA kuboresha tiba ya maono ya Mchungaji Ambilikile Mwasapile ‘Babu' katika Kijiji cha Samunge, wilayani Ngorongoro, Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kaskazini Kati itajenga jengo la mviringo litakalohudumia watu 700 kwa wakati mmoja, litakalogharimu zaidi ya sh milioni 100.
Hatua hiyo ya kanisa imekuja wakati muafaka tangu kuanza kwa tiba hiyo miezi mitano iliyopita watu na wagonjwa walikuwa wakisimama katika jua kali na wakati wa mvua hususan hizi za masika wakisubiri kupata ‘kikombe cha Babu' katika adha kubwa.
Akizungumza na waandishi wa habari jana Arusha, Askofu Thomas Laizer, alisema jengo hilo litakuwa na vyumba vya kuchemshia dawa zitakazotolewa na Babu, chumba cha kuhifadhi dawa hizo, ambapo sehemu ya ukumbini kutakuwa na jukwaa la kutolea huduma hiyo katika mistari mitano ya watu 20, kila mstari kwenda kupokea dawa hiyo.
Alisema ujenzi wa jengo hilo utaanza hivi karibuni, ambapo eneo la ujenzi wake limeshapatikana karibu na anakotolea huduma mchungaji huyo aliyepata umaarufu wa aina yake kutokana na tiba hiyo, ambapo michoro ya jengo hilo inakaribia kumalizika.
"Sisi kama kanisa tumeona ni wakati muafaka wa kujenga jengo hilo kwa ajili ya kuhifadhi watu hao ambapo kwa muda wote tangu kuanza kwa tiba hiyo watu na wagonjwa wanaotoka maeneo mbalimbali nchini na nje ya nchi walikuwa wakisimama kusubiri tiba hiyo," alisema Askofu Laizer.
Sambamba na hatua hiyo, kanisa hilo limefungua akaunti maalumu katika Benki ya CRDB Na. 0150036432600, ambapo aliwaomba watu wenye mapenzi mema kuchangia huduma zinazotolewa na Mchungaji Mwasapile ili ziwe endelevu.
Katika hatua nyingine, Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Elias Wawa Lali, amesema kuwa foleni katika Kijiji cha Samunge imeanza kupungua kwa kiwango kikubwa na anao uhakika kwamba muda uliotolewa na mchungaji huyo utafikiwa.
Aidha, alikiri kuwa kulikuwepo na madereva wakorofi ambao walikuwa wakichakachua njia ya Longido hadi Ziwa Natron na kumfikia Babu kirahisi na kusema kuwa hiyo ilitokana na watu wa Longido kuchelewa kuweka kizuizi ambapo sasa hali hiyo imerekebishwa.
Wakati hayo yakiendelea, makusanyo ya sadaka inayotolewa na wagonjwa ya sh 500 wakati wakipatiwa kikombe na Babu yamefikia sh milioni 50 tangu kuanza kwa tiba hiyo mwishoni mwa mwaka jana ambapo kanisa katika mgawo wake utakaoingia moja kwa moja katika ujenzi ni sh milioni 20. Fedha nyingine zinabakia katika matumizi ya kawaidi na kidogo kwa ajili ya Babu.
source: Babu Loliondo ajengewa jengo la milioni 100
ngoma ikilia sana i-karibu na kupasuka, yetu macho,
lama injili imesitirika, basi imesitirika kwao wasioamini ambao mungu wa dunia hii amewapofusha nafsi zao isiwazukie nuru ya utukufu wake Kristo aliye sura ya Mungu
• Ni mchango wa KKKT, litamwezesha kutibu watu 700 kwa mpigo
na Mwandishi wetu
Hatua hiyo ya kanisa imekuja wakati muafaka tangu kuanza kwa tiba hiyo miezi mitano iliyopita watu na wagonjwa walikuwa wakisimama katika jua kali na wakati wa mvua hususan hizi za masika wakisubiri kupata ‘kikombe cha Babu' katika adha kubwa.
Akizungumza na waandishi wa habari jana Arusha, Askofu Thomas Laizer, alisema jengo hilo litakuwa na vyumba vya kuchemshia dawa zitakazotolewa na Babu, chumba cha kuhifadhi dawa hizo, ambapo sehemu ya ukumbini kutakuwa na jukwaa la kutolea huduma hiyo katika mistari mitano ya watu 20, kila mstari kwenda kupokea dawa hiyo.
Alisema ujenzi wa jengo hilo utaanza hivi karibuni, ambapo eneo la ujenzi wake limeshapatikana karibu na anakotolea huduma mchungaji huyo aliyepata umaarufu wa aina yake kutokana na tiba hiyo, ambapo michoro ya jengo hilo inakaribia kumalizika.
"Sisi kama kanisa tumeona ni wakati muafaka wa kujenga jengo hilo kwa ajili ya kuhifadhi watu hao ambapo kwa muda wote tangu kuanza kwa tiba hiyo watu na wagonjwa wanaotoka maeneo mbalimbali nchini na nje ya nchi walikuwa wakisimama kusubiri tiba hiyo," alisema Askofu Laizer.
Sambamba na hatua hiyo, kanisa hilo limefungua akaunti maalumu katika Benki ya CRDB Na. 0150036432600, ambapo aliwaomba watu wenye mapenzi mema kuchangia huduma zinazotolewa na Mchungaji Mwasapile ili ziwe endelevu.
Katika hatua nyingine, Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Elias Wawa Lali, amesema kuwa foleni katika Kijiji cha Samunge imeanza kupungua kwa kiwango kikubwa na anao uhakika kwamba muda uliotolewa na mchungaji huyo utafikiwa.
Aidha, alikiri kuwa kulikuwepo na madereva wakorofi ambao walikuwa wakichakachua njia ya Longido hadi Ziwa Natron na kumfikia Babu kirahisi na kusema kuwa hiyo ilitokana na watu wa Longido kuchelewa kuweka kizuizi ambapo sasa hali hiyo imerekebishwa.
Wakati hayo yakiendelea, makusanyo ya sadaka inayotolewa na wagonjwa ya sh 500 wakati wakipatiwa kikombe na Babu yamefikia sh milioni 50 tangu kuanza kwa tiba hiyo mwishoni mwa mwaka jana ambapo kanisa katika mgawo wake utakaoingia moja kwa moja katika ujenzi ni sh milioni 20. Fedha nyingine zinabakia katika matumizi ya kawaidi na kidogo kwa ajili ya Babu.
source: Babu Loliondo ajengewa jengo la milioni 100
ngoma ikilia sana i-karibu na kupasuka, yetu macho,
lama injili imesitirika, basi imesitirika kwao wasioamini ambao mungu wa dunia hii amewapofusha nafsi zao isiwazukie nuru ya utukufu wake Kristo aliye sura ya Mungu