Kituo cha Haki za Binadamu (LHRC) champongeza Rais Samia kwa usikivu wake, chamuomba afute kabisa tozo za miamala!

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,821
141,728
Kituo cha haki za binadamu Tanzania (LHRC) kimempongeza Rais Samia kwa namna alivyoingilia kati swala la tozo za kizalendo zilizoanza kuumiza na kutesa wananchi

LHRC wamemuomba Rais Samia kuzifuta kabisa tozo hizo kwani zinaua uchumi badala ya kuujenga.

Nawasalimu kwa jina la JMT!
 
Viongozi wanamuingiza mama choo chá kiume. Inabidi awaangalie sana kwa kuwa wanampoteza
Nalog off
 
Aliyeazisha hili tatizo ni SSH, hivyo alilianzisha ili alimaliza yeye mwenyewe. Sasa mnampongeza Kwa lipi? Sijaelewa
 
Unampongeza mtu kwa kutengeneza tatizo na kulitatua?

Nchi zingine shirika kama ili wana-organize maandamano na kufanya movement za amani kusaidia wananchi kupata haki zao.

Wao wanaleta porojo za kupongeza kwa matatizo caliphate gene za wenyewe

Huu upumbavu wasomi uchwara nchi hii sijui utaisha lini.
 
Mwendazake asilimia kubwa aliendesha nchi na miradi kwa hela zakulazimisha kwa watu kwenye fedha nyingi benk.Huku wananchi wakidanganywa eti mapato ya ndani.

Akiona akaunti ya mtu ina madini mengi,

NCHI HII INA HERA

NCHI HII NI DONA KANTIRI!

TUMECHEZEWA SANA

Waliompitisha apate urais eti wamechezea nchi.

Baada ya Siku kadhaa anawaalika ikulu wastaafu watoe mawazo yao
 
Huyu rais ana mchakato wa kufanya consultation katika kusaini mambo anayoletewa?

Chama kina mfumo wa kuhakiki hoja na washikadau kabla ya kupeleka mambo bungeni yapitishwe ili kuwa sheria?

Rais kubadili mambo yaliyopitishwa kwa saini yake baada ya kuona wananchi wanapinga ni jambo zuri.

Lakini, jambo hili la kubadilishabadilisha mambo, government by trial and error, linaondoa imani ya wananchi kwa serikali.

Serikali inaonekana inaenda kwa kubahatishabahatisha, haifanyi utafiti wa kina kabla ya maamuzi makubwa.
 
Pongezi hizo ni pigo kubwa kwa Mbowe na genge lake, ambao siku zote wanapenda kuona serikali ikilaaniwa na kulalamikiwa na mashirika mbali mbali ya kitaifa na kimataifa.

Pia hili swala la tozo walitaka kulitumia kama ajenda ya kuvuta misukule zaidi ndan ya chama chao kwa bahati nzuri raisi Samia kashtuka.
 
Hawa LHRC wanampongeza vipi Rais wakati:

a)Hajasema kuwa anafuta tozo.

b)Serikali imetengeneza tatizo na kulitatua wenyewe.

c)Huyu Rais ametia fora katika uvunjifu wa haki za binadamu na katiba kwani tokea Nyerere hakuna Rais ambae amewahi kuweka watu 138 ndani waliokusanyika kwa ajili ya kutoa maoni yao ambayo ni haki yao kikatiba kwa wakati mmoja kama alivyofanya Samia jana huko Mwanza.

How possible taasisi kama LHRC wanakuwa na akili fupi kiasi hiki?!
 
Kituo cha haki za binadamu Tanzania ( LHRC) kimempongeza Rais Samia kwa namna alivyoingilia kati swala la tozo za kizalendo zilizoanza kuumiza na kutesa wananchi

LHRC wamemuomba Rais Samia kuzifuta kabisa tozo hizo kwani zinaua uchumi badala ya kuujenga

Nawasalimu kwa jina la JMT!
Kwani hadi implementation inafanyika hakujua? kama ni hivyo basi ni hatari kwa usalama wa nchi yetu.
 
Too soon, wangesubiri kitendo, japo pia sio mbaya wakipongeza kauli ya serikali iliyotolewa, nayo ni hatua kuelekea mageuzi.
 
Kwanza naona ni wanafiki tu hawa mbona hatujasikia wakisemea Hilo suala wanakuja kupongeza tu
 
Huu ni wehu.
Samia alikuwa wapi wakati tozo zomeanza?
Je, hakusaini yeye?
Msituletee mambo ya Magufuli, anafanya jambo, anatengua kisha anampa Makonda hela awalipe uvccm waandamane kumpongeza
 
Huyu rais ana mchakato wa kufanya consultation katika kusaini mambo anayoletewa?
Bunge lililojaa wanaccm ambalo linaimba nyimbo za sifa muda wote ndiyo tatizo. Kulipaswa kuwe na mijadala yenye tija na upana wa kina ktk bajeti na miswada inayopelekwa. Lkn wao kazi yao kuimba sifa. Madhara yake ndiyo haya.
 
Bunge lililojaa wanaccm ambalo linaimba nyimbo za sifa muda wote ndiyo tatizo. Kulipaswa kuwe na mijadala yenye tija na upana wa kina ktk bajeti na miswada inayopelekwa. Lkn wao kazi yao kuimba sifa. Madhara yake ndiyo haya.
Rais naye hawezi kukwepa lawama.

Kwa sababu ana uwezo wa kupewa muswada na kuukataa.

Anaweza kusema "nimepewa muswada huu lakini naona haujashirikisha wadau inavyotakiwa, na tozo zitapanda sana na kuathiri uchumi. Hivyo sitaupitisha muswada na kuufanya sheria mpaka ujadiliwe zaidi na kwenda kwa kufuata kanuni za kiuchumi zaidi kwa data".

Hakufanya hivyo.

Kapitisha tu.
 
Rais naye hawezi kukwepa lawama.

Kwa sababu ana uwezo wa kupewa muswada na kuukataa.

Anaweza kusema "nimepewa muswada huu lakini naona haujashirikisha wadau inavyotakiwa, na tozo zitapanda sana na kuathiri uchumi. Hivyo sitaupitisha muswada na kuufanya sheria mpaka ujadiliwe zaidi na kwenda kwa kufuata kanuni za kiuchumi zaidi kwa data".

Hakufanya hivyo.

Kapitisha tu.
Mkuu, rais (yeye binafsi) inawezekana siyo mzuri Sana kwenye wigo wa kuchambua madhara ya kiuchumi. Hivyo aliwategemea Sana wabunge wafanye uchambuzi wa kina zaidi. Badala yake wabunge wanamwaga sifa tu.
 
Back
Top Bottom