mgt software
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 13,767
- 7,115
Kukiwa kuna vuguvugu la kurudisha viwanja wazi vya mapumziko na MICHEZO , kiwanja cha wazi kwa ajili ya soko chauzwa kinyemela kwa mfanyabiashara, inasemekana kuna matapeli wapya wanatengeneza doc. wanashirikiana na watendaji wanauza viwanja wazi na sehemu zilizoachwa kwenye mabonde na makorongo,sehemu za mito, katika utafiti wetu tumegundua viwanja vitano , kuna vingine bado tunaendelea na utafiti, tuliitisha kikao cha wanabunju na kuunda umoja wa wanabunju tukiwa na maadhimio ya kulinda viwanja vyetu vya wazi pamoja na kuanzisha ulinzi shirikishi, katika vikao vyetu tulitoa dokezo la uvamizi wa viwanja na uamiaji holele wa wafanyabiashara ndogo ndogo kuvamia kiwanja cha shule, Mwenyekiti wa Mtaa tulikubaliana naye kuwaondoa, alifanya hivyo , ghafla ikaja barua ya kuwaambia wabaki ila wachimbe choo, tukarudisha wito kwa mtendaji , akawapa siku tatu waondoke wakaondoka, hapo ndipo sakata la kuvamia kiwanja kingine wazi na kujigawia, kila mtu alitoa tozo la laki moja kugawiwa eneo, jambo hili lilipingwa vikali maana hao vijana hawajulikani wanatoka wapi, pia vibanda ni sehemu ya maficho yao ya Ujambazi na wizi wa mifugo na majumbani.
Baada ya hapo tukamltafuta aliyevamia na kujenga , mlizi wake akatupa simu tukampigia tukiwa na mtendaji ili atuonyeshe doc. alionekana kubabaika na kuzima simu, tukaenda kwa m-pesa kupata jina kamili,alikana kuwa sio jina lake. Sasa ndio kwanza amemeliz aujenzi bado gate
chini ni picha za uvamizi
Baada ya hapo tukamltafuta aliyevamia na kujenga , mlizi wake akatupa simu tukampigia tukiwa na mtendaji ili atuonyeshe doc. alionekana kubabaika na kuzima simu, tukaenda kwa m-pesa kupata jina kamili,alikana kuwa sio jina lake. Sasa ndio kwanza amemeliz aujenzi bado gate
chini ni picha za uvamizi