Kitu gani kinamfikisha mtu kwenye ufanisi katika maisha

Alnadaby

JF-Expert Member
Sep 28, 2006
505
41
Nimeshakutana na wasomi kila aina,lakini majority yao ni watu wasiokuwa na uwezo hata wa kuendesha maisha yao.Na nimeshakutana na watu wasiokuwa na elimu ya maana...lakini ni watu makini,wana uwezo wa kifedha,wanajiamini na wanaendesha shughuli zao vizuri.
Sasa labda hapa ni kutafuta sababu za hawa wasomi kuwa watu wa vitabu,data,laptop,kuendesha semina n.k lakini wakawa dhaifu inapofika suala la kutajirika,kuwa na mamlaka na kujiamini.

Mfano ni fundi viatu wa miaka ya sitini Said Salim Bakhressa maarufu kwa ice cream na bidhaa tofauti hapa nchini.AU hata Billy Gates..aliyekimbia shule akiwa grade 10...na sasa ni mmoja ya matajiri wakubwa duniani.List yao ni ndefu...kina Ford..n.k.

Je ni kitu gani cha ziada ambacho wasiokuwa na elimu ya juu...walichonacho hadi wakafanikiwa katika malengo yao,ambacho hakipatikani kwa wenye Phd..n.k?
 
Kwanza kitu cha msingi hapo mheshimiwa tafuta a global definition ya MAFANIKIO or SUCCESS.......lakini kwa taarifa yako kila mmoja hapa anaweza kuja na definition yake tofauti na mwingine. So muhimu, tukubaliane kwanza katika jamii, Mafanikio or success ni nini na je, ni wakati gani utasema mtu fulani kafanikiwa? je ni kwa kuwa na majumba, mihela, magari,mademu bomba, cheo kikubwa, mcha Mungu etc ......halafu endelea from there!
 
Mafanikio ya mtu ni pale anapofikia lengo lake,anapokipata alichokuwa akikitaka.Kama lengo lengo lake katika maisha ni kuwa fundi mchundo basi akifaulu hapo anakuwa amefanikiwa.
Unapoweka lengo la kuwa bilionea ukawa hivyo basi hapo utakuwa umefanikiwa.Simple au vipi?
 
[I said:
Alnadaby;324342]Mafanikio ya mtu ni pale anapofikia lengo lake,anapokipata alichokuwa akikitaka.Kama lengo lengo lake katika maisha ni kuwa fundi mchundo basi akifaulu hapo anakuwa amefanikiwa.
Unapoweka lengo la kuwa bilionea ukawa hivyo basi hapo utakuwa umefanikiwa.Simple au vipi?[/I]

Kama lengo lake lilikuwa ni kupata PHD na akapata hiyo PHD na baadaye ukakutana nae na laptop yake huku akiendesha semina hapo utasemaje...

Kwa kuwa lengo lake halikuwa kuja kuwa na fedha nyingi, lengo lake lilikuwa ni kupata PHD, na sasa ana PHD anaishi mlimani uni ana-pick-up 4WD iliyochoka na Ngome wawili wa maziwa, hapo utasemaje, kwa kuwa lengo lake lilikuwa ni kupata PDH na sasa anayo.

WHAT'S SUCCESS FROM YA POINT OF VIEW....au ni success ya Jay-Z kwenye american gangsta.

Twende kazi.
MJ
 
Mafanikio ya mtu ni pale anapofikia lengo lake,anapokipata alichokuwa akikitaka.Kama lengo lengo lake katika maisha ni kuwa fundi mchundo basi akifaulu hapo anakuwa amefanikiwa.
Unapoweka lengo la kuwa bilionea ukawa hivyo basi hapo utakuwa umefanikiwa.Simple au vipi?

That's very simple brother! baada ya kumaliza chuo niliweka malengo ya kupat ajira yenye angalau mshahara wa laki mbili hivi....nikapata zaidi ya hapo, lakini uhalisia wake mpaka sasa najiona sijafanikiwa in life eti kwa kupata more than 200k! nataka nikwambie, ask hao mabilionea wakwambie kama wanaona wanamafanikio, kama sio wewe ndo unaona wanamafanikio! Mi nafikiri mafanikio ya mtu hasa yatapimwa na recognition yake kwenye jamii, how does someone brands himself/herself mbele ya jamii! Kwa mfano, watu kama Mwl. Nyerere, mi naweza sema he was a very successiful man in Tz etc...hizi material things ni vitu vya ziada tu mkuu!

