Kiukweli siyo Wakuu wa mikoa pekee, hata Mawaziri wanapaswa kujifunza kwa Makonda

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,780
141,667
Pamoja na kwamba wakuu wengi wa mikoa ubunifu wao bado uko chini hali inayowafanya waachwe mbali kiutendaji na mkuu wa mkoa wa Dsm, mimi naona hata baadhi ya mawaziri wanalo la kujifunza kutoka kwa huyu kijana. Kwa mfano wakati Rais akihangaika kuziba mianya mbalimbali ya upotevu wa mapato ya serikali na kuitengenezea vyanzo vipya, Wizara ya maliasili na utalii imekuwa butu kabisa katika ubunifu. Nimshauri tu waziri wa maliasili analo la kujifunza ktk area ya ubunifu kwani tunaitazama wizara yake kama sehemu muhimu sana katika kuongeza pato la serikali. Wapo mawaziri wengine mfano Mazingira, Kilimo na hata yule wa biashara na uwekezaji tunahitaji kuwaona mkija na ubunifu na siyo vibaya mkapita katika ofisi ya RC Dsm kujichotea uzoefu. Kwakweli tukiweka chuki zetu za kisiasa pembeni na kujikita kwenye utendaji tutakubaliana kuwa kijana anapiga kazi. Wakuu haya mambo ya kusoma sana ni kukariri tu fikra za watu wengine na ndio maana Prof Lipumba Cuf iliyojengwa na kina Mapalala inamfia mikononi kama ilivyo kwa Prof Muhongo aliyechemka kwenye mambo aliyoyabobea! Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni hata kama hamumpendi!!!
 
Mawaziri wengi sana ni Mizingo halafu karibia wote walisha haribu huko nyuma awamu ya 4, Magufuli sijui kwanini anawakumbatia,

Mawaziri wote wazee waondolewe, waingizwe vijana wenye ubunifu, angalia wizara ya Maji, katibu mkuu anafanya kazi zaidi ya waziri mwenyewe

Angalia wizara ya utalii yule mzee akapumzike awekwe kijana
 
Mawaziri wengi sana ni Mizingo halafu karibia wote walisha haribu huko nyuma awamu ya 4, Magufuli sijui kwanini anawakumbatia,

Mawaziri wote wazee waondolewe, waingizwe vijana wenye ubunifu, angalia wizara ya Maji, katibu mkuu anafanya kazi zaidi ya waziri mwenyewe

Angalia wizara ya utalii yule mzee akapumzike awekwe kijana
Mkuu umegonga mulemule!
 
Makonda,amajenga wodi za wagonjwa mpya kabisa katika wilaya zote
Makonda amemaliza kabisa tatizo la akina mama kulala wanne kwenye kitanda kimoja
Makonda anaelekea kumaliza kabisa tatizo la vyumba vya waaalimu mkoani Dar
Makonda anatoa viwanja 3,000 kwa akina mama na vijana kwa ajili ya kujenga viwanda vidogo na vya kati na watawezeshwa na manispaa husika
 
Makonda,amajenga wodi za wagonjwa mpya kabisa katika wilaya zote
Makonda amemaliza kabisa tatizo la akina mama kulala wanne kwenye kitanda kimoja
Makonda anaelekea kumaliza kabisa tatizo la vyumba vya waaalimu mkoani Dar
Makonda anatoa viwanja 3,000 kwa akina mama na vijana kwa ajili ya kujenga viwanda vidogo na vya kati na watawezeshwa na manispaa husika
Tena ni afadhali mawaziri wamehamia Dodoma maana walikuwa wanadai wanaingiliwa!
 
huyo makonda wenu endeleeni kumpamba ila ajiandae tu ataondoka na huyo anaempa kiburi. siku hazigandi
 
Pamoja na kwamba wakuu wengi wa mikoa ubunifu wao bado uko chini hali inayowafanya waachwe mbali kiutendaji na mkuu wa mkoa wa Dsm, mimi naona hata baadhi ya mawaziri wanalo la kujifunza kutoka kwa huyu kijana. Kwa mfano wakati Rais akihangaika kuziba mianya mbalimbali ya upotevu wa mapato ya serikali na kuitengenezea vyanzo vipya, Wizara ya maliasili na utalii imekuwa butu kabisa katika ubunifu. Nimshauri tu waziri wa maliasili analo la kujifunza ktk area ya ubunifu kwani tunaitazama wizara yake kama sehemu muhimu sana katika kuongeza pato la serikali. Wapo mawaziri wengine mfano Mazingira, Kilimo na hata yule wa biashara na uwekezaji tunahitaji kuwaona mkija na ubunifu na siyo vibaya mkapita katika ofisi ya RC Dsm kujichotea uzoefu. Kwakweli tukiweka chuki zetu za kisiasa pembeni na kujikita kwenye utendaji tutakubaliana kuwa kijana anapiga kazi. Wakuu haya mambo ya kusoma sana ni kukariri tu fikra za watu wengine na ndio maana Prof Lipumba Cuf iliyojengwa na kina Mapalala inamfia mikononi kama ilivyo kwa Prof Muhongo aliyechemka kwenye mambo aliyoyabobea! Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni hata kama hamumpendi!!!
It is true kabisa makonda anachapa kazi kizalendo sasa watu wanaomsema kuhusu hajasoma sasa si ni bora wamsifie kwa anachokifanya kuipeleka tanzania mbele kwasababu wapo waliosoma lkn hamna atakae weza kufanya kama makonda
 
