mitale na midimu
JF-Expert Member
- Aug 26, 2015
- 10,420
- 17,701
Kifo fumbo ambalo ni kutokuwa na majibu ya haraka sahihi na kwa sababu hawa jamaa hawarudi na hata kama wakirudi hatuwaamini.
1:Wahindu (hinduism)
Hakuna cha mbingu wala jehanam, Mtu akifa anarudi kwenye maisha haya kama kitu au kiumbe kingine.
2:Uislam
Quran 45:26. Sema: Mwenyezi Mungu anakuhuisheni, kisha anakufisheni, kisha anakukusanyeni Siku ya Kiyama isiyo na shaka. Lakini watu wengi hawajui.
hapa inaonekena Hata ufeje, mwili utakusanywa na kutakiwa kusimama mbele ya hukumu. wataalam wanaweza kutupa maarifa zaidi.
3:Wabudha
Hawa wanaamini Ukifa mwili utaoza lkn akili/mind itaendelea kuwepo. Na pia kuna kuzaliwa upya baada ya kifo.
4:Wayahudi/Judaism
Nafsi inaishi milele, mwili ni kama kasha ambalo limeazimwa roho likifa linaoza roho inaendelea kula maisha.pamoja na hili wanamaelezo ya ziada.
5:Wakristo
Hapa wamegawanyika makundi mawili.
wale wanaoamini Mtu akifa roho yake haifi, inaenda kula raha mbinguni, au kama ni ovu inateswa motoni. Pia wapo wanaoamini na mimi nikiwemo mtu akifa ni kaubirini analala usingizi mzuri wa mauti kusubiri hukumu ya haki siku ya kiyama. haendi popote.
6:Mababu zetu na Wababe wakiafrika wanasemaje.
Kifo sio mwisho wa maisha, bali ni mwendelezo wa maisha kwa mfumo tofauti ambao hauna mwili. Kwa baadhi ya mila Kifo ni sherehe maana jamaa anakuwa amehamishiwa katika maisha mengine ambayo ni bora zaidi.
8:Wanasayansi na wasiamini Mungu na Miungu
Hapa nao wanamaoni mengi, ila athiest na mwanasayansi nguli aliyefariki majuzi Stephen Hawking anasema Ubongo ni kama Kompyuta kuna wakati Unachoka unaacha kufanya kazi na kufa. Hakuna chochote mtu akifa, zaidi hakuna cha mbingu wala kiyama wala moto. Hizo ni hadithi za watu Wanaoogopa giza.
vipi wewe unaamini lipi.
1:Wahindu (hinduism)
Hakuna cha mbingu wala jehanam, Mtu akifa anarudi kwenye maisha haya kama kitu au kiumbe kingine.
2:Uislam
Quran 45:26. Sema: Mwenyezi Mungu anakuhuisheni, kisha anakufisheni, kisha anakukusanyeni Siku ya Kiyama isiyo na shaka. Lakini watu wengi hawajui.
hapa inaonekena Hata ufeje, mwili utakusanywa na kutakiwa kusimama mbele ya hukumu. wataalam wanaweza kutupa maarifa zaidi.
3:Wabudha
Hawa wanaamini Ukifa mwili utaoza lkn akili/mind itaendelea kuwepo. Na pia kuna kuzaliwa upya baada ya kifo.
4:Wayahudi/Judaism
Nafsi inaishi milele, mwili ni kama kasha ambalo limeazimwa roho likifa linaoza roho inaendelea kula maisha.pamoja na hili wanamaelezo ya ziada.
5:Wakristo
Hapa wamegawanyika makundi mawili.
wale wanaoamini Mtu akifa roho yake haifi, inaenda kula raha mbinguni, au kama ni ovu inateswa motoni. Pia wapo wanaoamini na mimi nikiwemo mtu akifa ni kaubirini analala usingizi mzuri wa mauti kusubiri hukumu ya haki siku ya kiyama. haendi popote.
6:Mababu zetu na Wababe wakiafrika wanasemaje.
Kifo sio mwisho wa maisha, bali ni mwendelezo wa maisha kwa mfumo tofauti ambao hauna mwili. Kwa baadhi ya mila Kifo ni sherehe maana jamaa anakuwa amehamishiwa katika maisha mengine ambayo ni bora zaidi.
8:Wanasayansi na wasiamini Mungu na Miungu
Hapa nao wanamaoni mengi, ila athiest na mwanasayansi nguli aliyefariki majuzi Stephen Hawking anasema Ubongo ni kama Kompyuta kuna wakati Unachoka unaacha kufanya kazi na kufa. Hakuna chochote mtu akifa, zaidi hakuna cha mbingu wala kiyama wala moto. Hizo ni hadithi za watu Wanaoogopa giza.
vipi wewe unaamini lipi.