Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,722
- 21,778
Kizimbani kwa kujifanya wake wa Waziri wa Elimu
Saturday, April 18, 2009 10:06 AM
WANAWAKE wawili wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala kwa kosa la udanganyifu kwa kujifanya ni wake wa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Prof. Jumanne Maghembe
Washitakiwa hao ni Hanifa Kassim Kawambwa [30] mkazi wa Temeke Mikoroshini na Hawa Aladita Sharif [30] mkazi wa Mbagala Chemchem.
Wanawake hao walifikishwa Mahakamani hapo jana kujibu mashitaka yanayowakabili wa kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.
Walisomewa mashitaka yao na Mwendesha Mashitaka Inspekta Msaidizi wa Polisi Denis Mujumba mbele ya Hakimu Janeth Kinyage wa Mahakama hiyo.
Mujumba alidai kuwa katika shitaka la kwanza, washitakiwa wote kwa pamoja mapema mwaka huu, walikula njama ya kujipatia kiasi cha shilingi 6,600,000 kutoka kwa Kiramuu Petro Mbowe.
Katika shitaka la pili imedaiwa kuwa Machi 27, mwaka huu, katika Benki ya Access iliyopo Temeke washitakiwa hao walijipatia Sh. 3,000,000 kutoka kwa Kiramuu Petro Mbowe kupitia akaunti iliyokuwa na namba 0221100609319.
Washitakiwa hao waliweza kujipatia fedha hizo baada ya kujitambulisha kuwa wao ni wake wa Waziri wa Elimu wa Tanzania Prof. Maghembe.
Washitakiwa walikana mashitaka hayo na kudai kuwa si kweli na waliweza kuwa nje kwa dhamana,.
Hivyo kesi hiyo iliahirishwa hadi hapo Mei 21, mwaka huu, itakapotajwa tena Mahakamani hapo.
Na Chondoma Shabani, Dar es salaam
Mtumie Rafiki Yako
Saturday, April 18, 2009 10:06 AM
WANAWAKE wawili wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala kwa kosa la udanganyifu kwa kujifanya ni wake wa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Prof. Jumanne Maghembe
Washitakiwa hao ni Hanifa Kassim Kawambwa [30] mkazi wa Temeke Mikoroshini na Hawa Aladita Sharif [30] mkazi wa Mbagala Chemchem.
Wanawake hao walifikishwa Mahakamani hapo jana kujibu mashitaka yanayowakabili wa kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.
Walisomewa mashitaka yao na Mwendesha Mashitaka Inspekta Msaidizi wa Polisi Denis Mujumba mbele ya Hakimu Janeth Kinyage wa Mahakama hiyo.
Mujumba alidai kuwa katika shitaka la kwanza, washitakiwa wote kwa pamoja mapema mwaka huu, walikula njama ya kujipatia kiasi cha shilingi 6,600,000 kutoka kwa Kiramuu Petro Mbowe.
Katika shitaka la pili imedaiwa kuwa Machi 27, mwaka huu, katika Benki ya Access iliyopo Temeke washitakiwa hao walijipatia Sh. 3,000,000 kutoka kwa Kiramuu Petro Mbowe kupitia akaunti iliyokuwa na namba 0221100609319.
Washitakiwa hao waliweza kujipatia fedha hizo baada ya kujitambulisha kuwa wao ni wake wa Waziri wa Elimu wa Tanzania Prof. Maghembe.
Washitakiwa walikana mashitaka hayo na kudai kuwa si kweli na waliweza kuwa nje kwa dhamana,.
Hivyo kesi hiyo iliahirishwa hadi hapo Mei 21, mwaka huu, itakapotajwa tena Mahakamani hapo.
Na Chondoma Shabani, Dar es salaam
Mtumie Rafiki Yako