Kiukweli, uteuzi wa RC Mghwira 'umewakereketa' zaidi wana-CCM

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,176
25,446
  • Wanajua kuwa wao ni wanachama wa chama tawala-CCM.
  • Wanajua kuwa CCM ndiyo inayounda Serikali baada ya kushinda kwenye uchaguzi mkuu mwaka 2015.
  • Wanajua kuwa, kama chama tawala, wanapaswa kutekeleza Ilani ya CCM waliyoinadi wakati wa uchaguzi.
  • Wanajua kuwa Serikali ya CCM inatokana na wanachama wa CCM.
  • Wanajua kuwa wapo vijana na watu wazima 'walioonekana' kwa Rais na kuteuliwa hapa au pale. Mfano, wale Vijana waliokuwa wakiitwa JUKWAA LA WAZALENDO.
  • Wanajua kuwa utetezi wa chama chao CCM mitandaoni, redioni na runingani si utetezi wa hivihivi na wa kizalendo. Ni utetezi wa kimaslahi katika kuvizia teuzi mbalimbali.
  • Wanajua na kuamini kuwa CCM ina hazina ya wanachama wanaoweza kushika nafasi yoyote ya kiuongozi Serikalini. Kwanini atoke ACT-Wazalendo?
  • Wanajua kuwa Rais anawapenda wanachama wa chama chake na anawatumikia watanzania kwa uwezo wake wote ili kuendelea kuking'arisha chama chake. Kwa RC Mghwira vipi tena?
  • Wanajua kuwa CCM imeuda na kutawala Serikali na Bunge na bado teuzi huongeza morali ya 'kujituma' ndani ya CCM. Hapo kwa RC Mghwira vipi?
  • Wanajua na kuamini kuwa wapinzani hawana watu kama wao wenye uwezo na uzoefu wa uongozi wa kitaifa.
Kimsingi, wanachama na wapenda CCM 'wamekereketwa' zaidi na uteuzi wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Taifa wa ACT-Wazalendo Anna Elisha Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro. Wanaumia tu kimoyomoyo. Tafadhali wana-CCM, wekeni mbele maslahi ya Taifa. Taifa hili ni letu sote. Msikasirike wapinzani kuongoza.
 
May be!! But its not the first time kwa Mwenyekiti wa CCM kufanya hivyo.
 
makundi ya wasapu yamepoa. ngoja nami nigombee uvfisiem nianze jaramba. ikifika 2022 kimyakimya naachana na siasa.

na hata hivyo Nina mishe zangu zakuniingizia kitoweo.
 
Inashangaza namna upinzani mlivyolikomalia utafikiri hii ni mara ya kwanza kwa jambo kama hili kufanyika, Mbatia alipoteuliwa kuwa Mbunge na Kikwete kelele hazikua kubwa hivi, nadhani maumivu makubwa yapo huko Chadema maana walikua wanaona wanastahili kumbe hamnna lolote. Kuna vyama vidogo tu vina watu potential kuliko chadema na lundo la wanasiasa wasio na weledi wala ubunifu zaidi ya kauli za kutisha na kukatisha tamaa.
 
Inashangaza namna upinzani mlivyolikomalia utafikiri hii ni mara ya kwanza kwa jambo kama hili kufanyika, Mbatia alipoteuliwa kuwa Mbunge na Kikwete kelele hazikua kubwa hivi, nadhani maumivu makubwa yapo huko Chadema maana walikua wanaona wanastahili kumbe hamnna lolote. Kuna vyama vidogo tu vina watu potential kuliko chadema na lundo la wanasiasa wasio na weledi wala ubunifu zaidi ya kauli za kutisha na kukatisha tamaa.
Mkuu, kuna tofauti kubwa kati ya Mbunge na Mkuu wa Mkoa. Mmoja ni wa Bungeni na mwingine ni wa Serikalini. Fikiri tena.
 
Kwa ubinadamu lazimu uumie kwa kuwa wao (CCM) wamekitumikia chama kwa muda mrefu labda, wamekipigania kutumia mbinu zote kibakie madarakani sasa wakati wa kula tamuuu anapewa mtu mwingine!!!!
 
kwa sasa maccm imekula kwao. wamebaki kusifia kinafiki huku wakiumia moyoni
Ukiitazama CCM hamna kitu hasahasa wabunge ,wao ni kudandia hoja tu,wanajikanyagajikanyaga isu ya mchanga wa madini itakuwa kama faru John badae isu ikiwa ngumu wataipotezea na wanakuwa kama gar bov stering inacheza cheza wanakosa inakosa muelekeo,
Bila kupepesa macho ni ndumilakuwili wapo wapo tu ingawa sio waote.WACHA WAISOME NAMBA.
 
Bashite amewaponza wengi, mkuu amegundua wengi ni MA..bashite eg. Gambo kaamua kutafuta wakuu wa idara nje ya ccm..kazi ni kwao wabaki kuimba tu sasa wenye akili warudi shule na wasome pia UTAWALA..
 
Inashangaza namna upinzani mlivyolikomalia utafikiri hii ni mara ya kwanza kwa jambo kama hili kufanyika, Mbatia alipoteuliwa kuwa Mbunge na Kikwete kelele hazikua kubwa hivi, nadhani maumivu makubwa yapo huko Chadema maana walikua wanaona wanastahili kumbe hamnna lolote. Kuna vyama vidogo tu vina watu potential kuliko chadema na lundo la wanasiasa wasio na weledi wala ubunifu zaidi ya kauli za kutisha na kukatisha tamaa
 
10 Reactions
Reply
Back
Top Bottom