Wapendwa Watanzania, hivi karibuni kimefunguliwa kiwanda cha kutengeneza spiriti katika eneo la Kifaru,Mwanga Kilimanjaro.Kwa wanaopita na mabasi kutoka Dar kwenda Arusha nadhani mnakumbuka harufu kali inayotoka kiwandani hapo. Mojawapo ya nishati wanayotumia kwenye ma boiler yao ni magogo mabichi! Wananunua kwa bei nzuri sana ili mradi magogo hayo yawe mabichi na hasa yale yanayotoa utomvu! Hivi sasa wafanyabiashara wenye malori maeneo mbalimbali mkoani hapa hasa wilayani Rombo na Moshi Vijijini wanaouzunguka Mlima wanasaka magogo mabichi kwa hali na mali na kwenda kuyauza kiwandani hapo!