Jaji Mfawidhi
JF-Expert Member
- Feb 20, 2016
- 13,992
- 20,282
Jina la Kituo HALINA MVUTO, limeacha majeraha mengi kwa watu wa kimara na mbezi kuvunjiwa bila fidia huku watu kama hao huko mwanza kwao alisema wasivunjiwe.Sasa kama mjasiriamali amepewa fremu ili auze maji na soda ndani ya kituo ghorofani kwa kodi (rent) ya Tsh. 36,028,200/= kwa mwezi sawa na Tsh. 1,201,000/= kwa siku uhalisia uko wapi! Machinga wanauza maji na soda hizo hizo ndani na nje ya kituo hicho hicho kwa rent ya kitambulisho chake cha Tsh, 20,000/= kwa mwaka sawa na Tsh. 55 kwa siku.
Attached ni mchanganuo wa bei ya pango kama ulivyoidhinishwa na DCC kabla haijavunjwa na Hayati Rais Magufuli mwezi February 2021 wakati wa uzinduzi.
Data hizo ni kutoka waraka ulioidhinishwa na aliyekuwa Mkurugenzi wa DCC uliosomeka "“Majina ya walioshinda zabuni ya upangishaji maeneo ya biashara na utoaji huduma mbalimbali katika Kituo Kikuu cha Mabasi Mbezi Luis 2020”
Mipango mingi ya ajabu ya aina hii kupitia TAMISEMI imeshindwa kama vile: Bus stand ya Dodoma, Machinga Coplex ya pale Ilala, Mwal Nyerere Airport Terminal 3, machinjio ya Vingunguti nk.
Ummy Mwalimu take action please, hapo hakuna biashara.
Data hizo ni kutoka andiko G. Kombe.
View attachment 1756589
by the way, makada wa CCM ndio waliopata hivyo viduka wacha wapambane na hali zao.