That's ma views mkuu
 
That's very simple brother! baada ya kumaliza chuo niliweka malengo ya kupat ajira yenye angalau mshahara wa laki mbili hivi....nikapata zaidi ya hapo, lakini uhalisia wake mpaka sasa najiona sijafanikiwa in life eti kwa kupata more than 200k! nataka nikwambie, ask hao mabilionea wakwambie kama wanaona wanamafanikio, kama sio wewe ndo unaona wanamafanikio! Mi nafikiri mafanikio ya mtu hasa yatapimwa na recognition yake kwenye jamii, how does someone brands himself/herself mbele ya jamii! Kwa mfano, watu kama Mwl. Nyerere, mi naweza sema he was a very successiful man in Tz etc...hizi material things ni vitu vya ziada tu mkuu!

That's ma views mkuu

Natafuta ni kitu gani kilichomfanya mtu kama Henry Ford wa kwanza kufanikiwa katika kutengeneza gari na hadi kufikia karne hii magari ya Ford yakawa bado yapo.Jamii imtambue isimtambue kama kafanikiwa au la...yale magari yake ndiyo yanayodhirisha kufaulu kwake katika maisha yake na ndiyo yanayomfanya awe successiful na kutambulika baadaye kwa jamii.Achievement yake ilikuja kutambulika na jamii baadaya ya yeye binafsi ku triumph.

Kuweka malengo ya kupata ajira ya mshahara wa laki mbili,hayo hayakuwa malengo halisi bali simple wish.Lengo halisi ni kuwa na burning desire ili kupata mafanikioa in a life time si temporary wish kama hiyo ya mshahara.

Hilo la Nyerere kuwa successiful man..mimi silitambui.Success inaanzia nyumbani kwenye level ya family.Cheki familia yake utajua naotaka kusema nini.Nyerere as a man was never successiful.Alitaka kujenga Taifa la kiujamaa...where is that?Kama Rais hakuwa successiful kabisa!Mimi nataka kujua kwa nini Professor Machunda hakujenga hata kibanda...cha maana huko Ukerewe lakini mtu kama Mwita Gachuma ni tajiri mkubwa.Education ya Machunda ilikuwa na maana gani?
 
Mkuu,

Sina ufanisi mkubwa katika maisha, lakini kuna mambo naweza eleza ama tunaweza kushirikishana. Na, sipendi kuandika mengi sana kwa mkupuo lakini ningependa twende kwa njia ya mjadala.

Nianze kwa kusema kuwa ufanisi wowote unatokana na dhamira.

Watu wengi wana dhamira lakini dhamira zao si thabiti. Wakidhamiria jambo basi katikati wanaingiza mambo. Ukichanganya mambo mawili wakati mmoja haijalishi wewe ni Genius kiasi gani bado utaharibu sehemu moja tena uombee sehemu hiyo isiwe ile ambayo ndiyo ingekuinua.

Ni ukweli mwingine usiopingika kuwa dhamira yoyote inahitaji kujitoa. Hapo ndipo inaposimama imani yangu: Maisha bila kuchukua risks hayafai hata kuishi!

Ni kweli; ukiwa na elimu nzuri basi maisha ya kati unaweza kuyaishi. Yani yale maisha ya kupata walau $2,000.00 kwa mwezi na kuwa na uhakika wa watoto kula na kusoma shule za kawaida (bila ufisadi) na kijigari chako cha kutokea utakuwa nayo.

Wasomi wengi hawako tayari ku-risk! Huwa sijui sababu nyuma ya hili, lakini ukweli ni kwamba wengi wao wanaridhika na hali walizofikia na labda wanaogopa sana kuchafua CVs zao. Ni wachache wenye kuthubutu! Hawa ni wazuri kwa maneno na wanaweza hata kuwa daraja la wale wenye uwezo wa kuthubutu kufanikiwa. Hawa huweza hata kuwapa mbinu za biashara wale wenye kuthubutu na kujikuta wanabakia na nafasi ya 'Consultants' (washauri?).

Wale wenye elimu za kati huwa wanajaribu kila jambo. Lile ambalo wanaona linawezekana, hulipangia mikakati ya namna ya kulifanikisha na endapo wanadhamiria kabisa kufanikisha basi hufanikisha.