Lile ni kama chapuo la kupewa uwaziri... mara paap jamaa katua tamisemi uwiiiii
 
Pamoja na kwamba wakuu wengi wa mikoa ubunifu wao bado uko chini hali inayowafanya waachwe mbali kiutendaji na mkuu wa mkoa wa Dsm, mimi naona hata baadhi ya mawaziri wanalo la kujifunza kutoka kwa huyu kijana. Kwa mfano wakati Rais akihangaika kuziba mianya mbalimbali ya upotevu wa mapato ya serikali na kuitengenezea vyanzo vipya, Wizara ya maliasili na utalii imekuwa butu kabisa katika ubunifu. Nimshauri tu waziri wa maliasili analo la kujifunza ktk area ya ubunifu kwani tunaitazama wizara yake kama sehemu muhimu sana katika kuongeza pato la serikali. Wapo mawaziri wengine mfano Mazingira, Kilimo na hata yule wa biashara na uwekezaji tunahitaji kuwaona mkija na ubunifu na siyo vibaya mkapita katika ofisi ya RC Dsm kujichotea uzoefu. Kwakweli tukiweka chuki zetu za kisiasa pembeni na kujikita kwenye utendaji tutakubaliana kuwa kijana anapiga kazi. Wakuu haya mambo ya kusoma sana ni kukariri tu fikra za watu wengine na ndio maana Prof Lipumba Cuf iliyojengwa na kina Mapalala inamfia mikononi kama ilivyo kwa Prof Muhongo aliyechemka kwenye mambo aliyoyabobea! Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni hata kama hamumpendi!!!

Makonda amekuwa na initiatives nyingi ambazo somehow zinaonekana kufanikiwa, ila tukumbuke;

1. Makonda ni mkuu wa mkoa mwenye support ya waziya mheshimiwa raisi na akikujia kuomba mchango lazima utatoa

2. Mkoa wa Dar es Salaam una vyombo vyote vya habari, hivyo ni rahisi kupata a cheap coverage ukilinganisha na Mkoa kama Katavi, Kagera, n.k

3. Zaidi ya asilimia 70 ya uchumi wa Nchi hii kwa maana ya makampuni makubwa yapo Dar es Salaam, hivyo hata budgets nyingi za CSR zinakuwa controlled from Dar.
 
Makonda amekuwa na initiatives nyingi ambazo somehow zinaonekana kufanikiwa, ila tukumbuke;

1. Makonda ni mkuu wa mkoa mwenye support ya waziya mheshimiwa raisi na akikujia kuomba mchango lazima utatoa

2. Mkoa wa Dar es Salaam una vyombo vyote vya habari, hivyo ni rahisi kupata a cheap coverage ukilinganisha na Mkoa kama Katavi, Kagera, n.k

3. Zaidi ya asilimia 70 ya uchumi wa Nchi hii kwa maana ya makampuni makubwa yapo Dar es Salaam, hivyo hata budgets nyingi za CSR zinakuwa controlled from Dar.
Mkuu nakubaliana na wewe lakini huko mikoani ndiko kwenye rasilimali kibao na vivutio vya utalii, RCs wa huko wanashindwaje kuvifanyia ubunifu endelevu!!!
 
Mkuu nakubaliana na wewe lakini huko mikoani ndiko kwenye rasilimali kibao na vivutio vya utalii, RCs wa huko wanashindwaje kuvifanyia ubunifu endelevu!!!

Toa mfano kwa mkoa kama Iringa au Katavi RC anatakiwa afanye nini? Huko tunajua wahimiza kilimo, - tunapata chakula mjini, wanahimiza upandaji miti tunapata mbao n.k, wanahimiza utunzaji wa vyanzo vya maji, wanahimiza ujenzi wa madarasa, elimu ya afya ya msingi n.k.
 
Back
Top Bottom