KERO Kituo cha SGR – Dar kitengewe sehemu ya madereva kuchukua abiria wao, kulipia buku hata kama unapita tu si sawa

KERO Kituo cha SGR – Dar kitengewe sehemu ya madereva kuchukua abiria wao, kulipia buku hata kama unapita tu si sawa

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Madereva tunapata changamoto kubwa pale kwenye Kituo cha SGR kilichopo Stesheni, Dar es Salaam, wanatukamata tukienda kubeba abiria, wanataka tuingie ndani ili tulipie shilingi 1,000, wakati sisi ni madereva wa mtandaoni na pale tunapita tu siyo kwamba tunaenda kuegesha vyombo vyetu.

Namaanisha kwamba wangetenga sehemu ya kuchukua abiria iwe tofauti na yule ambaye anaingia kupaki.

Unakuta abiria ana ku request sehemu ya shilingi 2000, mimi niingie hapo nilipe buku, kisha Bolt nao wakikata hela yao Asilimia 25, sasa hapo si ninakuwa nimefanya kazi bure tu.
 
Kwa ninavyojua, ukirequest Bolt mfano, ukiweka pickup point Mlimani City, gharama ya kuingia inajumlishwa kwa mteja. Same na ukipita kwenye toll bridges kama Kigamboni au Nyerere, Airport, etc.

Naamini na vituo hivyo wangeweka Bolt wenyewe hiyo option.
 
Hii parking ya SGR wangeweka 30minutes free(No return within 2hrs) ingesaidia hata kupunguza foleni. Mtu alipie akikaa zaidi ya 30 minutes. Tatizo wanawaza pesa tu.
Angalia wana long term parking 24hrs 20,000/- si afadhali nije na Bolt kuliko kuacha gari. Wangeweka 10,000/- kwa saa 24 watu wengi wangeacha magari na kusafiri na wangepata hela nyingi zaidi.
 
Hii parking ya SGR wangeweka 30minutes free(No return within 2hrs) ingesaidia hata kupunguza foleni. Mtu alipie akikaa zaidi ya 30 minutes. Tatizo wanawaza pesa tu.
Angalia wana long term parking 24hrs 20,000/- si afadhali nije na Bolt kuliko kuacha gari. Wangeweka 10,000/- kwa saa 24 watu wengi wangeacha magari na kusafiri na wangepata hela nyingi zaidi.
Wenye mawazo mazuri hawana madaraka ya kuamua mambo.
 
Kwa ninavyojua, ukirequest Bolt mfano, ukiweka pickup point Mlimani City, gharama ya kuingia inajumlishwa kwa mteja. Same na ukipita kwenye toll bridges kama Kigamboni au Nyerere, Airport, etc.

Naamini na vituo hivyo wangeweka Bolt wenyewe hiyo option.

Hata bolt kama unataka kwenda SGR wanaweka price za kushushwa nje/Ndani
 
Kwa ninavyojua, ukirequest Bolt mfano, ukiweka pickup point Mlimani City, gharama ya kuingia inajumlishwa kwa mteja. Same na ukipita kwenye toll bridges kama Kigamboni au Nyerere, Airport, etc.

Naamini na vituo hivyo wangeweka Bolt wenyewe hiyo option.
Unataka waendelee kupiga wananchi ili wapate fedha za kununua mikoba ya mamilioni ya kuwekea makaratisi ya bajeti? Unataka wazidi kununua Rolls Royce wakati wananchi wanakufa kwa kukosa dawa? Ndugu yangu hizo fedha zinaishia mifukoni mwa watu na ndiyo maana wanakuwa wakali kutaka uingie ndani. Ktuo kama hicho kinatakiwa kiwe na sehemu ya kushushia na kupakia abiria kwa haraka.
 
Hii parking ya SGR wangeweka 30minutes free(No return within 2hrs) ingesaidia hata kupunguza foleni. Mtu alipie akikaa zaidi ya 30 minutes. Tatizo wanawaza pesa tu.
Angalia wana long term parking 24hrs 20,000/- si afadhali nije na Bolt kuliko kuacha gari. Wangeweka 10,000/- kwa saa 24 watu wengi wangeacha magari na kusafiri na wangepata hela nyingi zaidi.
Katika vitu ambavyo kama ikiingia serikali makini inatakiwa iondowe kabisa ni hizo tozo za aina hii. Fedha asilimia 90 ya fedha zinazopatikana kwa tozo za aina hii zinaingia kwenye mifuko ya watu. Unakuta ki-stendi uchwara kimewekwa mahali halafu kila basi linalazimishwa kuingia ndani ili kulipa tozo. Na wanakuwa wakali kweli kweli kwa sababu haya ni mapato yao. Inatakiwa kuwe na ulipaji wa tozo usioruhusu upigaji wa kirahisi.
 
Back
Top Bottom