Kivuli cha dude kubwa cha kutisha kinanisumbua usiku

Me najiuliza sitting room usiku wa manane taa zikiwa zimezimwa huwa unafanya nini. Hilo moja.
Pili mirungi inatoa usingizi kama unapiga muda mrefu na Pia una stress inaweza kuwa chanzo cha hiyo hallucination
Sitting room na dining zmeshikana
Sasa huwa napenda kunywa chai usiku.
Mara zote kivuli kimenitokea nikienda kuchukua chai au maji kwenye friji
 
Huyu tatizo lake ni usingizi hajalala muda mrefu kwa sababu ya andasi ya mrungi huko unako taka aende ndiyo utampoteza zaidi maana atakutana na wajanja watazidi kumtia uwoga ili wapige pesa!!
Usingiz wa usiku tu sijaupata mda mrefu ila kama kulala nalala mchana.
Huko mm siwez kwenda ndugu yng nikapate dhambi ya shirk
 
hakuna cha malaika wala jini, huo ni uoga tu. hiyo itakuwa mbalamwezi au taa, na ikimulika kitu flan inaleta kivuli, ss uoga wako ww ndo unaona vtu vya ajabu.

acha kiwaza kulogwa tu, utalogwa kweli
Sijasema malaika wala jini, nimeuliza hichi kivuli ni cha nini
Sasa inakuwaje mama na ndugu wameshindwa wakati huku mm nikiwa nakiona.
Siogopi kulogwa wala sijawah kuwaza kama nimelogwa
 
"huwa nakiona nikiwa macho yanaangalia pembeni nikigeuka nikiface kinapotea"


Pole sana...

Itakua kope zinenasa ndani ya jicho, mwambie mtu afanye kama anakupulizia kwenye jicho ili zitoke...


Cc: mahondaw
 
Nadhani hiyo ni delusion of persecution, huwa inatokea sana kwa watu wenye schizophrenia au magonjwa mbalimbali ya akili!
 
Naungana na mshana jr kuwa; Usitake asilan kujua kinataka nini kwako. Huko ni kushauriana nacho kitu ambacho ni kibaya zaidi. Pili, usiende hospital kwani wataishia kukuchoma masindano ya vichaa.
Nenda maombi mazito ya kulikemea hilo pepo. Omba ka kichaa hadi Mungu akusikie akuokoe na hilo jinamizi. Sio malaika kama wanavyokuambia wengine bali ni pepo baya. Hapo, Damu ya Yesu tu ndo dawa yako mengine ni kupoteza muda na mauti kukujilia ghafula
 
Hizo ni imani potovu
Naungana na mshana jr kuwa; Usitake asilan kujua kinataka nini kwako. Huko ni kushauriana nacho kitu ambacho ni kibaya zaidi. Pili, usiende hospital kwani wataishia kukuchoma masindano ya vichaa.
Nenda maombi mazito ya kulikemea hilo pepo. Omba ka kichaa hadi Mungu akusikie akuokoe na hilo jinamizi. Sio malaika kama wanavyokuambia wengine bali ni pepo baya. Hapo, Damu ya Yesu tu ndo dawa yako mengine ni kupoteza muda na mauti kukujilia ghafula
 
Mm naona kama ishara mbaya maana kabla hakijaja kichwa kinauma halaf macho kama yanacheza halaf ndo naanza kukiona
Kingine kinatisha sema mm sio mwoga kivile tofaut na angekiona mtu mwingine
Dawa yake hii: ukiona kivuli hicho ita kutoka moyoni: YESU KRISTO! Mwombe afukuze nguvu za giza katika maisha yako, utaniambia natokeo.
 
Assalamoualaikom. Simamisha sala 5 na kuzidisha ibada. Jitahidi sn na ibada za usiku, kufunga na kutoa sadaka na bila kusahau kusoma Quran kwa wingi. Jitahidi kuudumisha udhu wako na jitahidi kuchukua udhu kabla ya kulala. Pia kithirisha kumsabihi Allah na kumuomba maghfira. Kwa kufanya hivi utakuwa umemcha Allah na utakuwa kipenzi chake, Naye atakulinda dhidi ya vitimbi vya majini na mashetani (almuhimu usithubutu kwenda kwa waganga)
Vinginevyo, ukisikiliza baadhi ya ushauri huku kuhusu chumvi... Sijui kuoga baharini nk utaingia ktk shirki. Matatizo uliyopata ni mtihani ktk mitihani ya Allah so zidisha kumcha Allah naye atakusaidia. Kila limfikalo mwanadamu ni kwa kadar yake Allah. Wengine wanapata mitihani ya maradhi, wengine umasikini, ufukara, ugumba, mke/mume, watoto, kazi nk. Mtihani wako wewe ni wa shetani. Jisaidie kwa subra na swala. Allah akuondolee mtihani huu. Aamiyn
 

Similar Discussions

7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom