Kitu kipya kinakuja Iphone 8

Zeni2017

JF-Expert Member
Apr 27, 2017
1,247
532
9b585eccad91d3dcc03b4cdf09515ed5.jpg


sasa wabongo hapo ndoa zitavunjika kisa ni Iphone 8. Waume watalazimishwa walipe milioni mbili ili wake wang'are na Iphone 8.

Isiwe tabu wewe kama Tecno yako au Huwaee ina WhatsApp na FB uko vizuri.

Hivi vitu kwa wenzetu haviumizi sana kichwa. Kwanza bili ya simu ni kwa mwezi si ya bando la halichachi. Na mtu anaweza kuwa na plan yenye uprade. Simu mpya ikitoka anarudisha ya zamani anapewa mpya.

Pia mtu anaweza kuchukua simu mpya bila ya kulipa chochote akalipa kidogo kidogo kwenye bili yake ya kila mwezi.

Mwingine anaweza kuzinguana na bima. Akasema simu imepotea akapata mpya.

Yote tisa kumi ni nusu ya vitu vilivyomo kwenye hizi simu babu kubwa havina shughuli yeyote Bongo.

Tuache masihara simu zinamalizia watu hela Bongo kichizi. Wanalalamika bei ya sembe lakini hawapigi hesabu wanapoteza pesa ngapi kwenye hivi visimu.

Halafu wachunguzwe hawa kina Voda kama wamesajiliwa na wanalipa kodi. Wasijekuwa ni wale wale kina mchanga wa dhahabu.
 
Mkuu mbona kama umeleta uzi kuonyesha hasira zako kwa ip users.
Kama hauziwezi ips kuwa mpole.
 
Mkuu kuna mtu analalamika iphone bei ghali ila kwake kuacha 100,000Bar au kuhonga ni kitu cha kawaida sana, sasa piga hiyo 100,000 kwa mwezi ni sh ngapi??

Kila kitu ni maamuzi tuu na mapenzi ya mtu. Pata kitu roho inataka.

[HASHTAG]#iphoneuser[/HASHTAG]
 
Mitandao yetu ya simu haipo creative kabisa. Yaani eti unanunua tecno afu inakubali mtandao mmoja kisha bei unayouziwa ni sawa na ya dukani ambayo inatumia mitandao yote. Wazimu mtupu.
 
Iphone 8 itatoka mwakini mwezi wa tisa, mwezi wa tisa mwaka huu inatoka 7s na ios 11,
Kawaida ya apple huwa wanafanya mabadiliko kidogo ya designing baada ya matoleo matatu na toleo la nne huwa na mabadiliko makubwa zaid.
Iphone 7s inakuwa na utofauti na iphone 7 kwa mtazamo japo sio mkubwa sana ila iphone 8 itakuwa tofauti zaid.
Ila performance ya iphone 8 haitakuwa na tofaut kuwa na iphone 7s, na zote zitamaliza kupokea update pamoja.
Iphone 5s na iphone 6 zinafanana kabisa kiutendaji
Iphone 6s na iphone 7 hali ni hiyo hiyo

Habari zote juu iphone 8 ni zakufikirika bado sio habar ramsi kutoka apple
 
Kitu kinakuja September na kuna ubuyu kuwa kitakuwa hakihitaji waya kuchaji.

Iphone 8 hadi mwakan mwez wa 9 natumia iphone toka iphone 3g had sasa na nimfatiliaji mvur wa update zao kwa kila device zao.
Apple soko lao aliendeshwi na sana kama soko la bidhaa zingine.
Ndio maana had leo hakuna mackbook iliyotoka touch screen ila bado wauza kwa gharama kubwa na kiwango kikubwa
 
12 Reactions
Reply
Back
Top Bottom