Kivuli cha dude kubwa cha kutisha kinanisumbua usiku

Makavengaaa

Member
Mar 6, 2019
41
56
Habari zenu wadau wote wa JF,

Nimepata tatizo ambalo silielewi, kwa muda mrefu nimekuwa nikiona kivuli cha mtu cheusi nikigeuka kinapotea ila hiyo hali haikunipa shida nilidharau halafu ilikuwaga ni home tu, Ila sasa hivi hata nikiwa kwengine.

Sasa kuna kivuli hicho kimenijia kwa mara ya tatu sasa hicho hakipotei kinakaa na huwa kwenye kuta za sitting room taa zikiwa zimezimwa usiku wa manane.

Leo hii ni mara ya tatu, huwa nakiona nikiwa macho yanaangalia pembeni nikigeuka nikiface kinapotea sasa leo nimemwita mama nikamwambia kile kivuli nachokwambia kiko ukutani vipi unakiona huku mimi nikiwa naangalia pembeni lakini nakiona mama akaniambia haoni kitu.

Sasa ndugu zangu wa JF mnisaidie hiki ni kitu gani maana nikiwaambiwa watu wengine wananiona kama nina wasiwasi au nimechanganyikiwa.

Kivuli chenyewe ni dude kubwa hivi halafu naona mkono wenye kucha ndefu ni cheusi.

Hii hali imenishangaza sana, mama ananiambiwa tunakuitia shehe akusomee.

Ila nimebaki na maswali, hiki kivuli kinataka nn kwangu kama kuna wadau wanafaham hali hii wanielezee.

Sitanii ndugu zangu nahitaji mawazo yenu
 
Huenda yakawa ni maluelue tu na wengine huona mpk mtu na huanza kukimbia aidha nawe itajakufikia hatua hii..!! Hapo ndo utajua kwanini kuna madaktari wa psychology.
 
Kuna mawili, huyo ni jini au malaika anayekulinda maana kila binadam ana malaika wake pembeni yake anayemlinda, ila hebu angalia hicho kivuli kinaonyesha ishara gani nzuri au mbaya
 
Waswahili huwa na usemi wao
unaosema CHA MTU MAVI UKIKIONA
KITEME sasa bwana nikushauri jambo moja kama umewahi kuchukua kitu au mali ya mtu iwe kwa bahati mbaya au kwa makusudi fanya kurejesha hiyo mali au hicho kitu kwa mwenye nacho, hilo tatizo lako litakwisha kabisa...!!!!
 
Hospital nawaambia vp, wasije wakanichoma shindano za wagonjwa wa akili
Signs za schizophrenia nenda hospital. Kadiri muda unavyozidi kwenda kitaanza kukutisha. Na unaweza kuwa violant. Ni vema uende hospital upate tiba mapema
 
Kuna mawili, huyo ni jini au malaika anayekulinda maana kila binadam ana malaika wake pembeni yake anayemlinda, ila hebu angalia hicho kivuli kinaonyesha ishara gani nzuri au mbaya
Mm naona kama ishara mbaya maana kabla hakijaja kichwa kinauma halaf macho kama yanacheza halaf ndo naanza kukiona
Kingine kinatisha sema mm sio mwoga kivile tofaut na angekiona mtu mwingine
 

Similar Discussions

7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom