Mgoyangi
Senior Member
- Feb 6, 2008
- 184
- 9
Ni zaidi ya Miezi 10 sasa hakuna kinachofanyika katika kiwanda cha Nyama tangu apatikane mwekezaji, kupitia ubia wa mwekezaji huyo na Mbunge wa Meatu, Salum Khamis, maarufu kama Salum Mbuzi miongoni mwa wapiga kura wake.
Wafanyakazi waliorithiwa kutoka Tanganyika Parkers, mmiliki wa awali wa kiwanda hicho kupitia mfilisi, sasa wanapiga miayo kwa kuwa hakuna wanacholipwa na wanadai heri enzi hizo kuliko kuwa chini ya mwekezaji huyu.
Kiwanda kina balaa, sababu hakijawahi kufanya kazi tangu kianze kujengwa miaka ya sabini mwishoni, kisa ufisadi, kwani, Mkandarasi alizidiwa kete, badala ya kuagiza yeye vifaa kama mkataba unavyodai, maafisa wa serikali waliagiza wao na kula cha juu, mkandarasi akachukia na kuamua kuondoka kabla ya kukamilisha ujenzi.
Tangu wakati huo kiwanda kikawa hifadhi ya popo na nyoka, baadaye amekuja anayedaiwa kuwa mwekezaji ambaye hajafanya kazi yoyote hadi leo, na mambo yamekuwa mabaya zaidi, pengine kutokana na kukatwa mirija, ya kufyonza pesa kwa kisingizio cha uwekzaji, maana hata huyo mwekezaji ni mbongo mburushi kama alivyo partner wake Salum Mbuzi.
Kilichokuwa kimetegwa hapa ni deal, sasa siyo wakati wake watanzania wameamka, na katika hili hakuna tena kinachoendelea. RIP Kiwanda cha Nyama Shinyanga.
Wafanyakazi waliorithiwa kutoka Tanganyika Parkers, mmiliki wa awali wa kiwanda hicho kupitia mfilisi, sasa wanapiga miayo kwa kuwa hakuna wanacholipwa na wanadai heri enzi hizo kuliko kuwa chini ya mwekezaji huyu.
Kiwanda kina balaa, sababu hakijawahi kufanya kazi tangu kianze kujengwa miaka ya sabini mwishoni, kisa ufisadi, kwani, Mkandarasi alizidiwa kete, badala ya kuagiza yeye vifaa kama mkataba unavyodai, maafisa wa serikali waliagiza wao na kula cha juu, mkandarasi akachukia na kuamua kuondoka kabla ya kukamilisha ujenzi.
Tangu wakati huo kiwanda kikawa hifadhi ya popo na nyoka, baadaye amekuja anayedaiwa kuwa mwekezaji ambaye hajafanya kazi yoyote hadi leo, na mambo yamekuwa mabaya zaidi, pengine kutokana na kukatwa mirija, ya kufyonza pesa kwa kisingizio cha uwekzaji, maana hata huyo mwekezaji ni mbongo mburushi kama alivyo partner wake Salum Mbuzi.
Kilichokuwa kimetegwa hapa ni deal, sasa siyo wakati wake watanzania wameamka, na katika hili hakuna tena kinachoendelea. RIP Kiwanda cha Nyama Shinyanga.