Nifupishe kwa sasa, niache nafasi ya wengine au hata mwanzisha mada kuongea ili twende sawa. Kama ni vitabu vya kusoma juu ya haya naweza kuwaletea lakini kwanza mada ikolee...
 
Mkuu hapo umenipa faida.Kwa njia rahisi kuwa na dhamira katika kile unachokitaka katika maisha ndiyo hatua ya awali.
Baada ya hapo sasa ni kukubali kuchukua risk!Hapo kwa wasomi wengi ndipo kwenye kikwazo.
Na hili la kukuta wasomi wengi ni ma consultants wa hao risk takers si la lujificha limeenea kila upande.

Kuna mchumi mmoja alikuwa msaidizi na consultant mzuri wa bilionea fualni hapa nchini.Siku moja yule bilionea aliamua kumwachisha kazi na kumpa mtaji mkubwa ili naye awe tajiri.Baada ya miaka miwili tu aliyepewa mtaji alirudi kwa bilionea kuomba ajira yake ya zamani maana hakuwa na kile kitu ambacho yule bilionea alikuwa nacho.Alishindwa kabisa kuendesha bishara yake binafsi wakati mataji kapewa na nyenzo anazo.Ni kitu gani alimiss mtu yule...Probably alikuwa anaogopa kutake decisions nzito..
 
Maxence

Consultants wengi wanachukua mshiko mzuri sana, so sidhani kama ni sawa kuwalabel kuwa hawajasucced.
Pia watu tunaona hao waliosucced by taking risk lakini hatuoni wote waliofeli
"According to the U.S. Small Business Administration, over 50% of
small businesses fail in the first year and 95% fail within the first
five years.? "
 
Natafuta ni kitu gani kilichomfanya mtu kama Henry Ford wa kwanza kufanikiwa katika kutengeneza gari na hadi kufikia karne hii magari ya Ford yakawa bado yapo.Jamii imtambue isimtambue kama kafanikiwa au la...yale magari yake ndiyo yanayodhirisha kufaulu kwake katika maisha yake na ndiyo yanayomfanya awe successiful na kutambulika baadaye kwa jamii.Achievement yake ilikuja kutambulika na jamii baadaya ya yeye binafsi ku triumph.

Kuweka malengo ya kupata ajira ya mshahara wa laki mbili,hayo hayakuwa malengo halisi bali simple wish.Lengo halisi ni kuwa na burning desire ili kupata mafanikioa in a life time si temporary wish kama hiyo ya mshahara.

Hilo la Nyerere kuwa successiful man..mimi silitambui.Success inaanzia nyumbani kwenye level ya family.Cheki familia yake utajua naotaka kusema nini.Nyerere as a man was never successiful.Alitaka kujenga Taifa la kiujamaa...where is that?Kama Rais hakuwa successiful kabisa!Mimi nataka kujua kwa nini Professor Machunda hakujenga hata kibanda...cha maana huko Ukerewe lakini mtu kama Mwita Gachuma ni tajiri mkubwa.Education ya Machunda ilikuwa na maana gani?

Will come back to you on this brother!
 
Consultants wengi wanachukua mshiko mzuri sana, so sidhani kama ni sawa kuwalabel kuwa hawajasucced.
Pia watu tunaona hao waliosucced by taking risk lakini hatuoni wote waliofeli
"According to the U.S. Small Business Administration, over 50% of
small businesses fail in the first year and 95% fail within the first
five years.? "
Dah,

Simaanishi kuwa Consultants hawana kipato kizuri. Tena kwa mimi niliye katika Construction Industry najua wazi kuwa hawa jamaa wana kipato kizuri sana.

Yani jaribu kumsoma mwanzisha mada na unaweza kunipata.

Naamini kila binadamu ana mafanikio japo si rahisi wengine kujiona kuwa wamefanikiwa kwakuwa hawajaribu kukumbuka wapi wametoka, walipo na kuangalia wanakoelekea
 
  • Thanks
Reactions: BIR
Check your facts! Gates studied at Harvard and took a leave of absence after deciding to start Microsoft.

Haya sawa...the fact that he dropped out(call it leave of absence) from Harvard to start his business is exactly that made him what he is today.
 
