KKKT Mbezi Beach msilazimishe waumini kuabudu kwa Kiingereza

Ibada ya kingereza kkt mbezi beach ni once a month, na ni option sio unalazimishwa, binafsi mimi na watoto wangu tunasali engkish service na first born wangu mafundisho ameopt english kwa sababu ndio lugha amekua akiitumia shule na tuliona kiswahili kitasumbua

Cha mshingi wewe chagua ibada unayoimudu, kama ni kiswagili au kingereza
Anasoma International School of Tanganyika?

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
 
Sababu ya kutumia lugha ya kingereza kwa watoto ni kwamba asilimia 98 ya watoto wa sunday school mbezi beach wanasoma shule za english medium au international school na walimu wanapata ugumu kuwafundisha kwa kiswahili

Na hata mafunzo ya kipaimara wameweka option ya english na kiswahili, mtoto anachagua anachoweza
Wanapataje Ugumu?kwamba mtoto akisoma International School au Englush medium hawezi zungumza Kiswahili fasaha?Wabongo sisi ni shida sana, Colonialism mentality inatuhangaisha sana

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
 
Wanajua kiswahili, binafsi wa kwangu anajua kiswahili lakini kinamsumbua, kumbuka shuleni since grade one anasoma masomo yote kwa.lugha ya kingereza, anapofika grade 3 ndio anaanza kusoma somo moja la kiswahili, unadhani hapo ni lugha gani atakua ameimaster sana kati ya english na kiswahili? Dunia imebadilika na maisha yamebadilika, ni lazima wazazi pia tujifunze kuadapt ulimwengu uliopo la sivyo watoto wetu watabaki nyuma
Dunia imebadilika kivipi?acha mindset za ajabu, Kenya wanaongea Kingereza tupu ila kuna watu wana maisha magumu sana hasana hata 100 mfukoni,

Dunia inahitaji vitu kama Networking, Exposure na kadhalika, mbona wachina wanatoka China na hasajui Lugha nyingine na wako Dunia nzima?

Wachina wako Msumbiji na aanapiga biashara ila hawajui Kireno na wanapiga pesa mbaya,

Anaye kudanganya Dunia inahita Kingerez ni nani?

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
 
Si bora hiyo kiingereza utaambulia,mimi ni RC kuna siku mwaka 2006 nilihudhuria ibada St Joseph kuna padre mzee kama Sijasahau jina ni Camilius,akapiga 'show'ya kilatini.Yani sikuambulia hata moja ilikuwa nafata wazee tu wakisimama ,wakipiga goti,wakikaa.
 
Hao wa kuongea kiingereza mbona walishafunga makanisa siku mingi, au wakija bongo ndo wanapata mzuka wa kwenda church..
 
Hahahaa hii ibada ipo Azania front na mimi ni mmoja wapo nasali hapo ila kuna mchungaji wetu alihamishiwa huko kutoka huku nafikiri labda ndiye aliyeenda kupeleka huko huu utaratibu. Kusudi kuu la hii ibada ni kuwapa nafasi waumini wa kigeni kushiriki ibada.

Kwa mf. waumini wengi wa Azania front ni wakazi wa Upanga, Oyster Bay, Masaki na Kinondoni maeneo haya kwa sehemu kubwa pia hukaliwa na wageni sana ambao kiswahili sio lugha wanayoimudu nahisi pia labda hata huko Mbezi walifanya ombi la kuwekwa hiyo ibada pia.
Wajifunze kiswahili sio wenyeji kuwekewa muda wao wa kuabudu ibada ya kizungu. Mbona mwanzo hizo ibada xilikua mchana kwa nini sasa wa cause 'incovinience' kwa wenyeji.
 
Ibada ya kingereza kkt mbezi beach ni once a month, na ni option sio unalazimishwa, binafsi mimi na watoto wangu tunasali engkish service na first born wangu mafundisho ameopt english kwa sababu ndio lugha amekua akiitumia shule na tuliona kiswahili kitasumbua

Cha mshingi wewe chagua ibada unayoimudu, kama ni kiswagili au kingereza
Bora ungesema watoto wanasali kingereza kwa lengo la kumudu lugha. Sasa wewe kasumbamtu unafikiri ukisali kwa kingereza ndio utasamehewa ufisadi na mungu? Msisumbue wenzenu kwa mindset zenu za kitumwa.
 
Wakati Taifa lina lengo la kuimarisha matumizi ya lugha yetu kwenye nyanja zote ikiwa ni pamoja na elimu wapinzani wa taifa kujikomboa kwenye ukoloni wa lugha na utamaduni wa kigeni wanajibu mapigo kupitia makanisa.

Kama muomini wa KKKT Mbezi Beach sioni mahitaji na ungezeko la ibada na mafunzo ya sunday school kwa Kiingereza.

Ilianza kidogo kwa misa chache sasa kila Jumapili na kwa sikukuu ya chrismas na mwaka mpya. Naona kuna wazee wa usharika wamejaa kasumba ya Kiulaya, binafsi sipendelei jambo hili.

Nina hakika mahitaji ya misa kwa Kiingereza ni madogo sana au hakuna kwa hiyo viongozi wasitulazishe kukosa misa ya pili saa 4.00 asubuhi kwa Kiswahili eti inageuzwa ya Kiingereza.
Ingekua jambo la maana kanisa kuanzisha darasa la lugha ya kiswahili kwa hao waomini wachache badala ya kuwawekea ibada muda muafaka kwa waomini wengi.

Kama ndio usomi mwenyewe ni msomi ngazi ya uzamili ila sipendi kulimbukia utamaduni wa watu wengine.
Hiyo Krisimasi ya lini? Kama ya mwaka juu mbona wewe na mimi tulihudhuria ilikuwa ya kizaramo! Unatatizo la kusahau.
 
