Kiwanja Wazi chavamiwa Bunju Beach chauza million 100, Watendaji wajichanganya

mgt software

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
13,767
7,115
Kukiwa kuna vuguvugu la kurudisha viwanja wazi vya mapumziko na MICHEZO , kiwanja cha wazi kwa ajili ya soko chauzwa kinyemela kwa mfanyabiashara, inasemekana kuna matapeli wapya wanatengeneza doc. wanashirikiana na watendaji wanauza viwanja wazi na sehemu zilizoachwa kwenye mabonde na makorongo,sehemu za mito, katika utafiti wetu tumegundua viwanja vitano , kuna vingine bado tunaendelea na utafiti, tuliitisha kikao cha wanabunju na kuunda umoja wa wanabunju tukiwa na maadhimio ya kulinda viwanja vyetu vya wazi pamoja na kuanzisha ulinzi shirikishi, katika vikao vyetu tulitoa dokezo la uvamizi wa viwanja na uamiaji holele wa wafanyabiashara ndogo ndogo kuvamia kiwanja cha shule, Mwenyekiti wa Mtaa tulikubaliana naye kuwaondoa, alifanya hivyo , ghafla ikaja barua ya kuwaambia wabaki ila wachimbe choo, tukarudisha wito kwa mtendaji , akawapa siku tatu waondoke wakaondoka, hapo ndipo sakata la kuvamia kiwanja kingine wazi na kujigawia, kila mtu alitoa tozo la laki moja kugawiwa eneo, jambo hili lilipingwa vikali maana hao vijana hawajulikani wanatoka wapi, pia vibanda ni sehemu ya maficho yao ya Ujambazi na wizi wa mifugo na majumbani.
Baada ya hapo tukamltafuta aliyevamia na kujenga , mlizi wake akatupa simu tukampigia tukiwa na mtendaji ili atuonyeshe doc. alionekana kubabaika na kuzima simu, tukaenda kwa m-pesa kupata jina kamili,alikana kuwa sio jina lake. Sasa ndio kwanza amemeliz aujenzi bado gate

chini ni picha za uvamizi
 

Attachments

  • plot iliyotapeliwa.JPG
    plot iliyotapeliwa.JPG
    161.6 KB · Views: 52
  • ukuta show room ya magari.JPG
    ukuta show room ya magari.JPG
    29.5 KB · Views: 60
  • miti ya tanesco miakamitatu.JPG
    miti ya tanesco miakamitatu.JPG
    27.2 KB · Views: 52
  • soko lililovamiwa.JPG
    soko lililovamiwa.JPG
    32.3 KB · Views: 48
hatujui maana anaikana jina lake, si unajua mambo ya m-pesa na tigo pesa, ikiwa mtu anakusumbua mtumia hela kama ka 1000.00 utapata jina lake kamili , mlizi anasema ni yeye , yeye akana jina ati!, habari hii ipo hata polisi wazo kwa OCD Mloto alishaenda na kujionea mambo, tunafatilia sana , wiki hii tutamuona mbunge wetu Mdee na Tibaijuka tupate ufafanuzi wa kubadilishiwa matumizi. Imekula kwake kwani Bunju Beach imejaa wasomi wasitafu na wafanyakazi mbali mbali .

Sorry picha ya nne ni uvamizi wamachinga na maficho ya vibaka.

picha ya tatu ni miti ya TANESCO iliyotelekezwa miaka mitatu huku waombaji wakiwa wamekata tamaa, Mladi huu noma hata maji hakuna huku serikali ilituuzia bei mbaya mwaka 2004 alafu wanasisitiza kupaendeleza kuwa makazi bora ya kuigwa. Je kwa staili hii itawezekana?
 
Back
Top Bottom