What's a connection between "success and dream come true"..there is a guy who's dream was to write a book, he tried to put everything together and get his book done in 5years. After he was busy looking for a publisher, he finally succed to get one and his book was hitting printing press, when that book was our hitting book shelves he said he was a happiest man in earth and his mission was complited, that he can now die happy....... did this man succeded?.

au mpaka uwe na nyumba ya kifahari, na magari ya kumwaga..

coz for that guy he believed he was born to write that book.

thx

MJ
 
Consultants wengi wanachukua mshiko mzuri sana, so sidhani kama ni sawa kuwalabel kuwa hawajasucced.
Pia watu tunaona hao waliosucced by taking risk lakini hatuoni wote waliofeli

"According to the U.S. Small Business Administration, over 50% of
small businesses fail in the first year and 95% fail within the first
five years.? "

Hapa kuna walakini, wengi ni wale walio ajiriwa na consultants firms kama KPMG, Delloitte, PWC n.k.

AU?

MJ
 
I will talk in absolutes to starkly underline the dire straits faced in a ploy at scaling the task of efficiency.

There is no such thing as ufanisi, maybe in relative form (of course) but the mediocrity of it all is cavalierly pedestrian to interest the passion of the generalist addressing this undefined, teasing pantomime.Efficiency is the stuff specifics starved middle managers throw around when they cannot muster the details enough to wrang a justifiable attack at the underlings, it is the epitomy of the Selassian illusion, to be pursued but never attained and therefore, for such middle managers, ideal for smirking guilt infested presentations without appearing to be in overdrive.

In the physical world Heinserberg's Uncertainty Principle rule out the perfect knowledge of a particles speed and position, likewise the speed of light, as verified by relativistic models, is unattainable by any matter, our very own existence is subject to probabilistic quantum wave functions to Einstein's dismay. We cannot create 100 efficient machines, cannot manufacture a perfect vacuum.

The only efficiency we can be guaranteed of that of being inefficient.
 
Last edited:
Consultants wengi wanachukua mshiko mzuri sana, so sidhani kama ni sawa kuwalabel kuwa hawajasucced.
Pia watu tunaona hao waliosucced by taking risk lakini hatuoni wote waliofeli
"According to the U.S. Small Business Administration, over 50% of
small businesses fail in the first year and 95% fail within the first
five years.? "


I am searching as to why some people succeed in life while others don't.Why some businesses fail and others thrive?

People who have had just a few years of education are most successiful than many graduates out there! What make the laymen succeed in business which most of the graduates do not have?

This is the point of my discussion.It would assist most of us in finding out what makes a successiful person...
 
What's a connection between "success and dream come true"..there is a guy who's dream was to write a book, he tried to put everything together and get his book done in 5years. After he was busy looking for a publisher, he finally succed to get one and his book was hitting printing press, when that book was our hitting book shelves he said he was a happiest man in earth and his mission was complited, that he can now die happy....... did this man succeded?.

au mpaka uwe na nyumba ya kifahari, na magari ya kumwaga..

coz for that guy he believed he was born to write that book.

thx

MJ
Huyo aliyendika kitabu alitimiza ndoto zake.Limitation yake ya success ilifikia hapo.
 
What's a connection between "success and dream come true"..there is a guy who's dream was to write a book, he tried to put everything together and get his book done in 5years. After he was busy looking for a publisher, he finally succed to get one and his book was hitting printing press, when that book was our hitting book shelves he said he was a happiest man in earth and his mission was complited, that he can now die happy....... did this man succeded?.

au mpaka uwe na nyumba ya kifahari, na magari ya kumwaga..

coz for that guy he believed he was born to write that book.

thx

MJ

He was ambitious and worked hard for it, usiniambie alikuwa kakaa tu mwisho wa siku akajikuta kapublish kitabu!
 
Consultants wengi wanachukua mshiko mzuri sana, so sidhani kama ni sawa kuwalabel kuwa hawajasucced.
Pia watu tunaona hao waliosucced by taking risk lakini hatuoni wote waliofeli
"According to the U.S. Small Business Administration, over 50% of
small businesses fail in the first year and 95% fail within the first
five years.? "


I am searching as to why some people succeed in life while others don't.Why some businesses fail and others thrive?

People who have had just a few years of education are most successiful than many graduates out there! What make the laymen succeed in business which most of the graduates do not have?

This is the point of my discussion.It would assist most of us in finding out what makes a successiful person...

I think your whole notion that people who have less education succeed more is false. I don't think that idea is backed up by any facts, its a myth.
 
Back
Top Bottom