Bwashee sali misa ya kwanza.

Binafsi naona wamechelewa sana kuanzisha hii misa ya kiinglishi.

Kanisani kwetu pale Anglican St Alban Huduma kwa lugha ya malkia ina zaidi ya miaka 100 sasa.........Ni misa ya pili.

Ya kwanza na ya tatu ni za kiswahili!
Bado mnaendeleza ushoga?
 
Wakati Taifa lina lengo la kuimarisha matumizi ya lugha yetu kwenye nyanja zote ikiwa ni pamoja na elimu wapinzani wa taifa kujikomboa kwenye ukoloni wa lugha na utamaduni wa kigeni wanajibu mapigo kupitia makanisa.

Kama muomini wa KKKT Mbezi Beach sioni mahitaji na ungezeko la ibada na mafunzo ya sunday school kwa Kiingereza.

Ilianza kidogo kwa misa chache sasa kila Jumapili na kwa sikukuu ya chrismas na mwaka mpya. Naona kuna wazee wa usharika wamejaa kasumba ya Kiulaya, binafsi sipendelei jambo hili.

Nina hakika mahitaji ya misa kwa Kiingereza ni madogo sana au hakuna kwa hiyo viongozi wasitulazishe kukosa misa ya pili saa 4.00 asubuhi kwa Kiswahili eti inageuzwa ya Kiingereza.
Ingekua jambo la maana kanisa kuanzisha darasa la lugha ya kiswahili kwa hao waomini wachache badala ya kuwawekea ibada muda muafaka kwa waomini wengi.

Kama ndio usomi mwenyewe ni msomi ngazi ya uzamili ila sipendi kulimbukia utamaduni wa watu wengine.
Kuna misa ngapi?
 
Nadhani mleta uzi sio muumini wa Mbezi beach. Pale kuna misa tatu. Ya sa moja na sa nne ni kiswahili. Ya sa nane mchana ni kiingereza. Pia Sunday school kuna option ya kiswahili na kiingereza. Unachagua unapopamudu
 
mkuu, ungetumia busara sana kulisema hili kwenye jumuiya yako, then wazee wa kanisa wakalichukua kama muhtasari na kuliwakilisha kwenye vikao vya baraza, ujumbe wako ungefika na kujadiliwa kwa kina.....sipingani wa kukubaliana na wewe.....mahali sahihi pa kuanzishia hii hoja yako papo......elewa na hasa kipindi hiki cha xmas...... uchagani (Mlimani - kwa wale tunaoenda kuabudu huko) misa ya pili mara nyingi huendeshwa ki-Chagga.........una haki ya kuchagua ibada kwa lugha yako pendwa.....
 
Bora ungesema watoto wanasali kingereza kwa lengo la kumudu lugha. Sasa wewe kasumbamtu unafikiri ukisali kwa kingereza ndio utasamehewa ufisadi na mungu? Msisumbue wenzenu kwa mindset zenu za kitumwa.
Pole sana mkuu, kila mtu ana uhuru wa kuchagua kilicho ndani ya uwezo wake wether ni utumwa au sio, hata hizi smart phone tunazotumia pia ni utumwa maana ni za wakoloni, hebubtuanze kutengeneza vya kwetu kwanza ndio tukatae vya mabeberu la sivyo mtabaki kuwalaumu mebeberu wakati lugha yao ndio inatawala dunia
 
Dunia imebadilika kivipi?acha mindset za ajabu, Kenya wanaongea Kingereza tupu ila kuna watu wana maisha magumu sana hasana hata 100 mfukoni,

Dunia inahitaji vitu kama Networking, Exposure na kadhalika, mbona wachina wanatoka China na hasajui Lugha nyingine na wako Dunia nzima?

Wachina wako Msumbiji na aanapiga biashara ila hawajui Kireno na wanapiga pesa mbaya,

Anaye kudanganya Dunia inahita Kingerez ni nani?

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
You have a point mkuu, lakini kwa uchumi wetu huu ambao 60% ya bajeti tunategemea matafifa makubwa ni ngumu kupenya kwenye uchumi wa dunia, lugha yetu ni maarufu tu hapa east africa na hata sio africa nzima, imagine mchina yeye anajitegemea 100% kwenye bajeti yake na elimu yao ni huru na pia soko la dunia linamtegemea mchina kwa asilimia kubwa tu, sio sahihi kujilinganisha na mchina

Kwa sasa, english ni lugha ya dunia, imagine sisi tukapiga marufuku hiyo lugha tukaanza kuzoma kiswahili tu, hivi tunapambana vipi na soko la ajira na uchumi duniani

Hata nafasi za kazi tu hapa bongo, hata za serikali zinataka fluent english speaker, hapa unajiteteaje mkuu?
 
Wanapataje Ugumu?kwamba mtoto akisoma International School au Englush medium hawezi zungumza Kiswahili fasaha?Wabongo sisi ni shida sana, Colonialism mentality inatuhangaisha sana

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
Imagine mtoto ameanza shule akiwa na miaka miwili, lugha anayoitumia shuleni ni kingereza tu anashinda shuleni masaa 8 mpaka tisa, mpaka anafika miaka 9 unadhani kiswahili atakua anakijua au anababaisha tu?

Ni sawa na mtoto ambae amezaliwa kwenye jamii wanayoongea lugha ya kikabila, niliwahi kwenda shinyanga, nilikutana na mtoto wa miaka mitano hajui hata neno moja ala kiswahili nilishangaa sana, wenyeji wakaniambia jamii yao wanawasiliana kwa kisukuma tu ndio maana unapoongea kiswahili lazima uwe na mti anawatafsiria wenyeji kwa kisukuma
 
Back
Top Bottom