Kiukweli Rais Magufuli ndio mwanasiasa pekee Tanzania aliyeanza moto na anamaliza miaka mitano moto bila kupoa

mitale na midimu

JF-Expert Member
Aug 26, 2015
10,420
17,701
Moto alioanza nao ndio anamaliza nao. Kuna watu tulidhani pumzi itakata katikati ya safari ila hilo halijaonekana.

Ameanza kwa kuogopwa na anamaliza kwa kuogopwa.

Hili nililithibitisha siku amezushiwa kufariki mitandani, Kuna jamaa mmoja mtumishi wa Umma alishukuru akasema afadhali aondoke tuanze kupiga madili. Basi nikajua kumbe jamaa moto haujakata.

Hadi leo maofisini pakisikia Rais anakuja, kiwango cha hofu kama mtu atimizi wajibu kiko vilevile kama alivyoanza kazi.

Kiukweli tukubali au tukatae Rais Magufuli amekuja na suprise kubwa kwenye siasa na utumishi wa umma. Amefaulu kuanza na kumaliza kama alivyoanza bila kulegea wala kuchoka, wala kukompromise misimamo yake na style yake ya kuongoza.

Hii imenifundisha kitu, hata katika mambo madogo madogo na viuongozi vyetu huku mitaani. imenikumbusha yule Mtanzania aliyevunja rekodi ya mbio za masafa marefu kwa kuanza kwa kasi na kumaliza kwa kasi akiongoza huku wengine wakitegemea atakata pumzi njiani.
 
Lakini kwanini bado mtaani hali mbaya hakuna ajira zilizo na zisizorasmi bado zipo za kutosha watumishi bado wanalia na mishaara midogo bado huduma ya afya iko chini mpaka ukienda mochwari kuchukua maiti haurusiwi mpaka madeni yake ya kulazwa yalipwe ajabu ajabu kwa kweli
 
Ndo nashanga kuna watu wanataka kutuwekea mtu wao ambaye hana rekodi yeyote.
mkuu JPM kavunja rekodi, hata mimi nilikuwa namuhesabia.
nilijua ni nguvu za soda, ila hajateteleka ameendelea kuwa hatari zaidi katika kukikalia kiti chake bila kucompromise.

Nakumbuka nilikuwa mshabiki wa JK ila Baada ya Richmond akawa neutral hadi anaondoka.
 
Lakini kwanini bado mtaani hali mbaya hakuna ajira zilizo na zisizorasmi bado zipo za kutosha watumishi bado wanalia na mishaara midogo bado huduma ya afya iko chini mpaka ukienda mochwari kuchukua maiti haurusiwi mpaka madeni yake ya kulazwa yalipwe ajabu ajabu kwa kweli
Yawezekana aina ya uongozi aliokuja nao kuna sehemu alipaswa kupafanyia maboresho.
nilimsikiliza mchumi mmoja anamuelezea na mkakati wake wa kuboresha miundombinu akasema ni mkakati wa kisasa na sahihi kabisa, hata kuna jamaa humu tulijaeili hadi notice za uchumi havard zikawekwa humu.

Ila ilitegemewa baada ya miaka kama miwli mitatu kwa startergy hii angalau ianze kuonyesha unafuu lakini naona bado hali sio rafiki sana.

kuna sehemu wenda anakwama.

ila kwa maana ya continuity ya misimamo aliyoanza nayo ajayumba wala hajatoa unafuu wowote kuyumbishwa hadi sasa. hicho ndio nakisemea.
Hajawahi kutokea diwani, mbunge au rais nchiñ aliyeonyesha consistence ya kiwango tunachoonyeshwa sasa.
 
Unadhani kiongozi kuogopwa na kuchukiwa ni sifa njema? Huyu amefeli big time
Kwa nini anaogopwa ndio sababu ya msingi. Aogopwi kwa sababu atakuua. bali kwa sababu kama uko nje au kinyume na kile ulichotarajiwa kufanya atakchukulia hatua.

wengine walianza kwa kuogopwa katikati ya safari wakawa neutral wakaishia kupuuzwa au kutohofiwa maana unauhakika kwa sasa hawezi kuchukua maamuzi magumu.

kufeli kwa mambo mengine sio hoja yangu,
 
mitale na midimu,
Sawa nikuambie kitu mkuu naomba uninukuu Upinzani bado utakuwa na utaendelea kuwa hai kwa sababu
Bado CCM haijawahi kujua majawabu sahihi ni nini wananchi wanachotaka ili waende sawa.

Na ndie Raisi mwenye nafasi nzuri ya kuwavuta raia wake kidiplomasia
Na ndie angejenga desturi ya kufanya mijadara na wapinzani wote kwa maana ya kujitasmini jee anacho kifanya kina reflection na ndoto zao endapo wangepata hiyo nafasi
 
Kajitahidi,kafanya kazi kubwa sana, mambo mengine ni ya kibinadamu.Twende naye tena Octoba 2020
 
Punguza ujinga kidogo japo nukta tu. Unaijua nguvu ya mamlaka ya Rais hata hadi uje umfananishe na Mbunge au Diwani?!
Huyu mbunge nimemlinganisha na ambayo huwa anaahidi kwenye kampn na jinsi ambayo anawahakikishia atatekeleza.

Rais namlinganisha na nguvu zake ambazo hata wenzake waliopita waliokuwa nazo ila Kuna utofauti Ktk consistency
 
Back
Top Bottom